Mwishokambi
JF-Expert Member
- Nov 23, 2020
- 390
- 1,425
Kamati ya usajili ya Simba imeyakata majina ya baadhi ya wagombea akiwemo Godfrey Nyange Kaburu na mafia Idd Kajuna bila kutueleza kinagaubaga sababu za kuwakata ni nini hasa. Na badala yake wamerudisha jina la mwanasiasa Murtaza Mangungu.
Simba, ikiwa chini ya Mangungu imekuwa mnyela mno kwa Yanga na hakuna dalili zozote za kuifunga Yanga chini ya uongozi wa Mangungu.
Simba ikiwa chini ya Mangungu haina mafanikio yoyote zaid ya kuingia makundi, ubingwa wa bara umepotea msimu uliopita na mwaka huu unapotea tena.
Mangungu sio kwamba hana uwezo hapana, isipokuwa Mangungu siasa za mpira wetu hazijui tofauti na akina Idd Kajuna, mimi naona kamati ya uchaguzi imetukosea sana, kila niwaangaliapo wagombea naiona Simba inakwenda kudidimia, kabisa kabisa.
Mwingine ni Asha Baraka, hivi huyo dada anaongea nini kwenye bodi? Mambo ya Twanga Pepeta na Simba wapi na wap, tunahitaji wagombea wawe na uwezo kiuchumi, sio wagombea ukiwapa elfu 3 tu ishu zote ziko G..M pale Kigamboni.
Kazi tunayo kiukweli.
Sent from my SM-F916B using JamiiForums mobile app
Simba, ikiwa chini ya Mangungu imekuwa mnyela mno kwa Yanga na hakuna dalili zozote za kuifunga Yanga chini ya uongozi wa Mangungu.
Simba ikiwa chini ya Mangungu haina mafanikio yoyote zaid ya kuingia makundi, ubingwa wa bara umepotea msimu uliopita na mwaka huu unapotea tena.
Mangungu sio kwamba hana uwezo hapana, isipokuwa Mangungu siasa za mpira wetu hazijui tofauti na akina Idd Kajuna, mimi naona kamati ya uchaguzi imetukosea sana, kila niwaangaliapo wagombea naiona Simba inakwenda kudidimia, kabisa kabisa.
Mwingine ni Asha Baraka, hivi huyo dada anaongea nini kwenye bodi? Mambo ya Twanga Pepeta na Simba wapi na wap, tunahitaji wagombea wawe na uwezo kiuchumi, sio wagombea ukiwapa elfu 3 tu ishu zote ziko G..M pale Kigamboni.
Kazi tunayo kiukweli.
Sent from my SM-F916B using JamiiForums mobile app