Viatu vya Nyerere na MKapa havimtoshi Rais Wetu


Underlined, kumiriki vitu kwa watanzania sio Tatizo, juulize kidogo anayemiliki ni nani?? Mtanzania au?? historia yake ikoje?? ukipata hayo majibu yake basi utaelewa kwamba bado kuna tatizo

Red:Najua mambo yanabadilika sana kutokana na utandawazi but jiulize huu mfumko wa bei unatoka wapi???
 
ukiona mtu anakimbilia ikulu mwogopeni sana kama ukoma,mi nimekaa sana pale kuliko maraisi wote wajao maana katiba yetu imesisitiza mwisho kumi rabdaa atokee kaditekta hapo kati,...jamani anaejua ikulu vizuri uwezi ukakimbilia hata siku moja ikuru ni mzigo,..ukipita njian unaona omba omba ure mzigo wako....lakini watu awajui hirooo embu jiulizeni mtu anaenda ikuru kwa kumwaga fwedha...ikuru kuna biashara gani pale,..mi nimekaa miaka 25 sijaona biashra yoyote ya kufanya ikuru...jiulize huyuy anagawa pesa ili aingie madarakani akiingia atalipaje,..?na kama alikopa kwa watu atawaripaje???hii ni raana,..ikulu si sehemu ya biashara hata siku moja..pare ni mahari patakatifu....lazima watu wapaheshimu...... Mwenye akiri timamu awezi kukimbilia ikulu hata siku moja...na ukiona mtu anamwaga fedha kuinga ikuru mwogopeni kama ukoma..wallahi nawaambia ipo siku mtu huyu atawaauza watanzania kuripa m,adeni yarimwingiza madarakani ndio maana chama kilikubaiana yoyote anaeingia kwenye kampeni ya urais akiwa na pesa yake tukatae kama ukoma...lazima tujiurize huyu mtu anaapata pesa wapi???ana biashara gani ya kumwaga pesa???na je atajilipaje??? Kuna mambno mengi sana ikulu mengine nashindwaa kuwaambiaa ,,,haaaa haaa aapana apana mliopata yanatosha ahsanteni tutaonana tena mungu akijalia WASAA WA MAREHEMU JK NYERERE TUKIELKEA UCHAGUZI
 
Well said bro.
Unajua kutokana na status ya Mwalimu, tunaji censor kuzungumza mapungufu ya uongozi wake hasa katika nyanja za uchumi. Alitaifisha viwanda na makampuni yote yakafa kutokana na aidha mfumo wa kutozingatia biashara[over-employment and mismanagement] yakafa yote. Appointments nyingi zilizingatia ukada badala ya competence[maoni yangu] Ilifikia mahala nchi ina upungufu wa kila kitu, hatukopesheki, hatuna hela [foreign reserve zero] na nchi ilikuwa inaenda on month to month basis. Mwishowe marafiki zetu wakaanza kutuchoka [NORDIC countries]. Hivyo mzee rukhsa alipo ingia madarakani the country was literaly broke. Leo tunawaponda kina Mkapa na Kikwete. Ukweli ni kwamba kila kiongozi alikuwa na changa moto zake [Mwalimu -kuleta umoja wa kitaifa/Ukombozi wa Afrika-Mwinyi kujenga misingi ya uchumi huria [as the world dictates] Mkapa kufufua uchumi na kulipa madeni -Kikwete kuendeleza democracy na kuendeleza fito za kujenga uchumi na uwekezaji ingawa ameingia madarakani kukiwa na changamoto nyingi-kwanza ukame halafu nishati, mikiki ya world wide recession ambayo imepelekea bei ya bidhaa tunazozalisha kuanguka vibaya sana na mengine mengi. Jamani hiyo si kazi ndogo Mnyonge mnyongeni lakini haki mpeni.
Hivi sasa kila anachofanya JK kinapondwa inachosikitisha ni kwamba nilitarajia wasomi ambao wanaweza kuchambua mambo kuliko sisi mambumbumbu wangezungumzia pros and cons lakini nao wameingia mtegoni kwa kuponda kila kitu.
Katika mizunguko yangu vijijini jinsi wanavyomuona JK ni tofauti kabisa na sisi urbanites. Haitokuwa la ajabu kama hawatamrudisha kwa kishindo. Sasa ikiwa hivyo tuseme wao ni wajinga au wanauelewa kuliko sisi urbanites??????
 
Alnadaby umenikumbusha operation vijiji vya ujamaa watu wengi walipoteza maisha mali zao nyumba aridhi nzuri lakini naona hiyo story imesahaulika kabisa wengi waliopo hapa JF nafikiri ni kizazi cha Mwinyi miaka ya 80 hawakuwepo wakati wa operation vijiji ilikuwa ya kinyama zaidi ya ile ya Pemba

lakini kwenye red napingana na wewe kati ya viongozi wetu wa kitaifa aliyefanya kazi kubwa ya kuiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia ni Nyerere kumbuka Tanzania ya kabla ya vita na Uganda mambo yalikuja kuharibika baada ya vita miaka ya 80-83 sababu inajulikana lakini kipindi hiki mambo yanazidi kuwa mabaya bila sababu ya msingi kuwa na TV tu hakuwezi kunifanya nione ni sababu kubwa kwa nchi kuwa imeendelea

ukiniambia leo niwa rank marais wetu kwa ubora nitaanza na Nyerere then Mkapa then Kikwete lastly Mwinyi na ninaweza ku substantiate kwa kila mmoja kwa udhaifu na ubora wake kumzidi mwingine lakini si kuwa Kikwete ni bora kuwazidi wengine
 


Tunaomba utupe mchanganua kwa nini unawarank kihivyo kwa mtazamo wako na si vinginevyo???
 
Tunaomba utupe mchanganua kwa nini unawarank kihivyo kwa mtazamo wako na si vinginevyo???
Mwenye macho haambiwa tazama na ili ujue unakwenda wapi inabidi kwanza utambue uko wapi na unatoka wapi.
 
Mwenye macho haambiwa tazama na ili ujue unakwenda wapi inabidi kwanza utambue uko wapi na unatoka wapi.

Am sorry kama nimeweka maelezo yangu vibaya na sina nia mbaya na mchango wa LUTENI but nilitaka kujua kwanini anawarank hivyo?? Tuko pamoja??
 
Ukizungumzia uchumi wa Nyerere huwezi kuutenganisha na vision yake ya Ujamaa na Kujitegemea kutaifishwa kwa viwanda ilikuwa ni implimentation/application ya vision yake na alikuwa sahihi kwa kipindi hicho angalia siasa zake za kutofungamana na upande wowote angalia stance yake juu ya utawala wa Makaburu SA angalia stance yake juu ya Israel angalia Azimio la Arusha ambalo sasa viongozi wengi ndio wanaanza kuona umuhimu wake hakuyumbishwa

changamoto alizokuwa nazo Mwalimu sioni kiongozi yeyote Tanzania leo anayeweza kulinganishwa naye Mwl alikuwa na uwezo wa kuzungumza na kusikilizwa hata baraza la UN

katika suala la demokrasia ingawa Nyerere alikuwa na ka udikteta lakini si kama wa Idd Amini udikteta wa kufanya kazi alitaka ufanye kazi kama anavyotaka yeye alikuwa na uwezo wa kumuita mtu yeyote siku yeyote kitu ambacho kiongozi wetu wa sasa hana hizo ni weakness zao wote

kuhusu kuchaguliwa au kutochaguliwa kwa Kikwete hilo halina wasiwasi atachaguliwa lakini hiyo haiondoi weakness yake inategemea na mfumo wa uchaguzi hata Nyerere kwa mfumo wake alikuwa anachaguliwa kwa asilimia 90-98 mfumo una legalize matokeo lakini hau legitimatize matokeo
 
ndio maana anapenda aitwe jk kwa kuwa anaweza kuvivaa viatu vya nyerere............ila ukweli jk nyerere alikuwa kiongozi exceptional kabisa.................hili la jk kujiita jk lilichangi a pia watu kumwamini kwani rai walikuwa wameshakata tamaa.....................sasa hali ni mbaya kumbe ilikuwa danganya toto tu..............
kazi ipo
 

Watanzania wamepumbazika na JK bila kuangalia nani JK, siku zote watanzania tumezoea kudanganywa tukiambiwa ukweli tunaona huyo mtu hafai, tunaelekea wapi
 


Nyerere is the best president so far and Mwinyi is the worst!! mimi nilioa wakati wa Mwinyi kwa harusi kubwa, nikajenga wakati wa Mwinyi, nikanumua magari mawili wakati huo lakini najua ilikuwa to the expenses of Walala hoi! That man was hands off, minds off na nchi tuliendesha sisi tuliokuwa na meno ya kutafuna!

Mwinyi aliwaumiza sana watanzania lakini wachache tulifaidika na tuliweza kupata chochote hata kama tungehitaji kichwa cha mtu!!

Nyerere alitujengea heshima sana watanzania, uzalendo na utaifa viliimarishwa na watu walijivunia kuwa watanzania kinyume na wakati mwingine wowote.

Huyu wa sasa yuko juu ya Mwinyi lakini viatu vya Mkapa na Nyerere hawezi kuvivaa, vitampwaya sana.
 

Sasa tutamsadiaje mkubwa wetu viatu viweze kumtosha???
 
Kwenye suala la uongozi, Mzee Ruksa alikwisha wahi kusema kuwa kila awamu na zama zake, na akalinganisha na kitabu kuwa kila kitabu na "chapter" yake. ukitaka chapter zifanane basi huna haja ya kuwa na kitabu.

Kwa kuendeleza fikra hizo ninasema hivi mvua za masika miaka yote hazifanani, za mwaka jana siyo za mwaka huu na kwa mantiki hiyo kila kiongozi anakutana na changamoto tofauti za kiutawala na hivyo anachokifanya ni cha wakati huo na kuwalinganisha akina Obama na George Washington au akina Ronald Reagan utakuwa unachemsha tu.

Mwacheni JK afanye kazi na amalize yale aliyoyakuta na kuboresha yale aliyopanga kuyafanya.
 

Mkuu sun Tzu nakubaliana na wewe lakini mipango ya muda mfupi na muda mrefu ya mheshimiwa katika kusukuma gurudumu la nchi siioni, au BADO TUNATEMBELEA KWENYE UZI WA BWANA MKAPA??
 

Jamani,

Mimi naona Mkapa ndiyo worst president ever! Mwizi (kiwira coal mine etc.), na kasaidia hata wageni kutuibia (NBC, Madini etc.) ..... sioni kitu kizuri cha kusema kuhusu Mkapa

Ukijaribu kuweka uwiano, so-called "kupaa kwa uchumi" wakati wa Mkapa haufui dafu kwa madhara aliyotuletea waTZ through uwekezaji na ubinafsishaji.
 


Mkuu kiwalani, Jamani kusema kweli mkapa alifanya madudu mengi but mazuri yake yameonekana aliweza kukuza uchumi wetu, kipindi kile wenye vipato halali walionekana ANGALIA SASA HIVI HELA ZA KIMAGUMASHI ZINAVYOCHAFUA UCHUMI WETU
 
Mkuu kiwalani, Jamani kusema kweli mkapa alifanya madudu mengi but mazuri yake yameonekana aliweza kukuza uchumi wetu, kipindi kile wenye vipato halali walionekana ANGALIA SASA HIVI HELA ZA KIMAGUMASHI ZINAVYOCHAFUA UCHUMI WETU

Mkuu King of Kings,

Hao wenye vipato halali uliowaona wewe ni akina nani??!! ...... mimi nilishuhudia NBC, na mashirika mengine "yakipigwa bei" ya kutupa, na pesa iliyopatikana ikaingizwa kwenye mahesabu ya wachumi na kusema uchumi umepaa na kwamba shilingi imepanda chati ... lakini fact is hakuna uchumi uliopaa; hayo mashirika yaliuzwa kwa bei za chini sana na mikataba mibovu ya madini ilisainiwa; ambapo wanaofaidi ni Barrick na ndugu zao na sisi kule Geita na Kahama tunaambulia mashimo, na kule North Mara ndugu zetu wanakufa kwa maji yenye sumu (cyanide).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…