Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Idadi ya vifo vilivyotokana na kuporomoka kwa jengo la ghorofa, Kariakoo jijini Dar es Salaam vimefikia 29, baada ya miili mingine tisa kupatikana.
Jengo hilo liliporomoka asubuhi ya Jumamosi Novemba 16, 2024 na kusababisha vifo, majeruhi zaidi ya 80 na uharibifu wa mali za mamilioni ya fedha.
Soma, Pia: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Waziri Mkuu aunda Tume ya watu maalumu 21 leo Nov 22, 2024
Leo Jumanne, Novemba 26, 2024, Msemaji Mkuu wa Serikali, Thobias Makoba akizungumza na waandishi wa habari akiwa eneo hilo la jengo lilipoporomoka amesema miili hiyo tisa imepatikana wakati shughuli ya kuondoa kifusi ikiendelea.
Makoba ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari- Maelezo amesema shughuli ya uokozi imefikia tamati leo Jumanne Novemba 26.
Jengo hilo liliporomoka asubuhi ya Jumamosi Novemba 16, 2024 na kusababisha vifo, majeruhi zaidi ya 80 na uharibifu wa mali za mamilioni ya fedha.
Soma, Pia: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Waziri Mkuu aunda Tume ya watu maalumu 21 leo Nov 22, 2024
Leo Jumanne, Novemba 26, 2024, Msemaji Mkuu wa Serikali, Thobias Makoba akizungumza na waandishi wa habari akiwa eneo hilo la jengo lilipoporomoka amesema miili hiyo tisa imepatikana wakati shughuli ya kuondoa kifusi ikiendelea.
Makoba ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari- Maelezo amesema shughuli ya uokozi imefikia tamati leo Jumanne Novemba 26.