Viongozi serikalini wabinafsi, wezi - Naibu Waziri wa Fedha

Viongozi serikalini wabinafsi, wezi - Naibu Waziri wa Fedha

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
Imeandikwa na Maulid Ahmed
Tarehe: 9th November 2009


NAIBU Waziri wa Fedha na Uchumi, Omar Yussuf Mzee amesema,viongozi serikalini ni wabinafsi, wanajali maslahi yao kuliko ya taifa.

Mzee pia amesema, watendaji hao si waadilifu, wanashirikiana na wazabuni kuongeza bei za kununulia vifaa.

Amewaeleza wabunge kuwa, hali hiyo imebainika tangu Sheria ya Ununuzi ya Umma ya mwaka 2004 ilipoanza kutumika.

“Changamoto nyingine tangu kuanza kwa sheria hii ni uwepo wa viongozi wa umma wanaojali zaidi umimi kuliko utaifa”, amesema Mzee leo jijini Dar es Salaam wakati anafungua semina ya siku mbili kwa wabunge kuhusu taratibu za ununuzi katika sekta ya umma.

Mzee amewaeleza wajumbe wa semina hiyo iliyoandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), kuwa, kwa ujumla wamebaini kwamba, kuna uwezo mdogo wa usimamizi katika manunuzi serikalini.

Wakati anawasilisha mada kuhusu umuhimu sekta ya manunuzi katika kukuza uchumi wa taifa, Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Dk. Ramadhan Mlinga amesema, katika ukaguzi uliofanywa na mamlaka hiyo kwa taasisi za umma 100 imebainika kuwa, taasisi za umma zinatoa upendeleo wa zabuni kwa kampuni za watendaji wa taasisi za umma, ndugu zao au marafiki zao.

“Kuna kupokea bidhaa duni au kazi zenye kiwango duni tofauti na ilivyoonyeshwa kwenye nyaraka za zabuni na mikataba na kunatozwa bei kubwa kwa ununuzi wa nyaraka za zabuni hata pale isipostahili”, amesema Mlinga.

Kwa mujibu wa Mlinga pia walibaini kuwa,taasisi za umma zinaweka masharti magumu ya ushiriki wa zabuni, kutotangazwa zabuni kwa walengwa,na kuchukua muda mrefu kufanya tathmini hadi kumtangaza mshindi wa zabuni.

Amesema, PPRA imejiwekea lengo kuwa hadi mwaka 2010 asilimia 80 ya taasisi zote za umma ziwe na uwezo wa kutekeleza ipasavyo sheria ya Ununuzi na kanuni zake.

Wakati anawasilisha mada kuhusu sheria hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya chuo cha Manunuzi na Ugavi(IPS), Didas Masaburi, amewaeleza wabunge kuwa, sheria hiyo ya mwaka 2004 inahitaji kurekebishwa ili kukabiliana na changamoto mbalimbali.

“Sheria inasema zabuni zisigawiwe vipande vipande lakini wanafanya hivyo ili kukwepa kutangaza na pia bodi ya zabuni inateuliwa na Mkuu wa shirika au Katibu Mkuu lakini bodi hiyo hiyo imepewa uwezo wa kumchukulia hatua mkuu huyo hivyo si rahisi kumchukulia hatua mtu aliyewateua” amesema Masaburi.
 
Mmh kumekucha...waziri wa utawala bora kasema hakuna asie fisadi ccm...huyu nae serikali imejaa ubinafsi loh....haya bado waziri mkuu na makamu wa raisi waje na yao...hapa tushapata semi za waziri na naibu waziri klutudhihiiirishia uchafu wa ccm...nnape upo,...njo na wewe ya uvccm...usiogope bwana afukuzwi mtu si umeona mama zako na baba zako kule dododma
 
Ahsante kwa kupasua hili

Lakini, hatutaki kutafuta cheap popularity. Tueleze ni viongozi gani, walifanya nini, wapi, ushahidi uko wapi ili wawajibishwe kikamilifu na liwe funzo kwa wengine.

Maana bila kufanya hivyo utaleta matatizo mawili.

1. Utaacha mafisadi waendelee kufanya ufisadi bila kudhibitiwa.

2.Utawapaka matope viongozi wengine serikalini ambao hawahusiki na ufisadi huu, kwani kauli hii bila majina na details itaonekana ku apply kwa viongozi wote serikalini.naamini kuna wengine, hata kama ni wachache, ambao hawahusiki na haya.

Kwa hiyo ndugu naibu Waziri ili kumaliza vita hii uliyoanzisha mwaga details hizo uonekana kweli unamaanisha unachosema. Ama sivyo utaonekana msanii unayetaka kuitumia vita dhidi ya ufisadi kujipatia umaarufu tu, hususan wakati huu ambao uchaguzi unajongea.
 
'Viongozi serikalini wabinafsi, wezi'

Imeandikwa na Maulid Ahmed

NAIBU Waziri wa Fedha na Uchumi, Omar Yussuf Mzee amesema,viongozi serikalini ni wabinafsi, wanajali maslahi yao kuliko ya taifa.

Mzee pia amesema, watendaji hao si waadilifu, wanashirikiana na wazabuni kuongeza bei za kununulia vifaa.

Amewaeleza wabunge kuwa, hali hiyo imebainika tangu Sheria ya Ununuzi ya Umma ya mwaka 2004 ilipoanza kutumika.

“Changamoto nyingine tangu kuanza kwa sheria hii ni uwepo wa viongozi wa umma wanaojali zaidi umimi kuliko utaifa”, amesema Mzee leo jijini Dar es Salaam wakati anafungua semina ya siku mbili kwa wabunge kuhusu taratibu za ununuzi katika sekta ya umma.

Mzee amewaeleza wajumbe wa semina hiyo iliyoandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), kuwa, kwa ujumla wamebaini kwamba, kuna uwezo mdogo wa usimamizi katika manunuzi serikalini.

Wakati anawasilisha mada kuhusu umuhimu sekta ya manunuzi katika kukuza uchumi wa taifa, Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Dk. Ramadhan Mlinga amesema, katika ukaguzi uliofanywa na mamlaka hiyo kwa taasisi za umma 100 imebainika kuwa, taasisi za umma zinatoa upendeleo wa zabuni kwa kampuni za watendaji wa taasisi za umma, ndugu zao au marafiki zao.

“Kuna kupokea bidhaa duni au kazi zenye kiwango duni tofauti na ilivyoonyeshwa kwenye nyaraka za zabuni na mikataba na kunatozwa bei kubwa kwa ununuzi wa nyaraka za zabuni hata pale isipostahili”, amesema Mlinga.

Kwa mujibu wa Mlinga pia walibaini kuwa,taasisi za umma zinaweka masharti magumu ya ushiriki wa zabuni, kutotangazwa zabuni kwa walengwa,na kuchukua muda mrefu kufanya tathmini hadi kumtangaza mshindi wa zabuni.

Amesema, PPRA imejiwekea lengo kuwa hadi mwaka 2010 asilimia 80 ya taasisi zote za umma ziwe na uwezo wa kutekeleza ipasavyo sheria ya Ununuzi na kanuni zake.

Wakati anawasilisha mada kuhusu sheria hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya chuo cha Manunuzi na Ugavi(IPS), Didas Masaburi, amewaeleza wabunge kuwa, sheria hiyo ya mwaka 2004 inahitaji kurekebishwa ili kukabiliana na changamoto mbalimbali.

“Sheria inasema zabuni zisigawiwe vipande vipande lakini wanafanya hivyo ili kukwepa kutangaza na pia bodi ya zabuni inateuliwa na Mkuu wa shirika au Katibu Mkuu lakini bodi hiyo hiyo imepewa uwezo wa kumchukulia hatua mkuu huyo hivyo si rahisi kumchukulia hatua mtu aliyewateua” amesema Masaburi.

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=4312
 
Kila Mtu anasema Lwake sasa...Kuna Mmomonyoko mkubwa wa maadili kwenye serikali ya Muungwana...Serikali imekuwa kama danguro,hakuna heshima hata kidogo!Inasikitisha...Historia itawaumbua hawa watawala.
 
Kumbe hata serikalini nako kuna makundi kama bungeni? Kweli tunayoyaona ni kivuli cha kuendesha mambo yetu kwa misingi ya uongo uongo
 
Sidhani kama WaTz wanajua maana ya sheria! It appears to be a grossly misunderstood concept!
 
Nashukuru kwa kupasua jibu kwani tusiposhiriki vita hii ya kujitolea basi nchi hii itageuka nchi ya kifisadi. Hivi mp haoni haya?? Au na yeye ana ndugu??? Ni mzabuni?
 
Kila Mtu anasema Lwake sasa...Kuna Mmomonyoko mkubwa wa maadili kwenye serikali ya Muungwana...Serikali imekuwa kama danguro,hakuna heshima hata kidogo!Inasikitisha...Historia itawaumbua hawa watawala.


Hakuna serikali hapa, it is agroup of selfish comedians masquerading as a government!!
 
Imeandikwa na Maulid Ahmed
Tarehe: 9th November 2009

NAIBU Waziri wa Fedha na Uchumi, Omar Yussuf Mzee amesema,viongozi serikalini ni wabinafsi, wanajali maslahi yao kuliko ya taifa.

Mzee pia amesema, watendaji hao si waadilifu, wanashirikiana na wazabuni kuongeza bei za kununulia vifaa.

Amewaeleza wabunge kuwa, hali hiyo imebainika tangu Sheria ya Ununuzi ya Umma ya mwaka 2004 ilipoanza kutumika.

“Changamoto nyingine tangu kuanza kwa sheria hii ni uwepo wa viongozi wa umma wanaojali zaidi umimi kuliko utaifa”, amesema Mzee leo jijini Dar es Salaam wakati anafungua semina ya siku mbili kwa wabunge kuhusu taratibu za ununuzi katika sekta ya umma.

Mzee amewaeleza wajumbe wa semina hiyo iliyoandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), kuwa, kwa ujumla wamebaini kwamba, kuna uwezo mdogo wa usimamizi katika manunuzi serikalini.

Wakati anawasilisha mada kuhusu umuhimu sekta ya manunuzi katika kukuza uchumi wa taifa, Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Dk. Ramadhan Mlinga amesema, katika ukaguzi uliofanywa na mamlaka hiyo kwa taasisi za umma 100 imebainika kuwa, taasisi za umma zinatoa upendeleo wa zabuni kwa kampuni za watendaji wa taasisi za umma, ndugu zao au marafiki zao.

“Kuna kupokea bidhaa duni au kazi zenye kiwango duni tofauti na ilivyoonyeshwa kwenye nyaraka za zabuni na mikataba na kunatozwa bei kubwa kwa ununuzi wa nyaraka za zabuni hata pale isipostahili”, amesema Mlinga.

Kwa mujibu wa Mlinga pia walibaini kuwa,taasisi za umma zinaweka masharti magumu ya ushiriki wa zabuni, kutotangazwa zabuni kwa walengwa,na kuchukua muda mrefu kufanya tathmini hadi kumtangaza mshindi wa zabuni.

Amesema, PPRA imejiwekea lengo kuwa hadi mwaka 2010 asilimia 80 ya taasisi zote za umma ziwe na uwezo wa kutekeleza ipasavyo sheria ya Ununuzi na kanuni zake.

Wakati anawasilisha mada kuhusu sheria hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya chuo cha Manunuzi na Ugavi(IPS), Didas Masaburi, amewaeleza wabunge kuwa, sheria hiyo ya mwaka 2004 inahitaji kurekebishwa ili kukabiliana na changamoto mbalimbali.

“Sheria inasema zabuni zisigawiwe vipande vipande lakini wanafanya hivyo ili kukwepa kutangaza na pia bodi ya zabuni inateuliwa na Mkuu wa shirika au Katibu Mkuu lakini bodi hiyo hiyo imepewa uwezo wa kumchukulia hatua mkuu huyo hivyo si rahisi kumchukulia hatua mtu aliyewateua” amesema Masaburi.

Nayeye pia yumo asiwasingizie wenzie apate umaarufu kirahisi... km analijua hilo kachukua hatua gani tangu agundue hayo mauchafu???
 
Back
Top Bottom