peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 14,255
- 23,949
Umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa wamefunga ofisi ya umoja huo wakilalamika kutoridhishwa na utendaji kazi wa Katibu wao, Aizaki Mbuya.
Vijana hao wamefanya shughuli hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Christian Mahenge.
Hata hivyo, Mahenge ametakiwa kufika kwenye kikao cha Kamati ya Maadili ya CCM Wilaya ya Mufindi, kueleza kwa nini wamechukua hatua hiyo.
Akizungumzia tukio hilo, Mahenge amemtuhumu Mbuya kuwa amekuwa akishindwa kutekeleza majumu yake ipasavyo huku fedha za umoja huo zikitafunwa.
Aidha Mahenge amesema umoja huo una miradi mingi lakini fedha zinazokusanywa zimekuwa zikitumika vibaya.