Video: Hivi "vetting" hufanyika kweli kabla ya uteuzi wa viongozi? msikilize Kenani Kihongosi akitetea kitendo chake cha kucharaza viboko watu...

The Palm Tree

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2013
Posts
7,951
Reaction score
12,541
Your browser is not able to display this video.

HAPA JAMAA ANAJITETEA BAADA YA KUTENDA NA KUISIKIA JAMII IKIMURUSHIA MADONGO...

Rais John Pombe Magufuli pamoja na kuwa ni aggressive, lakini sijawahi kumwona akishika kiboko kucharaza viboko watu hadharani...!!

Rais John Pombe Magufuli pamoja na kwamba hapendi wahalifu na matumizi mabaya ya rasrimali za nchi ikiwemo fedha, lakini hajawahi kuamuru wahujumu uchumi, watakatishaji fedha ama wezi wa mali ya umma wapigwe risasi ama viboko hadharani..!!

Rais John Pombe Magufuli, huponda na kufokafoka kwa maneno makali na ya kuudhi (sometimes) lakini huamuru uchunguzi kufanyika na hatua za kawaida za kikazi na kisheria kutendeka kwa wanaodhaniwa wamekosa...!!

Huyu DC yeye ni nani hasa hata afanye ujinga kama huu? Kwa kweli simuelewi na sijui kama nitamwelewa...!
Your browser is not able to display this video.

HAPA JAMAA ANATENDA UJINGA, ANATOA HUKUMU...

Laiti kama polisi wangejichukulia sheria mkononi kwa kuwaadhibu wahalifu au washukiwa wa uhalifu sawa na mtazamo na akili za huyu DC, basi mpaka sasa ina maana kusingekuwa na haja ya kujenga magereza na kusingekuwa na wafungwa magerezani maana hukumu ingekuwa inatolewa papo hapo kwenye tukio...!!

Jamii hususani watoto tunaowaandaa kuwa viongozi wa taifa hili baadae wajifunze nini toka kwa kiongozi kama huyu DC anayejitetea kwa ujinga wa tendo lake?....

Je, jamii ijifunze na kuona kuwa kumbe ni sawa watu kujichukulia sheria mkononi kwa wanaowadhania ni "wahalifu" ama "wakosaji" kama alivyofanya DC?..

Kama mtazamo wa DC ndivyo ulivyo, kumbe basi, hakuna haja ya kuwa na mahakama Tanzania...

Baada ya kuona uhalifu huo, kila mtu angetarajia kumuona DC akiamuru watu hao anaodhani ni wahalifu ama wezi wakipelekwa mahakamani na kuadhibiwa kwa taratibu za kisheria..

Lakini hapa, looh, DC anadhani yuko juu ya sheria kwa kujiamulia yeye mwenyewe kutuhumu, kushika na kusikiliza kesi na kisha kutoa hukumu (adhabu) ya kuwapa....!

Sijui ni kwanini tu huyu DC mpaka sasa bado yuko ofisini maana amekosa sifa za kuwa kiongozi ktk nafasi hiyo asilani...!!
 
Nchini argentina Ukiwa na moja ya sifa hizi tegemea teuzi anytime
.Kabila pendwa
.Rangi pendwa
.Kuwadhalilisha, kuwashughulikia wapinzani
.Kusifu na kuabudu
. Kukubali kupigwa chapa 666
. Kuisujudia Sanamu.
Huyo bwana ushahidi ingia youtube akiwa Iringa alitishia kuwauwa wapinzani akapewa teuzi.
 

Kwa hiyo tunafuata njia ya Argentina, right?

Kwa hiyo hata mungu aliyeiondoa CORONA kumbe ni mungu wa 666, right?

Duuh, mimi siko huko, sitaki kabisa kwenda huko...!
 
Nimemuelewa sana kuna watu wanakera sana chapa tu, walichofanya hao jamaa ni ujinga unaokera mno.

Tena angewatandika na wire ndio ingefaa zaidi badala ya fimbo.
 
kuchapa viboko ni ishara kua bado jamii yetu iko kwenye primitive stage,in modern days the most human degrading and embarrassing punishment ni kuchapana viboko hadharani.

.....and this is done by a reputable high govt leader. It's a shame that, we are led by primitive leaders like this DC...
 
Vetting huangalia historia na hutumika kutabiri tu kuwa huyu atatufaa na blaa blaa nyingine ila haijui future itakuwaje. Ndio maana watu hufanyiwa vetting ila baada ya madaraka watu hugeuka.
 
Vijana waaache kupenda kiki na sifa,,huyo kapenda sifa tuu,,moyoni alijua kabisa kuwa huo anafanya ni upumbavu.
 
Jiulize kwa nini Raisi Magufuli hajatengua uteuzi wake ? Mbona wengine hata kama ni Jumapili au sikukuu utasikia katenguliwa mara moja, maana yake ni kwamba Raisi wa nchi mwenyewe angefanya hivyo hivyo, huyo DC mnamuonea tu lkn aliyewachapa viboko hao Watanzania ni Raisi Magufuli mwenyewe, so sad, unapokuwa na Raisi wa nchi ambaye kwa kawaida anapaswa kulinda na kuwatetea Wananchi yeye ndiye wa kwanza kuonea, kudhalilisha mtu mweusi, Raisi Magufuli atashindwa na hatofanikiwa kama anaonea Watanzania, Mungu atamlaani na kumuadhibu.

Mahakama peke yake ndiyo inayopaswa kuhukumu, kama hao Watanzania walifanya makosa kuna polisi, wangewakamata na kuwafikisha Mahakamani na hukumu kutolewa kwa mujibu wa Sheria zetu, ...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…