Vinicius Jr hatasafiri kwenda Paris kwa vile anajua "Hatashinda" Ballon d'Or mwaka huu

Nafikiri ni kama adhabu sababu walichezea kichapo kikubwa na real Madrid. Nafikiri yeye ndiye atayeshinda.
 
Nyota wa Real Madrid Vinicius Jr hatohudhuria tuzo za Ballon d’Or zitakazofanyika usiku wa Leo Paris Ufaransa baada ya kugundua hatoshinda tuzo hiyo usiku wa leo.


Taarifa zinasema kwamba mpaka sasa nyota Mhispania Rodri ndiyo yupo katika nafasi bora zaidi ya kushinda tuzo hiyo kubwa ulimwenguni baada ya kuisaidia timu yake ya Manchester City kushinda taji la ligi la EPL na kuweka rekodi ya kubeba mataji manne mfululizo katika ligi hiyo huku pia akitoa mchango mkubwa kwa timu yake ya taifa ya Hispania kwa kushinda taji la EURO 2024 mbele ya Uingereza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…