Vifurushi vya Tigo vinaisha haraka kuliko vya voda

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Natumia tigo na voda. Naweza nikanunua GB tatu za Voda na zikakaa muda mrefu hadi unaridhika, hata siku tatu zinafika. Naingia Ista, YouTube nk. Lakini nikinunua GB 3 za tigo hata siku zinaweza zisimalize kwa matumizi hayohayo.

Na wewe umeexperience hii ya kifurushi cha Tigo kuisha haraka? Inaeababishwa na nini?
 
Sure kabisa nadhani tigo kuna setting zao za kula hizi mb.nimetumia voda siku tatu gb 1 ila tigo jioni haifiki unaambiwa ushamaliza

Ndugu Mteja,Umebakiwa na MB 256.00 za Kifurushi chako cha .Piga *102# kuangalia salio na *147*00# kununua kifurushi kingine.


Sent from my vivo 1907 using JamiiForums mobile app
 
Huwajui halotel wewe
 
Wana hii shida, wanatafuna vifurushi balaa.
 
Vifurushi vya voda vinaisha fasta kuliko zantel
 
Haloteli pia vinaisha sana
Mimi hao ndio kabisa wananiibia, bando linaisha fasta na wanatuma text nimemaliza lkn nikicheki kwenye data usage na kupiga mahesabu nakuta karibia Mb 200 kwny Gb 2 hazijatumika.
 
Mimi Katika kutumia Halotel , Airtel na Voda . Kwa Voda naona bando linakaa na na linaisha kihalali kulingsnisha na wengine .
 
Unatumia Instagram na Tiktock, una washa data full time, huweki data saver, na huja turn off "background data" kwenye setting halafu kwa siku unanunua MB 500 utaendelea kulaumu watu!
 
Mimi Katika kutumia Halotel , Airtel na Voda . Kwa Voda naona bando linakaa na na linaisha kihalali kulingsnisha na wengine .
Nikiwa na bando la voda huwa nakuwa na amani sana. Nafanya vurugu zote. Cha Tigo nakaa kwa machale sana.
 
Unatumia Instagram na Tiktock, una washa data full time, huweki data saver, na huja turn off "background data" kwenye setting halafu kwa siku unanunua MB 500 utaendelea kulaumu watu!
Hilo halielezei kwanini kifurushi cha Tigo kinaisha haraka kuliko cha voda
 
Nikiwa na bando la voda huwa nakuwa na amani sana. Nafanya vurugu zote. Cha Tigo nakaa kwa machale sana.
Hata mimi kuna siku nikijaribu kuunga cha Gb 2.2 mpk nikajisemea au wamenisahau wamenipa 5gB maana nimetumia pakubwa na bado nadunda
 
Huwajui HALOTEL hao ndio kinara wa kula mb Tanzania utasikia
Ndugu mteja umetumia 75% ya kifurushi chako.
 
Yaani saizi nawaza sijui nihamie mtandao gani,Tigo wamekuwa wezi kama voda,voda nilishaacha kutumia .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…