Vijembe vya mpambe/Afisa wa GSM aliyekuwepo kwenye kutia saini mkataba hewa wa udhamini

Vijembe vya mpambe/Afisa wa GSM aliyekuwepo kwenye kutia saini mkataba hewa wa udhamini

njaakalihatari

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2019
Posts
4,081
Reaction score
8,671
Amini usiamini hawa jamaa wanadai ni kampuni iliyoko serious na ilikuwa inataka kufanya kazi na simba ili biashara yao itangazwe..anyway sishangai sana maana wao hata kuikongoroa logo ya NBC hawakuona shida wanenda kisela mno, vuluvululu.

Embu soma upuuzi huu ulioandikwa na mpambe/afisa wa Gsm baada ya hafla ya kusaini mkataba hewa wa udhamini iliyohudhuriwa na utopolo fc pekee.

lopolopo gsm.png
 
Gharibu Said Mohamed Haa Hiyari Ni Yako Rangi Uitakayo
Majizi Haya!! Yamejaa Ghiriba Kwenye Mpira
 
wakaweka na cheki kabisa eti kumbe watu wamevalishwa matangazo miezi mitatu bila malipo
Sasa hapo nani aliyevunja mkataba?vipengere vya mkataba vinataka timu zote 16, zivae logo yake, timu moja imekataa na hata mabango yake, hayatakiwi uwanjani, TFF, ndio ameshindwa kutimiza matakwa ya ki mkataba.
 
Mwisho Wa Ubaya Ni Aibu
Ndiyo Gharibu Said Mohamed Anaumbuka Mchana Kweupe Watu Wanaona Hadharani
Hilo jinga lilikuwa linalalamika jezi ya simba ina makorokoro mengi kama team za sudan halafu yeye na matapeli wenzake wanalilia korokoro la gsm liongezwe kwenye bega la kushoto
 
Sasa hapo nani aliyevunja mkataba?vipengere vya mkataba vinataka timu zote 16, zivae logo yake, timu moja imekataa na hata mabango yake, hayatakiwi uwanjani, TFF, ndio ameshindwa kutimiza matakwa ya ki mkataba.
Kumbe target ilikuwa ni simba vipi ingegomea namungo ingevunja mkataba?
 
Sasa hapo nani aliyevunja mkataba?vipengere vya mkataba vinataka timu zote 16, zivae logo yake, timu moja imekataa na hata mabango yake, hayatakiwi uwanjani, TFF, ndio ameshindwa kutimiza matakwa ya ki mkataba.
ila nataka niulize swali. Je GSM yenyewe wakati wakuja kudhamini je ilisoma kanuni ya udhamini vizuri au ni janja janja. Manake kanuni inasema endapo club ikigoma itachuliwa hatua ambayo nikupigwa fine ya shs 3.sasa bac je kanuni hii GSM aliipitia?

Hoja sio kulazimisha vilabu vyote 16 vivae logo manake hata yanga alikiuka masharti ya kuvae nembo ya mdhamini mkuu NBC.alikiukaje kwa kubadilisha rangi ya nembo Bali sikutokuvaa wanajificha kwenye kuvaa kua aahaa sisi tunavaa je ndio nembo iliokusudiwa au ulitengeza yako ambayo inafanana na ile original ya NBC ya twiga mwekundu.

Pamoja na hao yote NBC yeye alielewa kipengele chauzamini kinasemaje .angekua Kama GSM angejitoa kwa madai kua TFF haijatimiza makubaliano Kuna club imebadilisha nembo yake .zile timu 15 ni haki kabisaa zilipwe pesa zao
 
Amini usiamini hawa jamaa wanadai ni kampuni iliyoko serious na ilikuwa inataka kufanya kazi na simba ili biashara yao itangazwe..anyway sishangai sana maana wao hata kuikongoroa logo ya NBC hawakuona shida wanenda kisela mno, vuluvululu.

Embu soma upuuzi huu ulioandikwa na mpambe/afisa wa Gsm baada ya hafla ya kusaini mkataba hewa wa udhamini iliyohudhuriwa na utopolo fc pekee.

View attachment 2113960
Hahahaa, kwa hakuna utofauti na yule Mangungo wa msovero? So they are all bogus!
 
Yanga wakatae wakubali Haji Manara anawaharibia sana,na kwa vile ameletwa na tajiri kubwa Ghalib basi viongozi wote wa Yanga wanakubali kila upuuzi wa Haji. Haji huyu ndiye alianza kutia mchanga kitumbua cha mkataba wa GSM na TFF kwa uropokaji wake kuikejeli Simba. Haji huyu kidogo aigharimu Yanga kuadhibiwa na CAF kwa utovu wa nidhamu aliofanya kule Port Harcourt na hata hii press conference yao ya malalamiko imezidi kuichafua Yanga. Haji ataendelea kuiharibia sana Yanga kwani ana mihemko ya kutaka kutafuta uhalali wa kuwa mwana Yanga ilhali inajulikana kabisa kuwa huyu ni Simba lia lia na yuko hapo kutengeneza hela kutoka kwa swahiba wake Ghalib.
 
Haji manara ni agent wetu pale tunaita external asset at Jangwani fuatilia mlolongo wote pale na matukio anayofanya hayatokei tu 😁😁Akimaliza kazi anarudi nyumbani
 
Yaani Simba inapendelewa hadi GSM kajitoa kudhamini Ligi😂😂
 
Back
Top Bottom