Vijana Mjini tunajipoteza wenyewe, Ardhi tunayo teknolojia hii hapa

Texas Tom.

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2013
Posts
510
Reaction score
273


















Hii nchi wangepewa waisrael ungekuta leo hii wanalisha afrika nzima, Babu yangu ana pori la ukubwa wa acre 800 (hectare 320 ivi) zamani alikua akilima mahindi/maharage/vitunguu akinyeeshea kwa maji ya kisima yakivutwa kwa pump ya disel za zamani sana ...sasa hivi shamba lile limegeuka pori tu, kisima kipo ila ni cha kusafisha tu maana hata leo ukitega sikio kwenye lile bomba lililozama ardhini unasikia milio ya maji, hakuna umeme ulopita maeneo yale ..wapi nitapata mhisani tuka install vitu solar kama hizi?
 

Attachments

  • images.jpg
    13.7 KB · Views: 1,797
  • images2.jpg
    9.3 KB · Views: 1,765
  • images3.jpg
    11.5 KB · Views: 1,745
  • images4.jpg
    10.7 KB · Views: 1,731
  • images6.jpg
    12.3 KB · Views: 1,724
  • images7.jpg
    9.6 KB · Views: 1,715
  • images8.jpg
    9.3 KB · Views: 1,720
  • images9.jpg
    11 KB · Views: 1,719
  • TllSis4.jpg
    15.2 KB · Views: 1,744
Ardhi iko wapi mkuu maana wengine hapa ni ardhi maeneo tuliyopo ni issue
 
taifa ili liendelee linaitaji vijana wawe na MAONO ,na wazee wawe na ndoto,JK amekalia kwenye safari tu na kuiga maneno bila matendo kila siku jk yupo singapore na thailand mara big result now,mara sijui kitu gani shame on you jk huna maono kabisa unadhani biashara ni bodaboda
 
Tatizo la watanzania tunatafuta VITU VIKUBWA haraka mno! wewe babu yako alikuachieni shamba, yeye alipata wapi wahisani wa kumpa pampu ya diesel? WAHISANI NI NGUVU ZAKO!





Hilo shamba la babu liko wapi tukuletee pesa, maana sisi wengine tuna shida mpaka kwenye suruwali, nyie watoto wa mjini mnavuta pesa kwenye ATM kila mwezi bila matatizo na mashati yenu meupe kama theruji!
 
Watu tunazungumzia kuliendeleza we ushakimbilia kwenye pesa
 
Last edited by a moderator:
Watu tunazungumzia kuliendeleza we ushakimbilia kwenye pesa

Lol! ulivosema limeshakuwa pori nikajua hamna ishu nalo mkuu niwaletee pesa mzungushie mambo mengine, si unajua mambo ya shamba suruwali kiraka!
 
Poa poa mkuu Texas Tom


CYBERTEQ ni kweli usemayo mkuu nakuna maeneo ardhi bado wanagawiana kulingana na mahitaji yako anakuambia unauona mti uleee ndio mwisho wakarti hapa Arusha kupata Acre moja ni issue

Mikoa yote ya kaskazini watu walijanjaruka mapema, kusini na magharibi bado sana watu wamelala!
 
Mikoa yote ya kaskazini watu walijanjaruka mapema, kusini na magharibi bado sana watu wamelala!


Ni kweli usemayo mkuu kweli huku kaskazini ni balaa kwa masuala ya ardhi ila ukienda magharibi na kusini na pia kaskazinimashariki huko bado ardhi ni bwerere na haijafika hizi bei zetu huku za Miliioni kadhaa
 
Tanzania kubwa sana hii mkuu, kuna maeneo ekari moja bado inauzwa elfu 10!!

Uongo dhambi! Yaani "msimbazi" moja ya Castle 4 mtu unapata ekari ya ardhi? Ina maana laki niliyofuta jana ingenipa ekari 10? Wapi huko nianze safari??
 
Uongo dhambi! Yaani "msimbazi" moja ya Castle 4 mtu unapata ekari ya ardhi? Ina maana laki niliyofuta jana ingenipa ekari 10? Wapi huko nianze safari??

Exactly !! Mbona kuna maeneo mengi makubwa tu hapa TZ yanayotolewa mpaka bure na serikali. Wewe tu ujipange kufyeka pori. #HelaYakoTu. Unajua Wa TZ wengi bado tumelala tena usingizi wa kukoroma. Kuna watu wanamezea mate ardhi yetu kweli yani wanatuangalia tu tunavyocheza na maisha. Nchi za watu opportunities its like zimekwisha u kno, kila sector watu washakaba !!
 
Poa poa mkuu Texas Tom


CYBERTEQ ni kweli usemayo mkuu nakuna maeneo ardhi bado wanagawiana kulingana na mahitaji yako anakuambia unauona mti uleee ndio mwisho wakarti hapa Arusha kupata Acre moja ni issue

hiyo ardhi kwa huku chini ni mafuta tupu kwa kule juu ya bara bara ni mawe, huo mto mkubwa ni mto wa msimu ila inapeleka maji mengi sana Lake Eyasi kipindi cha masika ...unaitwa mto Barray
 
ndugu texas tom hyo technolojia ni ya gharama sana kwa watu wanaoanza,labda awepo muwezeshaji kama mkopo ambao pia ni vigum kupata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…