Uchaguzi 2020 Video: Wananchi Same waandamana kupinga jina la mgombea waliloletewa na CCM

idawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2012
Posts
25,284
Reaction score
38,364
Wananchi wa kata ya Mbwambo Wilaya ya Same Mkoa wa Kilimanjaro wameungana na viongozi wao kupinga jina mgombea Udiwani lililorudishwa na Chama Cha Mapinduzi

Wananchi hao wakiwa na mabango mbali mbali ya kuwasihi viongozi wa CCM Taifa kuingilia kati sakata hilo wamemtaka Rais Magufuli aingilie kati.

Jina lililorudishwa alikuwa mshindi wa pili alipata kura 83 dhidi ya 117 za aliekuwa mshindi.

Diwani huyo ambaye hatakiwi na wananchi ameongoza kata hiyo kwa miaka 15 mfululizo

 
Kule mkoa Kilimanjaro ,CCM Kama haitambadilisha mwenyekiti wa ccm wa mkoa huo.kutakuwana matatizo makubwa mno ndani ya CCM.
 
Lissu alikwishasema, "Wakimaliza kwetu watakuja kwenu"

CCM wamezowea kupinduwa matokeo ya wapinzani wao sasa wanapinduana wenyewe!

Mafunzo ya Mungu yanasema, "Dhulma haidumu na itakapodumu basi inaangamiza" Hiyo ni Karma ya dhulma muliyoifanya CCM kwenye chaguzi zilizopita. Huyo mwenyekiti wa mtaa analalamika nini wakati yeye mwenyewe yuko hapo kwa dhulma!
 
Wafanye kweli wachague wa upinzani.
 
Wafanye kweli wachague wa upinzani.
Usikute Upinzani hauna nguvu maeneo hayo hivyo wanaamua kutoa kilio chao hadharani sababu hawani mbadala.
 
Reactions: BAK
 

Attachments

  • Vurugu zimeibuka katika ofisi za Chama cha Mapinduzi ( CCM) Wilaya ya Dodoma baa ( 750 X 750 ).mp4
    7.3 MB
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…