Vikosi vya waasi wa SDF vilivyofadhiliwa na US vyajiunga na serikali mpya ya Syria.Ni pigo kwa nguvu za utandawazi wa Marekani.

Vikosi vya waasi wa SDF vilivyofadhiliwa na US vyajiunga na serikali mpya ya Syria.Ni pigo kwa nguvu za utandawazi wa Marekani.

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Makubaliano yamefikiwa baina ya serikali mpya ya Syria na kundi la kikurdi la SDF ili kulijenga upya taifa lao ambalo limekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa zaidi ya miaka 14.
Kundi hilo chini ya kiongozi wao aitwaye Mazloum Abdi limetia saini ya kushiriki kwenye uongozi wa serikali mpya japo muafaka wa mwisho kuhusiana na silaha walizonazo bado haujafikiwa.
Kundi la SDF linalopatikana kaskazini mashariki mwa nchi hiyo ni kundi lenye ugomvi na serikali ya Uturuki na linakalia eneo lenye utajiri mkubwa wa gesi na mafuta.
Hivi karibuni kiongozi wa kikurdi ambaye ana mafungamano na wakurdi hao ametiliana saini na serikali ya Uturuki ili kumaliza ugomvi uliodumu kwa miongo kadhaa,
Inasemekana sababu mojawapo iliyowafanya viongozi wa kundi hilo la SDF kutiliana saini ya amani na serikali mpya ya Syria ni kutokana na kuhofia sera za raisi mpya wa Marekani,Donald Trump ambaye wakati wowote anaweza akaondosha vikosi vyake eneo na kukatisha misaada yote iliyokuwa ikipokea kutoka Marekani.

Syria's government signs a breakthrough deal with Kurdish-led authorities in the northeast

 
ni machafuko na mvurugiko tu na sio amani ya kweli
Jihadists kamwe hawawezi kukubali lakini kwa wale wanauelewa ukweli wanakubali vema kwamba Trump sio belligerent.
 
Wagonjwa wengi wa ukimwi wasio na uwezo wanawaza sana! Nawasubiria na wale wanaosema bora ukimwi kuliko kisukari muda utasema!
 
Subiri Syria ikija kusaini mkataba wa Amani na Israel muanze kuwatukana
Mkataba huo utakuwa wa kutafuta nafuu kutoka Syria kama ule wa Gaza na hautakuwa kwa maslahi ya Israel pekee.
 
Back
Top Bottom