Vifaru weusi nane wafa Kenya

Billy the Goat

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2013
Posts
566
Reaction score
353
Serikali ya Kenya imesema Vifaru hao walikufa kutokana na kunywa maji yenye chumvi nyingi.

Madaktari wa mifugo kutoka Idara ya Huduma kwa Wanyamapori ya Kenya (KWS) wanaamini kadiri wanyama hao walivyokunywa maji hayo ndivyo walivyozidi kuwa na kiu mpaka kufikia kupata Salt Poisoning

Vifaru hao nane ni Kati ya kundi la vifaru 14 waliokua wakihamishwa kutoka hifadhi ndogo ya Nairobi kwenda Hifadhi kubwa ya Tsavo East, ikiwa ni katika jitihada za kuwalinda Kwa kua vifaru weusi wapo katika kundi la wanyama walio hatarini kutoweka, huku Idadi ya Duniani ikikadiriwa kua chini ya Vifaru 5,500, wote wakiwa bara la Africa, huku 750 Kati Yao wakiwa nchini Kenya.

Vifaru wengine Tisa wa Aina hiyo waliuwawa mwaka Jana huko huko Kenya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…