Viongozi wa posho watatufikisha wapi?

Viongozi wa posho watatufikisha wapi?

mzamifu

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2010
Posts
6,400
Reaction score
3,853
Inasikitisha kuonana kuwa viongozi wengi hapa tz ni viongozi wa posho. Yaani wanatafuta uongozi kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Wakishapata uongozi wanakuwa hawajui hata la kufanya. Watautetea mfumo uliopo hata kama wanaona kuna upungufu ili maradi wanapata maslahi yao. Hawapendi kuwasikia wapinzani wala wana harakati au watu wenye mawazo mbadala kwa vile wanaogopa kupoteza nafasi zao.
Hii inadhihirishwa na hali ya kung'ang'ania madaraka hata kama wametenda kosa. Hakuna uwajibikaji. Kwanini katika nchi zilizoendelea viongozi hujiuzulu kwa kuwajibika na sio tanzania?
Wasomi na wanazuoni wachache wamenaswa na mtego huu wameacha taaluma zao na kukimbilia siasa ili wanufaike. Viongozi wajue kuwa mahela wanyojipangia ni jasho la watanzania hivo wanapaswa kuwarudishia kwa kwawatea maendeleo. Wakiendelea kufikiria maslahi yanayoambatana na vyeo vyao bila kufikiria kwanza wanatakiwa kuwafanyia nini wananchi hatutafika popote!
 
ndugu yangu tunahitaji nabii kutuondoa kwenye hili ombwe. hebu fikiria wazo la kufuta sitting allowance viongozi wetu macho yalivyowatoka, ukiona hata waziri mkuu anashabikia basi tumekwisha. Na ushahidi upo pale tulipoona waziri mkuu na spika wamesaign posho za kikao cha muda mfupi tu! kumbuka hawa tunawahudumia kila kitu ....nguo malazi etc. Ona mpaka leo wiki ya pili wote walionekana na kamati teule wamefuja pesa za walipakodi hakuna hata mmoja aliyechukua hatua au kuchukuliwa hatua. wanaogopana.. mwaga mboga ni mwage ugali. Mungu tusaidie, nabii atapatikana tu.
 
Inasikitisha kuonana kuwa viongozi wengi hapa tz ni viongozi wa posho. Yaani wanatafuta uongozi kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Wakishapata uongozi wanakuwa hawajui hata la kufanya. Watautetea mfumo uliopo hata kama wanaona kuna upungufu ili maradi wanapata maslahi yao. Hawapendi kuwasikia wapinzani wala wana harakati au watu wenye mawazo mbadala kwa vile wanaogopa kupoteza nafasi zao.
Hii inadhihirishwa na hali ya kung'ang'ania madaraka hata kama wametenda kosa. Hakuna uwajibikaji. Kwanini katika nchi zilizoendelea viongozi hujiuzulu kwa kuwajibika na sio tanzania?
Wasomi na wanazuoni wachache wamenaswa na mtego huu wameacha taaluma zao na kukimbilia siasa ili wanufaike. Viongozi wajue kuwa mahela wanyojipangia ni jasho la watanzania hivo wanapaswa kuwarudishia kwa kwawatea maendeleo. Wakiendelea kufikiria maslahi yanayoambatana na vyeo vyao bila kufikiria kwanza wanatakiwa kuwafanyia nini wananchi hatutafika popote!

Kamuulize Anne makinda.
 
ingikuwa mimi ndio mkuu wa majeshi tanzania...ningetumia wale makomandoo kuwakangaa mafisadi wote....LOWASA,KIKWETE,RIDHIWANI,PATEL,ROSTAM, etc
 
Back
Top Bottom