Pre GE2025 Vijana wafunga Ofisi ya Katibu wa UVCCM Mufindi

Pre GE2025 Vijana wafunga Ofisi ya Katibu wa UVCCM Mufindi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

peno hasegawa

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2016
Posts
14,255
Reaction score
23,949

Umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa wamefunga ofisi ya umoja huo wakilalamika kutoridhishwa na utendaji kazi wa Katibu wao, Aizaki Mbuya.

Vijana hao wamefanya shughuli hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Christian Mahenge.

Hata hivyo, Mahenge ametakiwa kufika kwenye kikao cha Kamati ya Maadili ya CCM Wilaya ya Mufindi, kueleza kwa nini wamechukua hatua hiyo.

Akizungumzia tukio hilo, Mahenge amemtuhumu Mbuya kuwa amekuwa akishindwa kutekeleza majumu yake ipasavyo huku fedha za umoja huo zikitafunwa.

Aidha Mahenge amesema umoja huo una miradi mingi lakini fedha zinazokusanywa zimekuwa zikitumika vibaya.
 
Back
Top Bottom