RWANDES
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 1,788
- 4,401
Rais wa Kenya William Ruto amekanusha madai kuwa ana mpango wa kufuta ukomo wa mihula miwili ya Urais nchini humo na kuweka ukomo wa umri wa kuwania kiti cha urais kwa miaka 75.
Mjadala huo uliibuliwa hivi karibuni na Mbunge wa Fafi Salah Yakub aliyedai kuwa serikali ya Ruto inajiandaa kuja na mpango huo.
Ruto amewataka wabunge wa nchi hiyo kutanguliza miradi ambayo ina athari ya moja kwa moja kwa maisha ya Wakenya.
“Mlichaguliwa kuwatumikia wananchi masuala yao lazima yatangulie. Kama Rais, sitashiriki katika juhudi zinazolenga kuvunja Katiba kwa ajili ya ubinafsi" amesema Rais Ruto katika hotuba yake.
Mjadala huo uliibuliwa hivi karibuni na Mbunge wa Fafi Salah Yakub aliyedai kuwa serikali ya Ruto inajiandaa kuja na mpango huo.
Ruto amewataka wabunge wa nchi hiyo kutanguliza miradi ambayo ina athari ya moja kwa moja kwa maisha ya Wakenya.
“Mlichaguliwa kuwatumikia wananchi masuala yao lazima yatangulie. Kama Rais, sitashiriki katika juhudi zinazolenga kuvunja Katiba kwa ajili ya ubinafsi" amesema Rais Ruto katika hotuba yake.