SI KWELI Video ya Ng'ombe akiendesha baiskeli

SI KWELI Video ya Ng'ombe akiendesha baiskeli

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2

Naomba msaada wa kuhakiki video hii kama ni ya kweli au imetengenezwa


1722584363425.png
 
Tunachokijua
Ufuatiliaji wa JamiiCheck umebaini kuwa Video ya ng'ombe anayeendesha baiskeli iliwekwa mtandaoni tangu Julai 26, 2024 katika mtandao wa Instagram kwenye akaunti inayoitwa Sirwan.Maghded tazama hapa.

Upi ukweli wa taarifa hii?

Katika kufuatilia ukweli wa taarifa hii JamiiCheck iliichapisha video hii kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii ambapo asilimia 90 ya wadau walieleza kuwa video hiyo si halisi na imetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya Akili Mnemba (Artificial Intelligence). Wadau hapo wa Mitandaoni walitoa vigezo mbalimbali vinavyoifanya video ya ng'ombe kuwa ya Akili Mnemba:

Mathalani, Mdau wa Instagram anayetumia jina la Sharman_smn alieleza kuwa video hiyo si halisi na imetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya Akili Mnemba. Katika kufafanua zaidi hoja hii Sharman_smn ametoa hoja 6 zifuatazo:

Video hii ni feki kwa sababu
1. Miguu ya nyuma nayo inazugusha pedal wakat hakuna kitu hicho kweny hiyo baiskeli, Usukani unatengana na main body katika muda fulani hivi. Huyo ng'ombe ana miguu mitatu tu, mguu wa nyuma upande wa pili wa baiskeli hauonekani, 4. Baiskeli haina kibao cha kukalia au kimingia tumboni?
Hakuna uwiano wa uzito wa Ng'ombe na uwezo wa baiskeli baiskeli, kimuonekano Baiskeli hiyo ni ya kawaida ya kutembelea ambapo wastani wa uzito inayiweza kuhimili ni 140kg, ng'ombe wa muonekano huo haapungui 600kg, so baiskeli haiwezi kusupport uzito huo
Kwa kipengele hicho hicho cha uwiano wa uzito na uwezo wa baiskeli kuhimili uzito, Hata kaka baiskeli ingeweza kubeba uzito huo basi magurudumu yake yasingeweza kuzunguka kwa speed hiyo, mwendo ungekuw wa kudorora sana na kungekuwa na ugumu wa kuepush pedals. Mambo ni mengi ila nafasi ya kuandika haitoshi. Ila Kwa ufupi hiyo ni video iliyozalizalishwa na akili mnemba (AI)

1722582763679-png.3059229

Maoni ya Sharman_smn kwenye akaunti ya Instagram ya JamiiCheck
Maoni ya Sharman_smn hayotofautiano na wadau wengine ambao nao wanakuballiana video hiyo sio halisi bali imetengenezwa kwa teknolojia ya Akili Mnemba. Baadhi ya maoni hayo yatazame kwenye picha hapa chini:

1722583455076-png.3059234

Maoni ya CamiliusMlagala Intagram
1722583880784-png.3059251

Maoni ya Eliaqim Xavery Maramoja (Mdau wa FaceBook)
Nini mtazamo wako kuhusu majibu haya ya wadau wa JamiiCheck?
Video ya ng'ombe akiendesha baiskeli sio kweli .uchunguzi wangu nikishirikiana na mdau anaetumia tumia mtandao wa TIKTOK kwa Jina LA SIRYOYA🏀🏀imeonesha video hii ni mojawapo ya video zinazotengezwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa VFX yaani visual effects au kwa kutumia artificial intelligence kwa ajili ya burudani na hazina ukweli wowote wa kisayansi na kimaumbile kulingana na uchunguzi uliofanywa na tovuti kama FACTLY, AFP FACT CHECK imeonesha video hiii iliundwa kwa ajili ya burudani na utani haukuwepo na ukweli wowote pia kuonekna miguu ya nyuma pia ilikuwa ikiendesha pasina sababu.hivyo ni muhimu kuhakiki taarifa kama hizi kabla ya kusambaza au kuiamini.ahsante Jamiicheck
 
Back
Top Bottom