VIDEO: Demba Ba avunjika mguu

lil wayne

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2016
Posts
992
Reaction score
904
Mashabuliaji wa zamani wa Klabu ya West Ham United ambaye kwa sasa anachezea klabu ya Shaghai Sheghua FC ya uchina amevunjika mguu akiwa katika moja ya mechi katika ligi ya uchina.

 
Ni hali ya kawaida kwa mchezaji kupata injury akiwa uwanjani, hasa kuvunjika mguu kama ilivotokea kwa mchezaji wa Manchester united luke shaw na mchezaji wa chelsea Zouma,

Lakini hali imekua mbaya sana kwa mshambuliaji wa zamani wa Newcastle pamoja na chelsea za england demba ba alimaarufu kama BA ambapo leo kavunjika mguu wake na kutengeneza alama ya Z alipokua anacheza na timu yake ya Shanghai Shenhua inayoshiriki ligi kuu nchini China Chinese Super League.

Mchezaji huyo alianza vema msimu wake ambapo ametupia kambani magoli 14 katika mechi 18 alizocheza


Get well soon BA bado nakumbuka goli ulilotufunga kwenye FA de gea akabaki anashangaa tu
 
Jamaa kaumia vibaya sana, sidhani kama atapona vizuri na kurudi kucheza mpira. Ukizingatia na umri wake umeenda
 
Nimetazama video ya jinsi Demba Ba alivyo vunjika mguu. Sidhani kama jamaa atarudi tena kwenye soka. Mungu amtie nguvu.
 
Jamaa kaumia vibaya sana, sidhani kama atapona vizuri na kurudi kucheza mpira. Ukizingatia na umri wake umeenda
Atapona vizuri japokuwa kasoro ni kasoro. Katika swala la umri ni bayana ana kazi kubwa mbele yake kurudi uwanjani, nampa pole. De Lima aliwahi kuumia zaidi ya Ba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…