KIMOMWEMOTORS
JF-Expert Member
- May 17, 2018
- 358
- 675
Salam wana jukwaa.
Kodi ilivyokadiriwa kwenye gari aina ya Subaru Exiga ya mwaka 2008, ambapo ushuru wa garii hii unasomeka kama Tsh 21,000,000 wakati Valuation iliyotumika kwenye kupata ushuru huo ni Dola 8000+
Uhalisia wa gharama za gari hii yaani CIF ni dola kati ya 2000 mpaka 5000+ kama ambavyo ntaambatanisha kwenye picha hapa chini. Kwa kweli kodi iliyokadiriwa ni kubwa mno kwa gari hii ukilinganisha na CIF halisi tunayoishuhudia kwenye mitandao ya wauzaji wa magari huko Japan ambayo ni kati ya CIF dola 1900 mpaka CIF dola 5000.
Subaru Exiga ya 2009 imethaminishwa kwa CIF dola 11,000 na Ushuru wake ni 22,000,000+ wakati ukiingia mitandao halisi ya wauza magari huko nje unakuta CIF dola 2000 mpaka 6000 ambayo ni chini sana tofauti na wanayotumia wao kwenye hesabu zao.
Ombi kwa mamlaka husika wajaribu kulipitia upya jambo hili au kama kuna vigezo maalum wanatumia kwa baadhi ya magari basi vizuri wakaweka utaratibu wa kutoa elimu juu ya vigezo hivyo ili watanzania wapate kufahamu.
Kama ni makosa ya kibinadamu pia wafanye marekebisho maana watanzania wengi wanataka kutumia gari hizi ila Ushuru mkubwa ni kikwazo.
Karibuni wadau kwa maoni zaidi ili Mamlaka ipate kuona uzito katika jambo hili na kwa aina nyingine za magari.
Kodi ilivyokadiriwa kwenye gari aina ya Subaru Exiga ya mwaka 2008, ambapo ushuru wa garii hii unasomeka kama Tsh 21,000,000 wakati Valuation iliyotumika kwenye kupata ushuru huo ni Dola 8000+
Uhalisia wa gharama za gari hii yaani CIF ni dola kati ya 2000 mpaka 5000+ kama ambavyo ntaambatanisha kwenye picha hapa chini. Kwa kweli kodi iliyokadiriwa ni kubwa mno kwa gari hii ukilinganisha na CIF halisi tunayoishuhudia kwenye mitandao ya wauzaji wa magari huko Japan ambayo ni kati ya CIF dola 1900 mpaka CIF dola 5000.
Subaru Exiga ya 2009 imethaminishwa kwa CIF dola 11,000 na Ushuru wake ni 22,000,000+ wakati ukiingia mitandao halisi ya wauza magari huko nje unakuta CIF dola 2000 mpaka 6000 ambayo ni chini sana tofauti na wanayotumia wao kwenye hesabu zao.
Ombi kwa mamlaka husika wajaribu kulipitia upya jambo hili au kama kuna vigezo maalum wanatumia kwa baadhi ya magari basi vizuri wakaweka utaratibu wa kutoa elimu juu ya vigezo hivyo ili watanzania wapate kufahamu.
Kama ni makosa ya kibinadamu pia wafanye marekebisho maana watanzania wengi wanataka kutumia gari hizi ila Ushuru mkubwa ni kikwazo.
Karibuni wadau kwa maoni zaidi ili Mamlaka ipate kuona uzito katika jambo hili na kwa aina nyingine za magari.