Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 57,951
- 32,619
Tuesday, April 27, 2010 5:05 PM
Tetemeko la ardhi limetokea kweli katika siku ambayo wanawake toka sehemu mbali mbali duniani walivaa vimini na wengine kuonyesha sehemu za matiti yao ili kupinga kauli za kiongozi wa kidini wa Iran aliyesema kuwa vimini vya wanawake ndivyo vinavyosababisha mabalaa duniani.Kampeni ya wanawake zaidi ya laki moja na nusu toka sehemu mbalimbali duniani kupinga kauli ya kiongozi wa kidini wa Iran kuwa wanawake wanaovaa vimini na nguo zisizo za heshima wanasababisha matetemeko ya ardhi imeula wa chuya baada ya tetemeko la ardhi kutokea kweli walipoamua kuvaa vimini na kuonyesha matiti yao.
Tetemeko kubwa la ardhi lenye ukubwa wa 6.9 lilitokea nchini Taiwan na kusababisha majengo kuyumba na kutokea kwa mmonyoko wa ardhi uliopelekea kuzikwa kwa magari matatu.
Hakuna taarifa ya vifo katika tetemeko hilo la ardhi lakini tetemeko hilo limewakatisha tamaa viongozi wa kampeni ya BoobQuaqe iliyoanzishwa kwenye mtandao wa FaceBook.
Akiongea katika sala ya ijumaa mjini Tehran nchini Iran aprili 16 mwaka huu,
mmoja wa viongozi wa juu wa kidini wa Iran, Ayatollah Kazem Sedighi alisema "Wanawake wengi siku hizi hawavai nguo za heshima na matokeo yake wanawachanganya wanaume na kupelekea kuongezeka kwa matendo ya zinaa ambayo ndiyo yanayosababisha matetemeko ya ardhi na mabalaa duniani".
"Majanga yanayotokea duniani yanatokana na madhambi ya watu", aliongeza Ayatollah Sedighi.
Kauli hiyo ilipelekea mwanafunzi Jennifer McCreight, 22 wa Indiana Marekani, aanzishe kundi kwenye facebook kupinga kauli za kiongozi huyo wa kidini wa Iran.
Jennifer alianzisha kundi linaloitwa "BoobQuaqe" kwenye Facebook ambalo liliwahimiza wanawake kuyaonyesha matiti yao hadharani majira ya mchana jana tarehe 26 aprili.
Akiliongelea tetemeko la ardhi lililotokea nchini Taiwan, Jennifer alisema kuwa matetemeko ya ardhi yenye ukubwa kati ya 6 na 6.9 hutokea mara moja kwa mwaka, kama likitokea tetemeko jingine ndani ya masaa 24 basi tutaanza kusali na kuvaa nguo za heshima.
NIFAHAMISHE.COM
Tetemeko la ardhi limetokea kweli katika siku ambayo wanawake toka sehemu mbali mbali duniani walivaa vimini na wengine kuonyesha sehemu za matiti yao ili kupinga kauli za kiongozi wa kidini wa Iran aliyesema kuwa vimini vya wanawake ndivyo vinavyosababisha mabalaa duniani.Kampeni ya wanawake zaidi ya laki moja na nusu toka sehemu mbalimbali duniani kupinga kauli ya kiongozi wa kidini wa Iran kuwa wanawake wanaovaa vimini na nguo zisizo za heshima wanasababisha matetemeko ya ardhi imeula wa chuya baada ya tetemeko la ardhi kutokea kweli walipoamua kuvaa vimini na kuonyesha matiti yao.
Tetemeko kubwa la ardhi lenye ukubwa wa 6.9 lilitokea nchini Taiwan na kusababisha majengo kuyumba na kutokea kwa mmonyoko wa ardhi uliopelekea kuzikwa kwa magari matatu.
Hakuna taarifa ya vifo katika tetemeko hilo la ardhi lakini tetemeko hilo limewakatisha tamaa viongozi wa kampeni ya BoobQuaqe iliyoanzishwa kwenye mtandao wa FaceBook.
Akiongea katika sala ya ijumaa mjini Tehran nchini Iran aprili 16 mwaka huu,
mmoja wa viongozi wa juu wa kidini wa Iran, Ayatollah Kazem Sedighi alisema "Wanawake wengi siku hizi hawavai nguo za heshima na matokeo yake wanawachanganya wanaume na kupelekea kuongezeka kwa matendo ya zinaa ambayo ndiyo yanayosababisha matetemeko ya ardhi na mabalaa duniani".
"Majanga yanayotokea duniani yanatokana na madhambi ya watu", aliongeza Ayatollah Sedighi.
Kauli hiyo ilipelekea mwanafunzi Jennifer McCreight, 22 wa Indiana Marekani, aanzishe kundi kwenye facebook kupinga kauli za kiongozi huyo wa kidini wa Iran.
Jennifer alianzisha kundi linaloitwa "BoobQuaqe" kwenye Facebook ambalo liliwahimiza wanawake kuyaonyesha matiti yao hadharani majira ya mchana jana tarehe 26 aprili.
Akiliongelea tetemeko la ardhi lililotokea nchini Taiwan, Jennifer alisema kuwa matetemeko ya ardhi yenye ukubwa kati ya 6 na 6.9 hutokea mara moja kwa mwaka, kama likitokea tetemeko jingine ndani ya masaa 24 basi tutaanza kusali na kuvaa nguo za heshima.
NIFAHAMISHE.COM