mpimamstaafu
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 4,445
- 4,707
Hakika Viongozi wa Soka Nchini TFF wanapaswa nao wawe na nyuso za aibu kwa Watanzania.Toka Uongozi huu wa TFF umeingia Madarakani tumeshuhudia migogoro badala ya maendeleo ya mpira wetu.Malalamiko ya vilabu,ratiba mbovu ligi kuu,Serengeti Boys kushindwa kufuzu licha ya mashindano kufanyikia hapa nchini,Taifa Stars kufanya vibaya Afcon huko Misri,na leo Taifa Stars kushindwa kuutumia vema uwanja wa nyumbani ilipocheza na Harambee Stars ya Kenya.Timu zetu zimeshindwa kufanya vizuri kutokana na Mipango mibovu ya TFF.Matokeo hayo yamepelekea Tanzania kushuka ktk Viwango vya FIFA.Nadhani wakati umefika kwa Viongozi wa TFF wawe na sura za aibu kwa Watanzania,Kujiuzulu sio dhambi ni kuonyesha ukomavu kiuongozi hebu wachukuwe maamuzi magumu ya KUJIUZULU ili wajaribu na Watanzania wengine.