Pre GE2025 Viongozi wa Dini wanatakiwa kuwahimiza waumini wao kutokupokea rushwa kipindi cha uchaguzi, wachague wadilifu ili tuwe na serikali tukufu

Pre GE2025 Viongozi wa Dini wanatakiwa kuwahimiza waumini wao kutokupokea rushwa kipindi cha uchaguzi, wachague wadilifu ili tuwe na serikali tukufu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

ZALEMDA

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2017
Posts
1,956
Reaction score
2,225
Tanzania imebahatika kuwa na waumini wa dini kuu mbili Ukristo na uislam. Dini hizi zinafundisha maadili ya kukataa rushwa, udadilifu, kuheshimiana, kutenda mema kwa wote ili tuweze kujikomboa kutoa umaskini hatuna budi kuchagua viongozi wacha Mungu, tena wadilifu.

Utakuwa hujajitendea haki kama utapokea rushwa, hongo ili umchague kiongozi wako ambaye anatakiwa kukuongoza kuelekea kwenye maendeleo yako wewe na watoto wako na nchi yako kwa ujumla.

Soma: Kuelekea 2025 - Kinana: Rushwa ni adui wa haki, Dini zote zinakataza na chama chetu kinakataza

Hivyo kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 2024, na uchaguzi mkuu 2025 chagua kiongozi ambaye unajua ni mwadilifu, yani pale kwenye jamii unaona namna alivyo mwadilifu sana kwa kwenda kanisani au msikitini,ana tenda mema, anakataa rushwa,anawajali maskini na wanyongwe,tena ni msomi.

Kwenye uchaguzi kataa mtu wa namna hii:

1. Siyo mwadilifu
2. Mshirikina
3. Mwenye majivuno
4. Mfanyabiashara asiyelipa kodi
5. Fanyabiashara au mwenye fedha lakini hachangii maendeleo ya jamii
6. Haendi kanisani au msikitini
7. Msomi lakini haonekani kwenye vikao vya kijamii

Wanaotaka kupata nafasi za uongozi sisi wananchi wa chini tuwajadili kwanza huko makanisani, misikitini, kwenye vijiwe, kwenye midahalo. Tusisubiri vyama vyetu vituchagulie. Yeyote atakayeonyesha dalili za rushwa tumkatae.

UKIPOKEA RUSHWA YA MWANASIASA ILI UMCHAGUE, UNAUZA UTU WAKO KAMA VILE ESSAU ALIVYOUZA HAKI YAKE YA MZALIWA WA KWANZA. NI KUJIDHALILISHA, KUWAUZA WATOTO WAKO NA WAJUKUU ZAKO NA NCHI YAKO KWA BEI YA KARANGA
 
Tatizo siyo kuhimizana ila kujisimamia wenyewe, umasikini na ujinga ni janga la Taifa ndugu. Ukimhubiria na kumhimiza mwenye njaa bila kumpa chakula ni sawa na kupuliza upepo.
.........................................
Njaa mbaya.
 
Tatizo siyo kuhimizana ila kujisimamia wenyewe, umasikini na ujinga ni janga la Taifa ndugu. Ukimhubiria na kumhimiza mwenye njaa bila kumpa chakula ni sawa na kupuliza upepo.
.........................................
Njaa mbaya.
OK.sasa njaa tutaiondoaje bila kuchagua viongozi wadilifu.? kumbuka kwamba siku ya ukombozi haiiji kiurahisi.mahala pengine lazima ufunge( usile chakula ) ili upate hitaji lako kutoka kwa MUNGU.kwa hiyo siyo sababu kwa mwenye njaa kupokea rushwa kwa chakula cha siku moja kama vile ESSAU
 
OK.sasa njaa tutaiondoaje bila kuchagua viongozi wadilifu.? kumbuka kwamba siku ya ukombozi haiiji kiurahisi.mahala pengine lazima ufunge( usile chakula ) ili upate hitaji lako kutoka kwa MUNGU.kwa hiyo siyo sababu kwa mwenye njaa kupokea rushwa kwa chakula cha siku moja kama vile ESSAU
Esau aliuza uzaliwa wake kwa dengu nyekundu....Mkuu njaa siyo jambo jema, mtu anaweza akajidhalilisha kuliko tunavyodhani.
By the way njaa ninayoizungumzia hapa ni zaidi ya chakula ila ni kukosa maarifa na kutokujitambua yaani njaa iliyohama kutoka tumboni na kuja kichwani, njaa hii ni njaa hatari sana.
 
Tanzania imebahatika kuwa na waumini wa dini kuu mbili Ukristo na uislam. Dini hizi zinafundisha maadili ya kukataa rushwa, udadilifu, kuheshimiana, kutenda mema kwa wote ili tuweze kujikomboa kutoa umaskini hatuna budi kuchagua viongozi wacha Mungu, tena wadilifu.

Utakuwa hujajitendea haki kama utapokea rushwa, hongo ili umchague kiongozi wako ambaye anatakiwa kukuongoza kuelekea kwenye maendeleo yako wewe na watoto wako na nchi yako kwa ujumla.

Soma: Kuelekea 2025 - Kinana: Rushwa ni adui wa haki, Dini zote zinakataza na chama chetu kinakataza

Hivyo kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 2024, na uchaguzi mkuu 2025 chagua kiongozi ambaye unajua ni mwadilifu, yani pale kwenye jamii unaona namna alivyo mwadilifu sana kwa kwenda kanisani au msikitini,ana tenda mema, anakataa rushwa,anawajali maskini na wanyongwe,tena ni msomi.

Kwenye uchaguzi kataa mtu wa namna hii:

1. Siyo mwadilifu
2. Mshirikina
3. Mwenye majivuno
4. Mfanyabiashara asiyelipa kodi
5. Fanyabiashara au mwenye fedha lakini hachangii maendeleo ya jamii
6. Haendi kanisani au msikitini
7. Msomi lakini haonekani kwenye vikao vya kijamii

Wanaotaka kupata nafasi za uongozi sisi wananchi wa chini tuwajadili kwanza huko makanisani, misikitini, kwenye vijiwe, kwenye midahalo. Tusisubiri vyama vyetu vituchagulie. Yeyote atakayeonyesha dalili za rushwa tumkatae.

UKIPOKEA RUSHWA YA MWANASIASA ILI UMCHAGUE, UNAUZA UTU WAKO KAMA VILE ESSAU ALIVYOUZA HAKI YAKE YA MZALIWA WA KWANZA. NI KUJIDHALILISHA, KUWAUZA WATOTO WAKO NA WAJUKUU ZAKO NA NCHI YAKO KWA BEI YA KARANGA
Watu tuna njaa na matatizo lukuki ikiwemo kausha damu halafu napewa suluhisho ya changamoto zangu, eti nikatae mbona nitajizima data, yaani nitaahirisha kufikiri kwa nafsi yangu, elimu inatakiwa itolewa kabla ya kupata changamoto tena inayo niwezesha kukabiliana na changamoto,
Mtizamo wangu kuhusu changamoto, (uncertainty), anaye sababisha changamoto kwa binadamu ni binadamu kwa kuto kujua ama kwa makusud, hata yeye mwenyewe anaweza kujisababishia changamoto kwa uzembe, uvivu, ujinga, hili ni somo pana na nina andiko lake najaribu kuwachangamsha akili
 
Dawa ilikuwa ni kuwapa meno makali zaidi kisheria ili wakabili suala hili.
 
Back
Top Bottom