Video Assistant Referee (VAR) Ni TV tu inayowekwa uwanjani lakini wanaohukumu wanakuwa hawapo uwanjani

Video Assistant Referee (VAR) Ni TV tu inayowekwa uwanjani lakini wanaohukumu wanakuwa hawapo uwanjani

Song of Solomon

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2021
Posts
2,752
Reaction score
5,609
Video Assistant Referee (VAR) Ni TV tu inayowekwa uwanjani lakini wanaohukumu wanakuwa hawapo uwanjani na huwezi kuongea nao wewe au kuwaona isipokuwa Referee akipitia kwenye mawasiliano,

mfano VAR ambayo itatumika kwa mkapa leo, mitambo iko UINGEREZA REFA Analetewa picha kwenye TV yake kupitia internet protocol interface

VAR inatumia Camera 33 kati ya hizo ni Camera 8 ambazo zenyewe kazi yake ni kupunguza kasi ya matukio (slow motion) na matukio yaliojificha kama migongano viwiko N.K na Camera 4 zinapunzuza kabisa kasi kwa kiasi kidogo sana na hizi zinashirikiana na Camera mbili za kuona offside kwa kutumia technologia inayoitwa (Hawk-Eye's virtual offside line technology)

ili kumuwezesha refari kukagua matukio kwa usahihi kwa msaada wa jopo la watu watatu wanahusika kurudisha matukio kwenye VAR. VAR IPO UINGEREZA kwenye kituo kinachoitwa Stockley Park, west London ambacho kina control matukio yote ya mpira ambayo inachezwa chini ya VAR.

VAR imetengenezwa na SHIRIKA LA MPIRA LA Royal Netherlands Football Association (KNVB).

VAR zinakadiriwa kwa msimu' mmoja zinalipiwa kiasi cha Dollar MILLION sita na MILLION miambili 6.2M

Tangu VAR ianze imesha chunguza matukio 2400 na matukio 109 tu ndio yalikataliwa kuwa sio sahihi.

Mwisho kabisa Referee ndie mtoamaamzi wa mwisho kwenye maamzi yake hata kama VAR imeamua kuwa kosa, yeye anaweza akakataa. Lakini atahukumiwa na umma kwakuwa kila mtu anaona tukio kwenye runinga yake ndio maana wako makini sana. Kutoka kituo cha utafiti cha

#VAR
 
Neno uwanjani una maanisha ndani ya pitch au hata kwenye vyumba vilivyopo hapo uwanjani? Ligi zingine mfano la liga kabla ya mechi kuanza wanawaoonyesha walioko VAR room, je hao wanaoonyeshwa wanakuwa hawapo kwenye chumba cha hapo uwanjani?
 
Neno uwanjani una maanisha ndani ya pitch au hata kwenye vyumba vilivyopo hapo uwanjani? Ligi zingine mfano la liga kabla ya mechi kuanza wanawaoonyesha walioko VAR room, je hao wanaoonyeshwa wanakuwa hawapo kwenye chumba cha hapo uwanjani?
Sio kwenye pitch
 
Sio kwenye pitch
Mitambo ya VAR ndo iko Uingereza na wale officials wake au VAR Officials wana chumba chao maalum pale uwanjani na kazi yao ni kutafsiri matukio kutoka kwenye hiyo mitambo iliyoko Uingereza?! Jamaa ana hoja ya msingi sana hapo juu maana kama kweli VAR Officials wako iliko hiyo mitambo basi hiyo room itakua kubwa kama mkoa wa Morogoro maana mechi zinazotumia VAR ni nyingi sana per day na maOfficials hawawezi kuamua matukio ya mechi zote zinazochezwa duniani per time zinazotumia VAR
 
Nyongeza: Laliga kabla ya mechi hua wanaonesha VAR Room ikiwa na hao Officials na mitambo yao ya computers, swali la msingi hapa ni kwamba hua wapo hapo uwanjani au wana centre yao sehemu nyingine au wanakua kule iliko hiyo mitambo Uingereza?!
 
Nyongeza: Laliga kabla ya mechi hua wanaonesha VAR Room ikiwa na hao Officials na mitambo yao ya computers, swali la msingi hapa ni kwamba hua wapo hapo uwanjani au wana centre yao sehemu nyingine au wanakua kule iliko hiyo mitambo Uingereza?!

Mtoa mada umekariri, VAR iliyofungwa kwa Mkapa inajitegemea hapo hapo…Ulichokielezea ni VAR ya EPL tyu ambayo inakuwa controlled sehemu moja tu toka viwanja vyote…Hii iliyofungwa kwa Mkapa ni kama ya kombe la Dunia pale Russia, kila uwanja una VAR system yake inayojitegemea na ndiyo maana kuna kuwa na VAR officials kuanzia wanne hadi sita inategemea na maamuz cha chama cha soka
 
... VAR IPO UINGEREZA kwenye kituo kinachoitwa Stockley Park, west London ambacho kina control matukio yote ya mpira ambayo inachezwa chini ya VAR.
Nahisi umeona mahali kuhusu VAR ya EPL basi ukakurupuka kuamnzisha uzi eti VAR ya mechi zote duniani ipo Uingereza. Hapo kwenye kituo si pangekuwa pana ukubwa wa ajabu!
NB: VAR ipo kwa Mkapa, nendeni mkaishangae
 
Mtoa mada umekariri, VAR iliyofungwa kwa Mkapa inajitegemea hapo hapo…Ulichokielezea ni VAR ya EPL tyu ambayo inakuwa controlled sehemu moja tu toka viwanja vyote…Hii iliyofungwa kwa Mkapa ni kama ya kombe la Dunia pale Russia, kila uwanja una VAR system yake inayojitegemea na ndiyo maana kuna kuwa na VAR officials kuanzia wanne hadi sita inategemea na maamuz cha chama cha soka
Soma vizuri mi sio mtoa mada, nimeuliza swali la nyongeza
 
Another one!!
Mwingine aliejaza kamasi kichwani
 
Back
Top Bottom