VIDEO: Sakata la Halima Mdee na wenzake 18 waliokuwa wanachama CHADEMA kufutiwa uanachama; Je, kuna anayemwelewa Spika Ndugai hapa?

VIDEO: Sakata la Halima Mdee na wenzake 18 waliokuwa wanachama CHADEMA kufutiwa uanachama; Je, kuna anayemwelewa Spika Ndugai hapa?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2013
Posts
7,951
Reaction score
12,541


Mengine yaliyopita yote tunayaelewa...

Hapa nimerudia kumtazama na kumsikiliza mara mbili tatu, sijafanikiwa kumwelewa kabisa. Kwangu mimi namuona kama mtu aliye "so desperate and confused". Hajali sheria wala taratibu ama katiba ya nchi tena...

Spika Ndugai na wenzake huko CCM chini John Pombe wanataka wapate chochote kwa njia yoyote haramu ama halali. Wako tayari kutoheshimu sheria na katiba ya nchi waziwazi kabisa...

Spika Ndugai anaagizwa na Jiwe "ku - abuse mamlaka na madaraka yake ya uspika" kwa kukanyaga kanyaga katiba na sheria za nchi mchana kweupe na bila hofu anatenda.

Hii imenitisha sana.

Kila mtu anajua kuwa CHADEMA ni chama cha siasa halali kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi yetu. Kina katiba na utaratibu wake wa kujiendesha na kujisimamia.

Ndugai na wenzake hasa Magufuli hawaipendi CHADEMA. Lakini kwa yeye Ndugai, sijui anaona taabu gani ingalau kuheshimu hilo tu la uwepo wa CHADEMA kisheria na kikatiba.

Akifanya hivi, na yeye ataheshimika na ataendelea kutenda na kutekeleza majukumu yake ya Uspika hata kama na sisi wengine hatumpendi.

Anamsema mwenzake Mbowe kuwa anatukana wanawake (sijui hata kama ni kweli).

Cha ajabu yeye anatukana na kuonesha dharau ya waziwazi kwa CHADEMA yote, wanachama na wafuasi wake wote mamilioni kwa mamilioni Tanzania na duniani note.

Kwa dharau kabisa Ndugai anapiga propaganda za kijinga kuwa CHADEMA ni kama kampuni ya mtu binafsi..

Mtu mwenye akili anaweza kujiuliza hivi;

Kama CHADEMA ni "kampuni ya mtu binafsi", ina maana hao anaowaita " wabunge" na kusema atawalinda, hajui kuwa watakuwa pale wakiwa na dhamana ya chama hichohicho anachokiita "kampuni binafsi ya mtu?"

Maana siyo kwamba hakitambui chama. Yeye hatambui kufutwa kwao uanachama tu.

Hakika Ndugai haeleweki. Yuko very frustrated.

Baadaye Ndugai ameendelea kusema, hatawatambua hawa kuwa ni "wabunge halali" iwapo tu kutakuwa na "sababu halali za kikatiba..."

Baada ya kusikia hili nikachoka kabisa. Nikajiuliza huku ni kuchanganyikiwa au ni kukosa ufahamu...?

Hivi ina maana Ndugai hajui sifa za kikatiba za mtu kuwa mbunge?

Na je, hivi huyu mzee ina maana hujui pia sifa za mtu kukoma au kukosa uhalali wa kuwa mbunge wa Bunge la JMT ambalo yeye ndiye kiongozi wake...?

Ningemwona wa maana sana kama angewashauri kina mama hawa kutumia njia za kisheria kudai haki yao ya uanachama (kama wanadhani au ona kuwa wameonewa) ndani ya chama au mahakama..

Lakini anachotenda Spika ni mbaya sana. Anaacha precedence mbaya sana kwa watoto wetu na mfumo wetu wa utawala...
 
Msimu wa mvua ndio huu.. usije ukalalamika wakulima tunapandisha bei..
 
Imenibidi nirudi katika video ya Freeman Mbowe, nitafute ni sehemu gani alipotoa tamko la kuwafukuza ubunge hao wanawake 19, sikupaona wala kupasikia. Alichotamka ni kuwavua nyadhifa zao ndani ya Chadema na kuwavua uanachamawa Chadema. Sasa hayo ya kuvuliwa ubunge yanatoka wapi? Hivi huyu Ndugai ni mzima kweli jamani?
 
Kwa kusema chadema ni kampuni binafsi ni kwamba hicho chama hakina hadhi ya kutoa wabunge wa viti maalum sababu ni Mbowe ndiye atachagua na sasa kama hana Sifa hao akina Mdee wanapata Sifa wapi ya kuwa wabunge kama CHADEMA ni kampuni binafsi.

Pia kwa kauli hiyo aliyoitoa akina Halima Mdee hawawezi kudai uanachama kwenye kampuni binafsi kama wanataka kuwa wanachama cha Siasa waende CCM kwenye chama cha Siasa hawawezi kuwa bungeni wakitokea kampuni binafsi.

Kuhusu Nusrat hivi kwanini alikuwa mahabusu kwa siku 130 kama hiyo seriakali ya CCM inawajali wanawake kosa alilokuwa ametenda na kusababisha kukaa huko mahabusu ni lipi hasa maana kama hakuwa na kosa lolote ni nani alimuweka huko na kwa faida ya nani na anafanywa nini huyo alimfanyia huo unyama.

Kuhusu hiyo huruma kwa Halima Mdee alipokuwa anasema huyu sitaki kumuona katika bunge hadi mwaka kesho alikuwa siyo mwanamke wakati huo alipokuwa anatolewa bungeni kwa kuonewa bila ya kosa sababu ni mwanamke wa upinzani.

Kule kupigwa magereza na kuvunjwa walivunjwa sababu ya mbowe kwani Mbowe alikuwa kafanya nini hadi wao wavunjwe Mbowe ndiye aliyewagombeza magereza wakaanza kuwapiga wanawake

Sijamuelewa spika naona kama anatakiwa aende tena India vile maana anavyoongea wabunge wamepigwa na askari magereza yeye kama spika alichukiwa hatua gani kwa wabunge wanawake kuvunjwa na askari magereza.

Inakuwaje anaanza kupata uchungu sasa hivi baada ya muda mrefu kupita, lakini kipindi wanapigwa alikuwa anachekelea sababu wamekwenda kumpokea Mbowe ambaye ndiye mbaya wao. Kosa la Mbowe ni kuwa na chama ambacho siyo cha kutumia kupata misaada ni chama chenye nia ya kuongoza nchi.

Hivi CCM kuna demokrasia huko ambako Magufuli huwa anasema yeye ndiye atachagua Rais akina Lukuvi na Kabudi hawawezi kuwa marais kwasababu yeye ndiye mwenye uwezo wa kuchagua Rais wa nchi hii kuna demokrasia gani. Hivi wakati wanamfukuza Membe walimfukuza kwenye kikao gani siyo kamati kuu japo CCM chombo chenye mamlaka ya kufukuza ni Halmashauri kuu mbona Membe walisema wamemfukuza kwenye kamati kuu kama CHADEMA.

Hivi mpaka msajiri wa vyama akakisajiri na kukipa usajiri wa kudumu hakuchunguza kama ni chama cha Siasa au ni kampuni ya mtu mmoja kama anavosema yeye chama kikuu cha upinzani anasema ni kampuni ya mtu binafsi. Ndugai amewadhalilisha sana wanachama wa CHADEMA katika nchi hii anatakiwa kuwaamba radhi vinginevyo wanasheria wa CHADEMA wampeleke mahakamani ili apunguze kuropoka ropoka hovyo.
 
Mambo ya gereji hayo... Kujitukanisha gereji ndio ujanja.
 
Huwezi kumuelewa mwehu. Ni abnormal huyo. Kumwita spika ni aibu kwa JMT. Labda tutumie neno subwoofer kuvicha aibu. Kiranja wa watunga sheria asiyejua sheria ni kinyaaa.
 
KAULI HII

Mengine yaliyopita yote tunayaelewa...

Yaonesha Ipo siri kubwa kwa sentensi hii tungoje tu tutajua mengi sababu spika hawezi kukaa na jambo moyoni, hii ndio khurka yake
 
Lakini anachotenda Spika ni mbaya sana. Anaacha precedence mbaya sana kwa watoto wetu na mfumo wetu wa utawala...
That's the worst effect, anadhoofisha utawala wa sheria na Katiba.

Kamdhalilisha Msekwa eti ana kumbukumbu ya mambo ya zamani ambayo yamebadilika. Katiba ya 1977 imebadilika ????

Halafu anasema waandishi wamemchukua Msekwa out of context. Waandishi wametuchezeshea clip ya Msekwa kama ilivyo, waandishi hawajasema chochote!

Kamgwaya Msekwa kawachimba biti waandishi!
 
View attachment 1638728

Mengine yaliyopita yote tunayaelewa...

Hapa nimerudia kumtazama na kumsikiliza mara mbili tatu, sijafanikiwa kumwelewa kabisa...!

Kwangu mimi namuona kama mtu aliye "so desperate and confused". Hajali sheria wala taratibu ama katiba ya nchi tena...

Spika Ndugai na wenzake huko CCM chini John Pombe wanataka wapate chochote kwa njia yoyote haramu ama halali..!

Wako tayari kutoheshimu sheria na katiba ya nchi waziwazi kabisa...

Spika Ndugai anaagizwa na Jiwe "ku - abuse mamlaka na madaraka yake ya uspika" kwa kukanyaga kanyaga katiba na sheria za nchi mchana kweupe na bila hofu anatenda...

Hii imenitisha sana.

Kila mtu anajua kuwa CHADEMA ni chama cha siasa halali kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi yetu. Kina katiba na utaratibu wake wa kujiendesha na kujisimamia...

Ndugai na wenzake hasa Magufuli hawaipendi CHADEMA. Lakini kwa yeye Ndugai, sijui anaona taabu gani ingalau kuheshimu hilo tu la uwepo wa CHADEMA kisheria na kikatiba...

Akifanya hivi, na yeye ataheshimika na ataendelea kutenda na kutekeleza majukumu yake ya Uspika hata kama na sisi wengine hatumpendi...

Anamsema mwenzake Mbowe kuwa anatukana wanawake (sijui hata kama ni kweli)...

Cha ajabu yeye anatukana na kuonesha dharau ya waziwazi kwa CHADEMA yote, wanachama na wafuasi wake wote mamilioni kwa mamilioni Tanzania na duniani note...!

Kwa dharau kabisa Ndugai anapiga propaganda za kijinga kuwa CHADEMA ni kama kampuni ya mtu binafsi..

Mtu mwenye akili anaweza kujiuliza hivi;

Kama CHADEMA ni "kampuni ya mtu binafsi", ina maana hao anaowaita " wabunge" na kusema atawalinda, hajui kuwa watakuwa pale wakiwa na dhamana ya chama hichohicho anachokiita "kampuni binafsi ya mtu..?"

Maana siyo kwamba hakitambui chama. Yeye hatambui kufutwa kwao uanachama tu...!!

Hakika Ndugai haeleweki. Yuko very frustrated...

Baadaye Ndugai ameendelea kusema, hatawatambua hawa kuwa ni "wabunge halali" iwapo tu kutakuwa na "sababu halali za kikatiba..."

Baada ya kusikia hili nikachoka kabisa. Nikajiuliza huku ni kuchanganyikiwa au ni kukosa ufahamu...?

Hivi ina maana Ndugai hajui sifa za kikatiba za mtu kuwa mbunge?

Na je, hivi huyu mzee ina maana hujui pia sifa za mtu kukoma au kukosa uhalali wa kuwa mbunge wa Bunge la JMT ambalo yeye ndiye kiongozi wake...?

Ningemwona wa maana sana kama angewashauri kina mama hawa kutumia njia za kisheria kudai haki yao ya uanachama (kama wanadhani au ona kuwa wameonewa) ndani ya chama au mahakama..

Lakini anachotenda Spika ni mbaya sana. Anaacha precedence mbaya sana kwa watoto wetu na mfumo wetu wa utawala...
Ili aonekane anawatetea kweli awarudishie ua nachama wa chadema kama kweli ana mamlaka hayo. Kwa sasa si wanachama
 
Back
Top Bottom