Elections 2010 Vifijo na nderemo vya tawala kwenye ngome ya Chadema Mlimani

KIDUNDULIMA

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2010
Posts
966
Reaction score
540
baada ya ya post yangu ya vilio na kusaga meno vya tawala ngome ya chadema pale mlimani, kuna watu walidiriki kusema mimi nia yangu ilikuwa mbaya kutoa taarifa ile eti nafurahia watu kukosa haki yao ya kupiga kura. Ukweli ni kuwa post ile ilisaidia sana watu wengi kutoa mawazo yao ya nini kifanyike ili kuwasadia watu wasipoteze haki yao ya kupiga kura. Wengine wenye influence walikwenda mpaka tume ya uchaguzi ili itoe taarifa sahihi kwa wa piga kura. Hivi ninavyoandika kwenye mbao za majina limebandikwa tangazo linalowataarifu watu kuwa kama ulipigia kura Nkuruma na jina hulioni, basi nenda kwenye kituo cha shuleni au Kafteria huko utalikuta, kitu ambacho hapo awali hakikufanyika. Watu wengi ambao walianza kukata tamaa kuwa ndoto zao za kuleta tumaini jipya zimepotea hivi sasa wanashangilia baada ya kuyakuta majina kwenye vituo vingine.

pendekezo: tuhakikishe na kwenye vituo vingine taarifa za wapi majina yanaweza kupatikana zibandikwe (kama hazijabandikwa) kwenye vituo hivyo ili kuwarahisishia watu utafutaji wa majina
 
Tunajuwa wewe CHEDEMA Bllod in Blood out!! Nimekugongea Thanx hapo juu!!
 
umefanya vyema songa mbele na kazi yako nzuri, usisahau kuwashawishi watu wako wa karibu kumpeleka Slaa Ikulu. Good work
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…