BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
JK, kama kweli una nia ya kuwashughulikia mafisadi basi Watanzania wote bila kujali itikadi za vyama vyetu na wale tusiokuwa na vyama tutakuunga mkono katika juhudi zako za kupambana na ufisadi na kuutokomeza kabisa. Wananchi tutafurahi kuona mafisadi wote wanafunguliwa mashtaka na kufilisiwa pale ambapo kuna ushahidi wa kutosha kuonyesha utajiri wao umepatikana kwa njia za haramu. Pia tutafurahi kuona aliyekuwa Gavana wa BoT Balalli anarudishwa haraka nchini ili kujibu tuhuma za ufisadi dhidi yake.
Tunataka kuona Tanzania ambayo haitakuwa na
watu ambao wako juu ya sheria na hata wakifanya madhambi sheria haiwagusi.
Vigogo kitanzini
na Ratifa Baranyikwa na Kulwa Karedia
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
SASA ni dhahiri kuwa Rais Jakaya Kikwete amedhamiria kuandika historia mpya kwa kuwa rais wa kwanza wa Tanzania kumfikisha mahakamani mtangulizi wake.
Ingawa hatua hiyo inaelezwa na wafuatiliaji wa mambo kuwa inaweza kuwa na athari mbaya kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja na serikali anayoiongoza, inabaki kuwa nguzo yake kuu ya kurejesha imani kwa wananchi wanaotaka kuona akitekeleza ahadi zake kama ambavyo amekuwa akiahidi mara kwa mara.
Tamko la serikali lililotolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Alhamisi, Aprili 24, bungeni Dodoma, kuwa inafuatilia taarifa za tuhuma kuhusu matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya viongozi wa Serikali ya Awamu ya Tatu, na iwapo ikithibitika kuwa walitenda makosa, watachukuliwa hatua zinazostahili, linaonyesha kuwa sasa Mkapa anaweza kufikishwa mahakamani.
Katika kuonyesha dhamira ya dhati ya serikali yake kuhakikisha inatekeleza matakwa ya wananchi ya kutaka kuwepo uchunguzi kwa viongozi wa juu serikalini wanaotuhumiwa kutumia madaraka yao vibaya, Rais Kikwete jana aliwaambia waandishi wa habari kupitia kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, kuwa juhudi za kupambana na vitendo vya rushwa zinaendelezwa bila ajizi.
Rais Jakaya Kikwete, ambaye jana aliongoza mamia ya Watanzania kuadhimisha miaka 44 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, sherehe zilizofanyika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam bila kuwepo kwa mtangulizi wake, Mkapa, aliwaomba wananchi kushirikiana na serikali yake katika mapambano dhidi ya vitendo vya ufisadi.
Katika taarifa yake hiyo iliyotolewa Ikulu, alisema mafanikio ya mapambano yanayoonekana hivi sasa yanategemea zaidi ushirikiano wa wafanyakazi na akawataka kuwa mstari wa mbele katika harakati hizo.
Aidha, aliwataka kuzingatia kujiepusha na vitendo vya kupokea au kutoa rushwa, kwa sababu nao wananungunikiwa na umma kujihusisha navyo.
Taarifa hiyo ambayo Kikwete anaeleza kuwa hatakuwepo katika maadhimisho ya Sikukuu ya Mei Mosi, ilieleza kuwa wafanyakazi wakiipiga vita rushwa, vigogo wanaodaiwa kupokea rushwa watapata wakati mgumu wa kufanikisha vitendo vyao viovu.
Rais amewaomba wafanyakazi wafanye mambo matatu, kwanza, wajiepushe wao wenyewe na vitendo vya rushwa .wakatae kutumika katika vitendo vya rushwa na wasaidie kutoa taarifa za rushwa ili zifanyiwe kazi na wahusika wabanwe, inasomeka sehemu ya taarifa hiyo ya Rais Kikwete.
Tamko hili la Rais Kikwete ambaye jana alitangaza kutohudhuria sherehe za Mei Mosi kutokana na kuwa safarini katika nchi za Uganda na Ethiopia, limetafsiriwa na wafuatiliaji wa mambo kuwa hatua yake ya kwanza ya kuuthibitishia umma wa wafanyakazi kuwa hakuna kiongozi atakayesalimika kama atabainika kuhusishwa na rushwa.
Aidha, walieleza kuwa Rais Kikwete amelazimika kutoa tamko hilo ili kupoza dukuduku la wafanyakazi kuonyesha hasira yao kwa serikali katika maadhimisho hayo, jambo linaloweza kuzidi kujenga taswira mbaya kwa serikali yake.
Pamoja na Mkapa, tamko la Waziri Mkuu Pinda, sambamba na lililotolewa jana na Rais Kikwete, yanonyesha kuwa viongozi wengine waandamizi walio katika hatari ya kufikishwa mahakamani iwapo tuhuma zinazoelekezwa kwao zitathibitika kuwa kweli, ni pamoja na Andrew Chenge na Basil Mramba, ambao walikuwa mihimili na washauri wa karibu wa Mkapa wakati wa utawala wake.
Tayari Chenge ambaye alilazimika kujiuzulu wadhifa wa uwaziri hivi karibuni ameanza kuchunguzwa kwa tuhuma za kuhusika na kashfa za rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi ambayo Tanzania iliuziwa na Kampuni ya BAE ya nchini Uingereza.
Wachambuzi wameeleza kuwa iwapo Mkapa na Chenge watathibitika kuhusika na makosa ya jinai, basi haitakuwa rahisi kwa Mramba kuachwa pembeni kwa sababu alikuwa mshauri mkuu wa masuala ya fedha wa Mkapa.
Katika hatua nyingine, kutoonekana na ukimya wa sasa wa Mkapa umeanza kuzusha hisia tofauti miongoni mwa jamii.
Mkapa jana pia hakuonekana katika sherehe za maadhimisho ya miaka 44 ya Muungano huku viongozi wengine wastaafu wakihudhuria sherehe hizo.
Ukiacha Mkapa, viongozi wastatafu waliohudhuria ni Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye.
Haikufahamika hasa sababu za kutohudhuria kwa Mkapa katika sherehe hizo, ikiwa ni mara ya pili kukosekana katika matukio makubwa ya kitaifa na yale yanayokihusu chama chake, ambacho alikuwa mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka kumi.
Mkapa hakuhudhuria Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi uliofanyika Butiama, mkoani Mara mwishoni mwa Machi, mwaka huu.
Wadadisi na wachambuzi waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili walieleza kushangazwa kwao na kutoonekana kwa Mkapa katika matukio hayo makubwa ya kitaifa na kichama na kudai kuwa huenda kunasababishwa na uzito wa tuhuma zinazomkabili.
Baadhi ya tuhuma zinazoelekezwa kwa Mkapa ni pamoja na kumiliki Kampuni ya kuzalisha umeme ya Tanpower Resources Ltd, ambayo ilishinda zabuni ya kununua mradi wa kuzalisha umeme kutoka mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira ulioko Mbeya.
Madai hayo ambayo ni miongoni mwa yale yaliyoelezwa kuchunguzwa na Serikali, yanaelezwa kuwa huenda ni moja kati ya mambo yanayomkosesha raha kiongozi huyo na kumfanya ashindwe kujumuika na viongozi wenzake hata katika masuala muhimu.
Aidha, sherehe hizo za muungano ambazo jana zilifanyika kwa mbwembwe za aina yake, hazikuhudhuriwa pia na viongozi wengine wa vyama vya siasa.
Watu wengine mashuhuri ambao hawakuhudhuria sherehe hizo ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Andrew Chenge.
Matukio ya jana yalivuta hisia za wengi katika sherehe hizo zilizoanza majira ya saa 4:05 asubuhi, baada ya Rais Kikwete kuwasili uwanjani hapo akiwa katika gari la wazi pamoja na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange.
Wakati akiingia uwanjani, rais aliweza kuvumilia mvua iliyokuwa ikinyesha.
Sherehe hizo pia zilipambwa na mbwembwe za helikopta za jeshi pamoja na ndege za usafirishaji zilizopita uwanjani hapo zikitokea upande wa kaskazini mwa uwanja huo.
Katika kuadhimisha sherehe hizo, Rais Kikwete jana alitoa msamaha kwa wafungwa 3,300.
Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, kwa vyombo vya habari, ilisema msamaha huo utahusu wafungwa wanaotumikia kifungo chini ya miaka mitano.
Alisema msamaha huo utawahusu wafungwa wazee na wenye umri zaidi ya miaka 40, lakini hauwagusi wafungwa waliohukumiwa kunyongwa, waliokamatwa na dawa za kulevya, unyanganyi wa kutumia silaha, wanaotumikia kifungo cha maisha, kujamiana na wenye makosa ya kuwapa mimba wanafunzi.
Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 11 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
Mkapa lazima tumfunge, tusipomfunga yeye basi watoto wake. Haiwezekani ukala pesa za masikini halafu mtu aachwe hivi hivi. Huyu lazima jeuri yake tuikomeshe. Rais kikwete akishindwa atuambie sisi wananchi ili tumshughulikie. Pesa yote anayopewa ya kustaafu haimtoshi mpaka analiibia taifa kiasi hiki!!!!!! BASILI MRAMBA TUNAJUA NDO ANAMILIKI KIBO HOTELI PALE ARUSHA. HUYU NAYE LAZIMA ACHUNGUZWE. ALIZITOA WAPI HIZO HELA WAKATI UKOO WAKE NI MASKINI KAMA WATANZANIA WENGINE. KUZAA WATOTO NA MAMA MKAPA NDO IKAWA DILI YA WAO NA MKAPA KUTUIBIA. LAZIMA TUWAKOMESHE. RAIS ASIPOWAKOMESHA, WANANCHI TUKO TAYARI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
na Methew, Dar, - 27.04.08 @ 10:43 | #8968
Mkapa lazima tumfunge, tusipomfunga yeye basi watoto wake. Haiwezekani ukala pesa za masikini halafu mtu aachwe hivi hivi. Huyu lazima jeuri yake tuikomeshe. Rais kikwete akishindwa atuambie sisi wananchi ili tumshughulikie. Pesa yote anayopewa ya kustaafu haimtoshi mpaka analiibia taifa kiasi hiki!!!!!! BASILI MRAMBA TUNAJUA NDO ANAMILIKI KIBO PALACE HOTELI PALE ARUSHA. HUYU NAYE LAZIMA ACHUNGUZWE. ALIZITOA WAPI HIZO HELA WAKATI UKOO WAKE NI MASKINI KAMA WATANZANIA WENGINE. KUZAA WATOTO NA MAMA MKAPA NDO IKAWA DILI YA WAO NA MKAPA KUTUIBIA. LAZIMA TUWAKOMESHE. RAIS ASIPOWAKOMESHA, WANANCHI TUKO TAYARI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
na Methew, Dar, - 27.04.08 @ 10:45 | #8969
WALE WANAOBAINIKA,
WASULUBISHWE, WASULUBISHWE,
KAMA WANVYOTUSULUBISHA
MASHULE HAYANA MADAWATI
HOSPITALI HAZINA MADAWA
MADAKTARI WETU WAMEKATA TAMAA
WALIMU WETU WAMEKATA TAMAA
VIONGOZI SAFI WASIOKUWA MAFISADI WANAKATA TAMAA
SHERIA NA HAKI VIACHIWE VICHUKUE MKONDO WAKE
VYOMBO VYOTE VYA DOLA VIACHIWE VIFANYE KAZI KIKAMILIFU, KWA KUFUATA SHERIA BILA KUINGILIWA
HAYA YAKITEKELEZWA, WANANCHI TUTAREJESHA IMANI
TUTAFANYA KAZI KWA JUHUDI KUBWA
TAIFA LITASONGA MBELE KIUCHUMI
MH RAIS TEKELEZA,
UMMA WA WATANZANIA SAFI UPO NYUMA YAKO
VIONGOZI WAKONGWE WA ZAMANI WAPO NYUMA YAKO
JUMUIA ZA KIMATAIFA ZIPO NYUMA YAKO
VYOMBO VYOTE VYA DOLA VIPO NYUMA YAKO
INAWEZEKANA
JITENGE NA MAFISADI
na G.A. Kilimwano, Kijitonyama, DSM, - 27.04.08 @ 11:07 | #8973
kikwete raisi wangu mpenzi lazima uondowe uvivu kwa huyu mkapa katutowa kapa watanzania sasa atakula jeuri yake kiongozi huyu ni jeuri ***** fisadi kauwa watu bila hatia watu walikuwa wanaandamana kwa amani kudai haki yao ya kikatiba leo kwa ujeuri wako tu umewauwa sasa mungu kakupa laana na kweli sasa bora chizi kwa dhamani kuliko muwaji wewe ewe mwenyezimungu endelea kumuadhiri huyu fisadi
na king, tz, - 27.04.08 @ 11:19 | #8978
Mzee huyu kwanza atengwe kanisani anakosali, maana kuungama kwa Padri haitoshi kama hatajitokeza kuwaomba msamaha watanzania walio wengi na kurudisha migodi ya Mbeya jambo ambalo anaweza kulifanya na umma ukafikilia kumsamehe.
Majina ya mashule na majengo yaliyoitwa kwa jina lake, bila ridhaa ya watanzania ambao aliwakosea yabadilishwe, maana jina limenajisika ktk jamii.
Amemsaliti Nyerere ambaye nusura sehemu zingine alitaka kupigwa mawe kwa kulitetea jina lake,baada ya kufa 'Mkapa'akajichafua na kibaya ZAIDI akawachafua wasaidizi wake wa karibu ambao 'walianza kula bila kunawa' na kusugua midomo chini kama 'nguruwe mwitu'.
Kumfunga haitasaidia,maana atakuwa sehemu maalumu,jambo muhimu ni kuchukua alivyovichukua na kumtenga ktk jamii.
Kiongozi mmoja katika visiwa vidogo vya 'SAMOA' alipoukosea umma alitengwa bila kualikwa au kuhudhuria sherehe mpaka alipoomba msamaha kwa umma!.
Alipoingia madarakani alitangaza mali alipotoka ameona mzigo wa kutangaza, alishinikiza kuuza nyumba za watanzania ktk maeneo muhimu ya nchi na kusababisha usumbufu kwa walio nunua pindi nguvu ya UMMA/ saa ya ukombozi itakapofika na wananchi kuzidai kwa nguvu!
na Bwato Mwende Kihulo, NewZeland, - 27.04.08 @ 12:23 | #8982
MH RAIS
ILI KUKWEPA LAWAMA,
JITENGE PEMBENI NA HAWA MAFISADI
CHAPA KAZI, ONGOZA WATANZANIA BILA HOFU YOYOTE
ONGOZA TAIFA KWA UADILIFU NA UNYOFU,
HII NDIYO ILIYOKUWA SIRI YA JK NYERERE KUWA MAARUFU
WAKONGWE NA MASHUJAA WA TAIFA HILI WALIOKUWA SAFI WOTE WAPO NYUMA YAKO (KINA KAWAWA, MSUYA, WARIOBA, SALIM n.k.)
CHA MSINGI ACHIA VYOMBO VYA DOLA VIFANYE KAZI BILA KUINGILIWA, USIUMIZE KICHWA CHAKO
UNAPOJARIBU KUWALINDA UTAJICHAFUA
KAMA ILIWEZEKANA KUREJESHA MALI YA WATANZANIA KUTOKA MIKONONI MWA WAKOLONI, KWA NINI ISIWEZEKANE KUREJESHA MALI YA WATANZANIA KUTOKA MIKONONI MWA MAFISADI?
LAKINI
SHERIA IFUATWE
na R. Shenawi, Ubungo, DSM, - 27.04.08 @ 13:06 | #8987
INGEKUWA VIZURI AKAMSHITAKI ILI NA YEYE AKIMALIZA MUDA WAKE WA URAIS ASHUGHULIKIWE VILEVILE.ILA HAKUNA LOLOTE LITAKALOFANYIKA MNAZUGWA TU WADANGANYIKA MAANA WAMESHAWAJUA MNAPENDA SANA STORI BILA VITENDO.KWANI WALIOKWISHA WAJIBIKA KUNA NINI TENA?MTABAKIA KUSIKIA TUME IMEWASILISHA MAPENDEKEZO ILA TUMEUNDA KAMATI KUSHAURI KISHA TUUNDE TASK FORCE KUIMPLIMENTI..WAJINGA NYIE UTAIBANAJE SERIKALI ILIYOPITA WAKATI YEYE MWENYEWE KIKWETE ALIKUWA MMOJA WA SERIKALI HIYO?MSHITAKI MKAPA UONE KAMA KUNA ATAKAE SALIMIKA KTK SERIKALI ILIYOPITA.UTALALAMIKIA VIPI MIKATABA MIBOVU WAKATI WAWEKEZAJI WALITAFUTWA NA KIKWETE NA BALOZI ZAKE AKIWA WAZIRI WA MAMBO YA NJE?UTAMTENGA VIPI NA MIKATABA MIBOVU?
MKAPA ANAAKILI NDIO MANA HATAKI KUONGEA NA MAKANJANJA MANA ANAWAJUA WALIVYOMABINGWA WA KUGEUZA MANENO.PALE MMEKWAA KISIKI MANA NA YEYE ALIKUWA KWENYE TAALUMA HIYO ANAUJUA USANII WOTE, WACHEZEENI WAKINA CHENGE WASIOJUA UJANJA WENU.KWASASA HATA WAANDISHI MNACHEZESHWA NGOMA MSIOIJUA KUMCHAFUA MKAPA ILA MJUE WALIOLIANZISHA HILO WANALIPWA VIZURI KAZI KWENU NYIE MLIODANDIA TU NA KUSHABIKIA.MWISHONI MTAONA HAYA MAANA HAKUNA HATA MOJA MNALOLIFIKIRIA LITATOKEA.
na chadu, rahaleo, - 27.04.08 @ 13:13 | #8989
Tunasubiri nini kumweka msalabani huyu Mkapa si tayari tumejua ametuibia Kiwira Coal Mine, kaanzisha ANBEN katuibia KIlimanjaro International Airport na mkewe na mdudu mengine tumpeleke akalindwe na Zombe huko gerezani ametuibia mno roho inauma sana
na Mponjoli, Arusha, - 27.04.08 @ 13:19 | #8992
Chadu, rahaleo, - 27.04.08 @ 13:13 | #8989,
Kwa taarifa yako Zambia iliwezekana kumshitaki Chiluba kwa tuhuma za ufisadi na nchi sasa inasonga mbele.
Usitake kutisha watu.
Ulimwengu unakwenda ukibadilika. Uliwengu wa leo siyo wa jana. Kama unadhani haiwezekani basi itawezekana
Watanzania wa leo siyo watanzania wa jana
Tuhuma hizi za ufisadi hazivumiliki
Nahisi kwamba NA WEWE NI FISADI
na chadudu, rahakesho, - 27.04.08 @ 13:26 | #8993
Thinking the unthinkable,sinking the unsinkable MV Ufisadi
na gonga, maswa, - 27.04.08 @ 13:50 | #8998
Jamani watanzania msidanganywe na hawa wasanii kwani hakuna lolote litakaloendelea hapa ni kudanganyana na siku zisonge mbele, utasikia kamati imegundua mambo mengi halafu itaundwa kamati ya kupendekeza mambo mengi yafanikishwaje baada ya hapo pindisha atasema apewe muda ili acheki kama ni jinai au madai baada ya hapo atasema wanapesa nyingi ukiwapeleka mahakamani watakushinda then litaachwa na kuibuliwa lingine na sisi watanzani tulivyo mashabiki tutusahau hili na kuamia kwenye jipya,kwa mtazamo wangu kikwete hana sera za kuleta maendeleo hivy hili msioji sana anafanya nini juu ya maendeleo ya nchi anatumia ufisadi kuteka mawazo yetu na tumesahau kuhoji serikali imefanya nini mpaka sasa hivi kwani kilakitu hakiendi sawa. 0757-670808
na mtanganyika, tanganyika, - 27.04.08 @ 14:55 | #9005
Tunataka kuona Tanzania ambayo haitakuwa na
watu ambao wako juu ya sheria na hata wakifanya madhambi sheria haiwagusi.
Vigogo kitanzini
na Ratifa Baranyikwa na Kulwa Karedia
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
SASA ni dhahiri kuwa Rais Jakaya Kikwete amedhamiria kuandika historia mpya kwa kuwa rais wa kwanza wa Tanzania kumfikisha mahakamani mtangulizi wake.
Ingawa hatua hiyo inaelezwa na wafuatiliaji wa mambo kuwa inaweza kuwa na athari mbaya kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja na serikali anayoiongoza, inabaki kuwa nguzo yake kuu ya kurejesha imani kwa wananchi wanaotaka kuona akitekeleza ahadi zake kama ambavyo amekuwa akiahidi mara kwa mara.
Tamko la serikali lililotolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Alhamisi, Aprili 24, bungeni Dodoma, kuwa inafuatilia taarifa za tuhuma kuhusu matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya viongozi wa Serikali ya Awamu ya Tatu, na iwapo ikithibitika kuwa walitenda makosa, watachukuliwa hatua zinazostahili, linaonyesha kuwa sasa Mkapa anaweza kufikishwa mahakamani.
Katika kuonyesha dhamira ya dhati ya serikali yake kuhakikisha inatekeleza matakwa ya wananchi ya kutaka kuwepo uchunguzi kwa viongozi wa juu serikalini wanaotuhumiwa kutumia madaraka yao vibaya, Rais Kikwete jana aliwaambia waandishi wa habari kupitia kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, kuwa juhudi za kupambana na vitendo vya rushwa zinaendelezwa bila ajizi.
Rais Jakaya Kikwete, ambaye jana aliongoza mamia ya Watanzania kuadhimisha miaka 44 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, sherehe zilizofanyika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam bila kuwepo kwa mtangulizi wake, Mkapa, aliwaomba wananchi kushirikiana na serikali yake katika mapambano dhidi ya vitendo vya ufisadi.
Katika taarifa yake hiyo iliyotolewa Ikulu, alisema mafanikio ya mapambano yanayoonekana hivi sasa yanategemea zaidi ushirikiano wa wafanyakazi na akawataka kuwa mstari wa mbele katika harakati hizo.
Aidha, aliwataka kuzingatia kujiepusha na vitendo vya kupokea au kutoa rushwa, kwa sababu nao wananungunikiwa na umma kujihusisha navyo.
Taarifa hiyo ambayo Kikwete anaeleza kuwa hatakuwepo katika maadhimisho ya Sikukuu ya Mei Mosi, ilieleza kuwa wafanyakazi wakiipiga vita rushwa, vigogo wanaodaiwa kupokea rushwa watapata wakati mgumu wa kufanikisha vitendo vyao viovu.
Rais amewaomba wafanyakazi wafanye mambo matatu, kwanza, wajiepushe wao wenyewe na vitendo vya rushwa .wakatae kutumika katika vitendo vya rushwa na wasaidie kutoa taarifa za rushwa ili zifanyiwe kazi na wahusika wabanwe, inasomeka sehemu ya taarifa hiyo ya Rais Kikwete.
Tamko hili la Rais Kikwete ambaye jana alitangaza kutohudhuria sherehe za Mei Mosi kutokana na kuwa safarini katika nchi za Uganda na Ethiopia, limetafsiriwa na wafuatiliaji wa mambo kuwa hatua yake ya kwanza ya kuuthibitishia umma wa wafanyakazi kuwa hakuna kiongozi atakayesalimika kama atabainika kuhusishwa na rushwa.
Aidha, walieleza kuwa Rais Kikwete amelazimika kutoa tamko hilo ili kupoza dukuduku la wafanyakazi kuonyesha hasira yao kwa serikali katika maadhimisho hayo, jambo linaloweza kuzidi kujenga taswira mbaya kwa serikali yake.
Pamoja na Mkapa, tamko la Waziri Mkuu Pinda, sambamba na lililotolewa jana na Rais Kikwete, yanonyesha kuwa viongozi wengine waandamizi walio katika hatari ya kufikishwa mahakamani iwapo tuhuma zinazoelekezwa kwao zitathibitika kuwa kweli, ni pamoja na Andrew Chenge na Basil Mramba, ambao walikuwa mihimili na washauri wa karibu wa Mkapa wakati wa utawala wake.
Tayari Chenge ambaye alilazimika kujiuzulu wadhifa wa uwaziri hivi karibuni ameanza kuchunguzwa kwa tuhuma za kuhusika na kashfa za rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi ambayo Tanzania iliuziwa na Kampuni ya BAE ya nchini Uingereza.
Wachambuzi wameeleza kuwa iwapo Mkapa na Chenge watathibitika kuhusika na makosa ya jinai, basi haitakuwa rahisi kwa Mramba kuachwa pembeni kwa sababu alikuwa mshauri mkuu wa masuala ya fedha wa Mkapa.
Katika hatua nyingine, kutoonekana na ukimya wa sasa wa Mkapa umeanza kuzusha hisia tofauti miongoni mwa jamii.
Mkapa jana pia hakuonekana katika sherehe za maadhimisho ya miaka 44 ya Muungano huku viongozi wengine wastaafu wakihudhuria sherehe hizo.
Ukiacha Mkapa, viongozi wastatafu waliohudhuria ni Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye.
Haikufahamika hasa sababu za kutohudhuria kwa Mkapa katika sherehe hizo, ikiwa ni mara ya pili kukosekana katika matukio makubwa ya kitaifa na yale yanayokihusu chama chake, ambacho alikuwa mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka kumi.
Mkapa hakuhudhuria Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi uliofanyika Butiama, mkoani Mara mwishoni mwa Machi, mwaka huu.
Wadadisi na wachambuzi waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili walieleza kushangazwa kwao na kutoonekana kwa Mkapa katika matukio hayo makubwa ya kitaifa na kichama na kudai kuwa huenda kunasababishwa na uzito wa tuhuma zinazomkabili.
Baadhi ya tuhuma zinazoelekezwa kwa Mkapa ni pamoja na kumiliki Kampuni ya kuzalisha umeme ya Tanpower Resources Ltd, ambayo ilishinda zabuni ya kununua mradi wa kuzalisha umeme kutoka mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira ulioko Mbeya.
Madai hayo ambayo ni miongoni mwa yale yaliyoelezwa kuchunguzwa na Serikali, yanaelezwa kuwa huenda ni moja kati ya mambo yanayomkosesha raha kiongozi huyo na kumfanya ashindwe kujumuika na viongozi wenzake hata katika masuala muhimu.
Aidha, sherehe hizo za muungano ambazo jana zilifanyika kwa mbwembwe za aina yake, hazikuhudhuriwa pia na viongozi wengine wa vyama vya siasa.
Watu wengine mashuhuri ambao hawakuhudhuria sherehe hizo ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Andrew Chenge.
Matukio ya jana yalivuta hisia za wengi katika sherehe hizo zilizoanza majira ya saa 4:05 asubuhi, baada ya Rais Kikwete kuwasili uwanjani hapo akiwa katika gari la wazi pamoja na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange.
Wakati akiingia uwanjani, rais aliweza kuvumilia mvua iliyokuwa ikinyesha.
Sherehe hizo pia zilipambwa na mbwembwe za helikopta za jeshi pamoja na ndege za usafirishaji zilizopita uwanjani hapo zikitokea upande wa kaskazini mwa uwanja huo.
Katika kuadhimisha sherehe hizo, Rais Kikwete jana alitoa msamaha kwa wafungwa 3,300.
Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, kwa vyombo vya habari, ilisema msamaha huo utahusu wafungwa wanaotumikia kifungo chini ya miaka mitano.
Alisema msamaha huo utawahusu wafungwa wazee na wenye umri zaidi ya miaka 40, lakini hauwagusi wafungwa waliohukumiwa kunyongwa, waliokamatwa na dawa za kulevya, unyanganyi wa kutumia silaha, wanaotumikia kifungo cha maisha, kujamiana na wenye makosa ya kuwapa mimba wanafunzi.
Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 11 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
Mkapa lazima tumfunge, tusipomfunga yeye basi watoto wake. Haiwezekani ukala pesa za masikini halafu mtu aachwe hivi hivi. Huyu lazima jeuri yake tuikomeshe. Rais kikwete akishindwa atuambie sisi wananchi ili tumshughulikie. Pesa yote anayopewa ya kustaafu haimtoshi mpaka analiibia taifa kiasi hiki!!!!!! BASILI MRAMBA TUNAJUA NDO ANAMILIKI KIBO HOTELI PALE ARUSHA. HUYU NAYE LAZIMA ACHUNGUZWE. ALIZITOA WAPI HIZO HELA WAKATI UKOO WAKE NI MASKINI KAMA WATANZANIA WENGINE. KUZAA WATOTO NA MAMA MKAPA NDO IKAWA DILI YA WAO NA MKAPA KUTUIBIA. LAZIMA TUWAKOMESHE. RAIS ASIPOWAKOMESHA, WANANCHI TUKO TAYARI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
na Methew, Dar, - 27.04.08 @ 10:43 | #8968
Mkapa lazima tumfunge, tusipomfunga yeye basi watoto wake. Haiwezekani ukala pesa za masikini halafu mtu aachwe hivi hivi. Huyu lazima jeuri yake tuikomeshe. Rais kikwete akishindwa atuambie sisi wananchi ili tumshughulikie. Pesa yote anayopewa ya kustaafu haimtoshi mpaka analiibia taifa kiasi hiki!!!!!! BASILI MRAMBA TUNAJUA NDO ANAMILIKI KIBO PALACE HOTELI PALE ARUSHA. HUYU NAYE LAZIMA ACHUNGUZWE. ALIZITOA WAPI HIZO HELA WAKATI UKOO WAKE NI MASKINI KAMA WATANZANIA WENGINE. KUZAA WATOTO NA MAMA MKAPA NDO IKAWA DILI YA WAO NA MKAPA KUTUIBIA. LAZIMA TUWAKOMESHE. RAIS ASIPOWAKOMESHA, WANANCHI TUKO TAYARI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI.
na Methew, Dar, - 27.04.08 @ 10:45 | #8969
WALE WANAOBAINIKA,
WASULUBISHWE, WASULUBISHWE,
KAMA WANVYOTUSULUBISHA
MASHULE HAYANA MADAWATI
HOSPITALI HAZINA MADAWA
MADAKTARI WETU WAMEKATA TAMAA
WALIMU WETU WAMEKATA TAMAA
VIONGOZI SAFI WASIOKUWA MAFISADI WANAKATA TAMAA
SHERIA NA HAKI VIACHIWE VICHUKUE MKONDO WAKE
VYOMBO VYOTE VYA DOLA VIACHIWE VIFANYE KAZI KIKAMILIFU, KWA KUFUATA SHERIA BILA KUINGILIWA
HAYA YAKITEKELEZWA, WANANCHI TUTAREJESHA IMANI
TUTAFANYA KAZI KWA JUHUDI KUBWA
TAIFA LITASONGA MBELE KIUCHUMI
MH RAIS TEKELEZA,
UMMA WA WATANZANIA SAFI UPO NYUMA YAKO
VIONGOZI WAKONGWE WA ZAMANI WAPO NYUMA YAKO
JUMUIA ZA KIMATAIFA ZIPO NYUMA YAKO
VYOMBO VYOTE VYA DOLA VIPO NYUMA YAKO
INAWEZEKANA
JITENGE NA MAFISADI
na G.A. Kilimwano, Kijitonyama, DSM, - 27.04.08 @ 11:07 | #8973
kikwete raisi wangu mpenzi lazima uondowe uvivu kwa huyu mkapa katutowa kapa watanzania sasa atakula jeuri yake kiongozi huyu ni jeuri ***** fisadi kauwa watu bila hatia watu walikuwa wanaandamana kwa amani kudai haki yao ya kikatiba leo kwa ujeuri wako tu umewauwa sasa mungu kakupa laana na kweli sasa bora chizi kwa dhamani kuliko muwaji wewe ewe mwenyezimungu endelea kumuadhiri huyu fisadi
na king, tz, - 27.04.08 @ 11:19 | #8978
Mzee huyu kwanza atengwe kanisani anakosali, maana kuungama kwa Padri haitoshi kama hatajitokeza kuwaomba msamaha watanzania walio wengi na kurudisha migodi ya Mbeya jambo ambalo anaweza kulifanya na umma ukafikilia kumsamehe.
Majina ya mashule na majengo yaliyoitwa kwa jina lake, bila ridhaa ya watanzania ambao aliwakosea yabadilishwe, maana jina limenajisika ktk jamii.
Amemsaliti Nyerere ambaye nusura sehemu zingine alitaka kupigwa mawe kwa kulitetea jina lake,baada ya kufa 'Mkapa'akajichafua na kibaya ZAIDI akawachafua wasaidizi wake wa karibu ambao 'walianza kula bila kunawa' na kusugua midomo chini kama 'nguruwe mwitu'.
Kumfunga haitasaidia,maana atakuwa sehemu maalumu,jambo muhimu ni kuchukua alivyovichukua na kumtenga ktk jamii.
Kiongozi mmoja katika visiwa vidogo vya 'SAMOA' alipoukosea umma alitengwa bila kualikwa au kuhudhuria sherehe mpaka alipoomba msamaha kwa umma!.
Alipoingia madarakani alitangaza mali alipotoka ameona mzigo wa kutangaza, alishinikiza kuuza nyumba za watanzania ktk maeneo muhimu ya nchi na kusababisha usumbufu kwa walio nunua pindi nguvu ya UMMA/ saa ya ukombozi itakapofika na wananchi kuzidai kwa nguvu!
na Bwato Mwende Kihulo, NewZeland, - 27.04.08 @ 12:23 | #8982
MH RAIS
ILI KUKWEPA LAWAMA,
JITENGE PEMBENI NA HAWA MAFISADI
CHAPA KAZI, ONGOZA WATANZANIA BILA HOFU YOYOTE
ONGOZA TAIFA KWA UADILIFU NA UNYOFU,
HII NDIYO ILIYOKUWA SIRI YA JK NYERERE KUWA MAARUFU
WAKONGWE NA MASHUJAA WA TAIFA HILI WALIOKUWA SAFI WOTE WAPO NYUMA YAKO (KINA KAWAWA, MSUYA, WARIOBA, SALIM n.k.)
CHA MSINGI ACHIA VYOMBO VYA DOLA VIFANYE KAZI BILA KUINGILIWA, USIUMIZE KICHWA CHAKO
UNAPOJARIBU KUWALINDA UTAJICHAFUA
KAMA ILIWEZEKANA KUREJESHA MALI YA WATANZANIA KUTOKA MIKONONI MWA WAKOLONI, KWA NINI ISIWEZEKANE KUREJESHA MALI YA WATANZANIA KUTOKA MIKONONI MWA MAFISADI?
LAKINI
SHERIA IFUATWE
na R. Shenawi, Ubungo, DSM, - 27.04.08 @ 13:06 | #8987
INGEKUWA VIZURI AKAMSHITAKI ILI NA YEYE AKIMALIZA MUDA WAKE WA URAIS ASHUGHULIKIWE VILEVILE.ILA HAKUNA LOLOTE LITAKALOFANYIKA MNAZUGWA TU WADANGANYIKA MAANA WAMESHAWAJUA MNAPENDA SANA STORI BILA VITENDO.KWANI WALIOKWISHA WAJIBIKA KUNA NINI TENA?MTABAKIA KUSIKIA TUME IMEWASILISHA MAPENDEKEZO ILA TUMEUNDA KAMATI KUSHAURI KISHA TUUNDE TASK FORCE KUIMPLIMENTI..WAJINGA NYIE UTAIBANAJE SERIKALI ILIYOPITA WAKATI YEYE MWENYEWE KIKWETE ALIKUWA MMOJA WA SERIKALI HIYO?MSHITAKI MKAPA UONE KAMA KUNA ATAKAE SALIMIKA KTK SERIKALI ILIYOPITA.UTALALAMIKIA VIPI MIKATABA MIBOVU WAKATI WAWEKEZAJI WALITAFUTWA NA KIKWETE NA BALOZI ZAKE AKIWA WAZIRI WA MAMBO YA NJE?UTAMTENGA VIPI NA MIKATABA MIBOVU?
MKAPA ANAAKILI NDIO MANA HATAKI KUONGEA NA MAKANJANJA MANA ANAWAJUA WALIVYOMABINGWA WA KUGEUZA MANENO.PALE MMEKWAA KISIKI MANA NA YEYE ALIKUWA KWENYE TAALUMA HIYO ANAUJUA USANII WOTE, WACHEZEENI WAKINA CHENGE WASIOJUA UJANJA WENU.KWASASA HATA WAANDISHI MNACHEZESHWA NGOMA MSIOIJUA KUMCHAFUA MKAPA ILA MJUE WALIOLIANZISHA HILO WANALIPWA VIZURI KAZI KWENU NYIE MLIODANDIA TU NA KUSHABIKIA.MWISHONI MTAONA HAYA MAANA HAKUNA HATA MOJA MNALOLIFIKIRIA LITATOKEA.
na chadu, rahaleo, - 27.04.08 @ 13:13 | #8989
Tunasubiri nini kumweka msalabani huyu Mkapa si tayari tumejua ametuibia Kiwira Coal Mine, kaanzisha ANBEN katuibia KIlimanjaro International Airport na mkewe na mdudu mengine tumpeleke akalindwe na Zombe huko gerezani ametuibia mno roho inauma sana
na Mponjoli, Arusha, - 27.04.08 @ 13:19 | #8992
Chadu, rahaleo, - 27.04.08 @ 13:13 | #8989,
Kwa taarifa yako Zambia iliwezekana kumshitaki Chiluba kwa tuhuma za ufisadi na nchi sasa inasonga mbele.
Usitake kutisha watu.
Ulimwengu unakwenda ukibadilika. Uliwengu wa leo siyo wa jana. Kama unadhani haiwezekani basi itawezekana
Watanzania wa leo siyo watanzania wa jana
Tuhuma hizi za ufisadi hazivumiliki
Nahisi kwamba NA WEWE NI FISADI
na chadudu, rahakesho, - 27.04.08 @ 13:26 | #8993
Thinking the unthinkable,sinking the unsinkable MV Ufisadi
na gonga, maswa, - 27.04.08 @ 13:50 | #8998
Jamani watanzania msidanganywe na hawa wasanii kwani hakuna lolote litakaloendelea hapa ni kudanganyana na siku zisonge mbele, utasikia kamati imegundua mambo mengi halafu itaundwa kamati ya kupendekeza mambo mengi yafanikishwaje baada ya hapo pindisha atasema apewe muda ili acheki kama ni jinai au madai baada ya hapo atasema wanapesa nyingi ukiwapeleka mahakamani watakushinda then litaachwa na kuibuliwa lingine na sisi watanzani tulivyo mashabiki tutusahau hili na kuamia kwenye jipya,kwa mtazamo wangu kikwete hana sera za kuleta maendeleo hivy hili msioji sana anafanya nini juu ya maendeleo ya nchi anatumia ufisadi kuteka mawazo yetu na tumesahau kuhoji serikali imefanya nini mpaka sasa hivi kwani kilakitu hakiendi sawa. 0757-670808
na mtanganyika, tanganyika, - 27.04.08 @ 14:55 | #9005