Vikao lukuki vya Waziri Makamba na mabepari wa gesi na mafuta vinafikirisha

Vikao lukuki vya Waziri Makamba na mabepari wa gesi na mafuta vinafikirisha

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Mheshimiwa JPM alikuwa na mapungufu mengi lakini jambo moja kwa hakika ni alikuwa hawezi kukaa na dukuduku moyoni. Hata alipowatumbua watu aliwananga hadharani kwanini amewala vichwa.

Wakati anatutangazia kuwa tusahau kuhusu gesi ya Mtwara kwakua tulishapigwa na hivyo basi tujikite kwenye mradi wa kizalendo wa JNHPP alituambia waziwazi. Inawezekana mambo haya yalikuwa SIRI lakini mzee baba alimwaga mchele kwenye kuku wengi

NI wazi kuwa mabepari na mabeberu yaliyokuwa yanatafuta kutupiga kwenye sekta hii ya gesi na mafuta hayakufurahia, kwani wengi walitegemea serikali kupitia TANESCO ndio awe mteja mkubwa wa gesi hiyo ambayo tungeuziwa kwa bei mbaya huku mafisadi yakijipatia % zao.

Lakini ndio hivyo tena, mzee baba hatunaye tena, na sasa wale vijana wa awamu ya nne wamerudi. Huyu Mh. Makamba kaanza kwa vikao lukuki na hao mabepari, kisha tunaanza kutangaziwa upungufu wa maji kwenye mabwawa yetu ambao sio wa kweli. Lengo ni nini hasa?

Wazalendo uchwara fanyeni kazi yenu vizuri, lindeni maslahi ya nchi. Achaneni na mambo ya kijinga ya kukimbizana na CDM, lindeni rasilimali za nchi dhidi ya maadui wa ndani na nje.
 
[emoji30]
20211123_161945.jpg
 
JPM kafa kaoza muacheni Samia na Mawaziri wake wachape kazi.

Songa mbele January Makamba, una maadui wengi ila utashinda tu.

Kosa lako ni "URAIS" tu ndio utachafuliwa kila kona.
 
Mzee baba amwkuta miktaba iliishasainiwa hadu gharama ya kununua hiyo gas..Hata makamba kaufyata kaamua kuhamasisha wawekeze kwwnye umeme wa jua na upepo
Kule kwenye umeme wa upepo nako kuna swahiba wake huyu Makamba,anaitwa Shamte na kampuni yake Wind African Energy.
Huyo ndio ring leader wa hili sakata la sasa.
 
Sasa hapa wa kumlaumu ni Makamba ama aliyemteua? hebu nendeni moja kwa moja kwenye mada.. Btn mliambiwa mapema kabisa wekeni mikataba yote WAZI wananchi wanaojua kusoma wasome HAMTAKI.

Sasa kilichomo ndani ya mkataba wa GESI ya Ntwara hatukijui hata wewe mwandishi hukijui - haya kilichomo ndani ya Ujenzi wa hilo bwawa la kufua umeme huko Rufiji hatukijui, sasa wa kulaumiwa ni nani hapa? SIRI ndani ya SIRI hadi lini ndugu zangu ? matokeo ya SIRI ndiyo haya - umeme hauwaki na maji hayatoki na wa kumlaumu hayupo. Makamba mnamuonea bure.
 
Sasa hapa wa kumlaumu ni Makamba ama aliyemteua? hebu nendeni moja kwa moja kwenye mada.. Btn mliambiwa mapema kabisa wekeni mikataba yote WAZI wananchi wanaojua kusoma wasome HAMTAKI.

Sasa kilichomo ndani ya mkataba wa GESI ya Ntwara hatukijui hata wewe mwandishi hukijui - haya kilichomo ndani ya Ujenzi wa hilo bwawa la kufua umeme huko Rufiji hatukijui, sasa wa kulaumiwa ni nani hapa? SIRI ndani ya SIRI hadi lini ndugu zangu ? matokeo ya SIRI ndiyo haya - umeme hauwaki na maji hayatoki na wa kumlaumu hayupo. Makamba mnamuonea bure.
Habari zake za kusema kuna ukame ndio zina tushtua. Wakati wa richmond watu walitengeneza tatizo la umeme kisha wakatupiga mabilioni kwa mgongo wa kuzalisha umeme wa dharura.
 
Kesho anakuja na suluhisho Labda ndo walilompa wenye gesi yao.
Richmond ilikuwa ni suluhisho pia, yaani watu walitengeneza tatizo la mgao wa umeme kisha wakaja na solution. Matokeo yake tukapigwa mabilioni. Ngoja tuone kesho.
 
JPM kafa kaoza muacheni Samia na Mawaziri wake wachape kazi.

Songa mbele January Makamba, una maadui wengi ila utashinda tu.

Kosa lako ni "URAIS" tu ndio utachafuliwa kila kona.
Sisi kazi yetu ni kusema panapobidi kusema, ikija Richmond nyingine msije sema hatukuonya, mabepari wamerudi kwa kasi ya umeme.
 
Huyu Makamba hadi anafika 2030 atasababisha vifo vya BP kwa wenye chuki naye wengi sana!! Mwanzo yalianza majungu kwa Mwigulu, yakaonekana hayana kiki, yamehamia kwa Makamba!! Kwa siku lazima "kakikundi ka chuki" kaanzishe threads si chini ya 10 kuhusu JM, jambo jema ni kwamba Kiongozi wa sasa haishi kwa kusikiliza "Wapika majungu wa mitandaoni walioshindwa maisha", Anaishi kwa Ethics za kiuongozi alizofundisha since akiwa kijana.
 
Wazalendo wakweli wanatakiwa kujua kwamba chadema sio adui number moja wa taifa hili,adui #1 ni msoga team kinachouma zaidi ni kakikundi ka watu wachache sana uki eliminate hao tutasonga mbele kama taifa.
 
Back
Top Bottom