Vincent "Ray" Kigosi anafaa kugombea Ubunge

Tajiri Mapesa

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2020
Posts
707
Reaction score
728
Habarini wakuu,

Natumai mu wazima wa afya njema. Naomba niende moja kwa moja kwenye mada twaja.

Nadhani tunamhamu bwana Kigosi ambaye wanamwita Ray. Wakuu hili halina ubishi huyu bwana ni bingwa wa movie za kuongoza makampuni na kukaa ofisini. Na hata ukimsikiliza pindi akiwa ameshika uhusika kwenye movie zake, hakika lazima uelewe kile alicho kenya.

Kwa hivyo mimi naweza kusema huyu bwana ana karama na weledi wa kuwa kiongozi serikalini.

Mnaonaje tumpe Ubunge wakuu.

Ni hayo tu.
 
Mara ya mwisho kuangalia Bongo movie ni pale jamaa alipofika hospitali na akapewa taarifa kuwa mgonjwa wake amefariki, ndio hapo jamaa akaanguka na kuzimia. Na nesi akapiga simu kuita ambulance. Mpaka leo sitaki kusikia kabisa habari za hawa watu.
 
Mara ya mwisho kuangalia Bongo movie ni pale jamaa alipofika hospitali na akapewa taarifa kuwa mgonjwa wake amefariki, ndio hapo jamaa akaanguka na kuzimia. Na nesi akapiga simu kuita ambulance. Mpaka leo sitaki kusikia kabisa habari za hawa watu.
Kwani haiwezekani?
 
Bado anaish kwao sinza(kwa wazazi) au ameshaama??????
 
Vinsent hafai.Bora Wema Sepetu
 
kwa bunge la tz nyakati hizi YEYOTE anafaa tu, wanaenda pale hawana utofauti wowote!.
 
Ray uigizaji wake ni wa kupayuka sijaona maajabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…