junior mussa
New Member
- Mar 9, 2019
- 1
- 5
Cha Kwanza wapendwa vijana ni kujitambua na kujua we ni Nani na unatoka wapi na unakwenda wapi......kuthubutu,kujitoa na kuangalia mbele kwakuwa umri unakwenda kwa kasi ya ajabu,kutokuwa tegemezi na kusubilia wazazi wakufanyie kila kitu hayana....... Mie binafsi nilianza kwa kuosha magari kwa kulipwa elfu tatu kwa kila siku. Nilifanya hivyo kwa mwaka mzima na nilijiwekea sh.elfu Moja kwakila siku,badae kidogo niliongezewa pesa nikawa nalipwa sh.elfu 5000.....hapo nikaanza kujiwekea sh.elfu 2500.kwa muda wa miezi sita..nikaanzisha biashara ya kuuza mgahawa wa chakula mpaka sasa ninaendelea na biashara hiyo na maisha yangu yamebadilika na Sikai tena nyumbani kwa wazazi wangu nimepanga chumba na ninamke na mtoto mmoja. Hakuna kinachoshindikana kikubwa ni ujasiri na uthubutu. Tatizo vijana wangi wanadharau pesa ndogo wakati ndogo ikitunzwa ndo huwa kubwa..... Tuamke vijana tujiamini na tuwe na ndoto na Mungu ni mwema atatusaida Kufika tunapotaka. Junior mussa.... #mwanza mjini.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app