Viingilio vya mechi ya taifa star na Nigeria

Viingilio vya mechi ya taifa star na Nigeria

Nyenyere

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2010
Posts
14,804
Reaction score
10,715
Wakuu, nimeshangaa kusikia viingilio vimewekwa kwa viwango vya juu kuliko hata mechi za ligi. Kiingilio cha chini ni 7,000/= na cha juu kabisa ni 40,000/=. Jukwaa B kwa mechi za Yanga hutozwa 10,000 - 15,000/= lakini kwa mechi hii ni 20,000/=. Wakati wadau wengine walipendekeza hata iwe bure kabisa, TFF wametazama maslahi zaidi kuliko uzalendo. Kwa hali hii bado tuna safari ndefu kwenye kuamsha hamasa.
 
Haiwezi kuwa bure mkuu kwa tamko la TFF pekee...

Huo uwanja una gharama zake na mwenye nao ni serikali...
 
Wakuu, nimeshangaa kusikia viingilio vimewekwa kwa viwango vya juu kuliko hata mechi za ligi. Kiingilio cha chini ni 7,000/= na cha juu kabisa ni 40,000/=. Jukwaa B kwa mechi za Yanga hutozwa 10,000 - 15,000/= lakini kwa mechi hii ni 20,000/=. Wakati wadau wengine walipendekeza hata iwe bure kabisa, TFF wametazama maslahi zaidi kuliko uzalendo. Kwa hali hii bado tuna safari ndefu kwenye kuamsha hamasa.

Tangu ligi iishe na kufuatiwa na CECAFA Kagame Cup iliyowaingiza hasara sasa hivi TFF wanaonekana kuwa na 'njaa'. Timu ya Taifa iko katika hali ngumu, inahitaji mchezaji wa 12 (mashabiki wengi) ili iweze kushinda mechi hiyo. TFF isiweke fedha mbele bali iangalie uwezekano wa kuondoa kiingilio ili mashabiki waingie bure, uwanja ujae pomoni, Nigeria wazomewe hadi wachanganyikiwe.

CC. Jamal Malinzi ( Kwa hatua zako).
 
Hakika nilipanga kwenda,tena nilipie watu watano kwa tiketi ya elfu 5 ila kwa elfu 7 hakika siwezi kwenda soka letu bado sana kufikia malengo
 
Hivyo viingilio waache walipie wao na familia zao. We toa jero tuu kacheki DSTV SS3 vibanda umiza kama hali yako ya chini, kwa wale wanaojiweza nunua popcorn tulia sitting room kwako ucheki game mwanzo mwisho.

Litimu lenyewe halina hamasa then bado viingilio vipo juu. Nasema wapigwe tuu NIGERIA inabidi waigonge hiyo timu ya Malinzi na wenzake hata Goli 2,000,000,000,000,000,000.
 
Watanzania wamepoteza imani kabisa na Taifa Stars
 
Haiwezi kuwa bure mkuu kwa tamko la TFF pekee...

Huo uwanja una gharama zake na mwenye nao ni serikali...

Si lazima iwe bure mkuu, kama kweli tunataka watanzania waamshe ari kusapoti timu yao kama nyakati za Maximo, basi viingilio vingekuwa wa chini zaidi. Mfano tiketi ya chini kabisa ingeuzwa 3,000/= wengi wangeshawishika.
 
1. Ally Mustafa

2. S. Kapombe

3. H Mwinyi

4. Kelvin Y

5. Nadir H

6. Frank D / S. Ndemla

7. Mrisho N / Simon M

8. Mudathir Y / D Kaseke

9. John Bocco

10. Mbwana Samata

11. Thomas Ulimwengu
 
1. Ally Mustafa

2. S. Kapombe

3. H Mwinyi

4. Kelvin Y

5. Nadir H

6. Frank D / S. Ndemla

7. Mrisho N / Simon M

8. Mudathir Y / D Kaseke

9. John Bocco

10. Mbwana Samata

11. Thomas Ulimwengu


Mechi ya kesho tunahitaji washambuliaji wa kati 2 tu. Ni kati ya Samatta na John Bocco au Ulimwengu. Kuwaweka wote 3 kwa pamoja ni zaidi ya kamari kwa aina ya timu tunayocheza nayo.

Piga ua mechi ya kesho inamhitaji kijana mmoja anaitwa Himid Mao kama combative midfielder na kiungo mchezeshaji Ndemla au Domayo au wote kwa pamoja. Kwa mtazamo wangu timu itacheza vzr kama itapangwa hivi;

1. Barthez
2. Kapombe
3. Ngwali
4. YondanI
5. Cannavaro
6. Himid Mao
7. Ndemla/ Kaseke
8. Domayo
9. Ulimwengu/ Bocco
10. Samatta
11. Farid Mussa/ Rashid Mandawa
 
Back
Top Bottom