Viongozi wa kitaifa mmekuwa watumwa wa Wamachinga

Viongozi wa kitaifa mmekuwa watumwa wa Wamachinga

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Ni wazi viongozi wa serikali wamekuwa watumwa wa wamachinga, wanawaogopa. Tanzania imekuwa ikishuhudia matukio ya moto kuunguza masoko na shule, jambo moja la kushangaza ni pale soko liunguapo, viongozi wa serikali wanaacha kazi zao na kwenda msibani! Pole na ahadi za kila aina zitatolewa.

Tukio la kuungua moto shule hupita kimyakimya kuashiria kuwa Tanzania elimu haina thamani.

Huwa hatushuhudii viongozi wakimiminika kuhani misiba ya wanafunzi kuunguliwa shule na vifaa vyao! Hapa hakuna uchungu kwa sababu hakuna kura toka kwa watoto!

Hii ni aibu kwa viongozi kuwa watumwa wa kura na madaraka! Utumwa huu ndio umewafanya viongozi wasijali ubora wa elimu ipatikanayo Tanzania.
 
Hujaonesha ufumbuzi wa tatizo bali umeongeza kwamba waongeze hatua ambazo mpera mada utatafsiri hawaogopi
 
Uongozi ni Chaka la Kupigia Hela
Utumwa huu unawafanya wamachinga kuwa na nguvu kuliko serikali, kuna siku wamachinga watatangaza baraza lao la mawaziri kutokana na kauli yao ya kutokuwa na imani na sefikali. Haya ndiyo yatakuwa matokeo ya kutegemea kura za kudanganyana.
 
Uko sooo insensitive, hiyo ni dalili ya psychopathy !
 
Back
Top Bottom