Vijana mbio zinaweza kuwatoa kimaisha

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Kila mtu ana ndoto ya kuboresha maisha yake. Kama umezaliwa na afya njema na unapenda kufanya mazoezi jifundishe kukimbia.

Uzuri wa siku hizi smartphones unaweza kuitumia kwa vitu vingi sana. Unaweza ku download app ya kukufundisha kukimbia marathon.

Ukijiona unaweza hata nusu marathon tafuta mashindano ujisajili, yawe South Africa, Kenya au nchi nyingine. Ukishaonekana kwenye mashindano mawili matatu utaanza kupokea mialiko na hata hela ya maandalizi.

Wakimbiaji wa Kenya wengi wameshaagana na umasikini.
 
Mdada njia Bora ya kutoboa now...ni kutunga nyimbo ya kumsifia jiwe na serikali yake, sifu kisawasawa then nenda tbc hakika utairecord bure na itapromotiwa vilivyo, utaalikwa ikulu na kwenye matamasha mbalimbali kumuimbia na kumtukuza jiwe,TBC kutakuwa Kama sebuleni maisha utatoboa kirahisi Sana bila changamoto
 
Hii huwa ni bonge la fursa...ila watanzania bado tumelala...wakenya na waethiopia wanapiga pesa nzuri kupitia hapa...Sasa mtu anakimbia masaa mawili anashinda anakula 400m...Mungu akupe nnn... Cha msingi ni kufanya mazoezi ya Nguvu sio mzahamzaha...Kuliko kung'ang'a nia kazi ya kubeti Bora kuwekeza kwenye hapa.
 
Mkipata hizo fursa si mtazalisha ajira kwa vijana wenzenu na ku inspire wengine . Unaweza kukimbia beach kuanzia Aghakhan mpaka Unonio
 
Mkipata hizo fursa si mtazalisha ajira kwa vijana wenzenu na ku inspire wengine . Unaweza kukimbia beach kuanzia Aghakhan mpaka Unonio
Ni suala la mazoezi tu...hakuna kinachoshindikana....Mo falah alikuwa anaenda Kenya kufanya mazoezi ya kupanda milima....Usain bolt alikuwa anafungwa taili kubwa la gari miguuni alafu anakimbia nalo...vijana wa dar nendeni kimara milima kibao...pesa ya riadha iko nje nje... Ni juhudi binafsi tu .tofauti na michezo kama bondia au mpira wa miguu ni migumu kidogo
 
Kupanda milima na kukimbia kwenye mchanga ni mazoezi mazuri sana. Ukiwekwa kwenye lami utashangaa unavyo waacha wazungu.
 
Kupanda milima na kukimbia kwenye mchanga ni mazoezi mazuri sana. Ukiwekwa kwenye lami utashangaa unavyo waacha wazungu.
Kweli kabisa! Wazo zuri hili muhimu mazoezi,lishe nzuri na uvumilivu.
 
Sio rahisi kama ulivyo andika
 
Dah,hii mambo sio rahisi,nilifanikiwa kushiriki mashindano mawili ambayo yalijumuisha wakenya.
La kwanza nilikuwa kwenye kikosi cha shule,tulikuwa tunatumia uwanja uwanja,wakenya walituzunguka mpaka unajitoa uwanjani.
La pili ni kili Marathon,nilikimbia km 42 angalau nikaambulia medali.
Wenzetu wamejipanga ,wana kila huduma inayohitajika kuanzia walimu,lishe,kambi nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…