Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 1,278
- 797
VIONGOZI WA UWT WASHUHUDIA ATHARI ZA MAFURIKO RUFIJI, WATOA MSAADA WA CHAKULA NA MAHITAJI MAALUM
Viongozi wa kitaifa wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wametembelea eneo la Muhoro wilayani Rufiji lililoathiriwa na Mafuriko yaliyotokana na uwepo wa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha wilayani humo.
Katika msafara huo kutoka Ofisi ndogo ya UWT Taifa Dar es Salaam jana Aprili 17, 2024 Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) aliongozana na Naibu Katibu Mkuu wa UWT Tanzania Bara Ndg. Riziki King’wande (MNEC), Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Ndg. Tunu Kondo,Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Taifa na wajumbe wa Kamati ya Maafa ya UWT Taifa.
Mwenyekiti Chatanda na Ujumbe wake walitembelea Makazi ya watu yaliyoathirika huku wakijionea kituo cha Afya cha Muhoro kilichosimamisha utoaji wa huduma na kutembelea kambi iliyoandaliwa na Serikali kwa waarhirika wa mafuriko iliyopo eneo la Chumbi.
Mwenyekiti Chatanda ameishukuru Serikali kwa kutenga kambi maalum kwa waathirika huku akitoa pole zilizoambatana na msaada wa chakula na mahitaji maalum iliyopokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Rufuji, Mhe. Meja Edward Gowele.
“Nimshukuru sana Mwenyekiti wetu wa CCM na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta mahema,chakula na mahitaji mengine kwa kweli anawapenda wananchi wake,na sisi wanawake tukasema tuwakimbilie watanzania wenzetu hivyo niwahakikishie kuwa tupo pamoja” Alisema Mwenyekiti Chatanda.
UWT imetoa vitu mbalimbali ikiwemo Magodoro, Nguo, Chakula, Sukari, Mashuka, Chandarua na vitu vinginevyo.
Viongozi wa kitaifa wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wametembelea eneo la Muhoro wilayani Rufiji lililoathiriwa na Mafuriko yaliyotokana na uwepo wa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha wilayani humo.
Katika msafara huo kutoka Ofisi ndogo ya UWT Taifa Dar es Salaam jana Aprili 17, 2024 Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) aliongozana na Naibu Katibu Mkuu wa UWT Tanzania Bara Ndg. Riziki King’wande (MNEC), Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Ndg. Tunu Kondo,Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Taifa na wajumbe wa Kamati ya Maafa ya UWT Taifa.
Mwenyekiti Chatanda na Ujumbe wake walitembelea Makazi ya watu yaliyoathirika huku wakijionea kituo cha Afya cha Muhoro kilichosimamisha utoaji wa huduma na kutembelea kambi iliyoandaliwa na Serikali kwa waarhirika wa mafuriko iliyopo eneo la Chumbi.
Mwenyekiti Chatanda ameishukuru Serikali kwa kutenga kambi maalum kwa waathirika huku akitoa pole zilizoambatana na msaada wa chakula na mahitaji maalum iliyopokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Rufuji, Mhe. Meja Edward Gowele.
“Nimshukuru sana Mwenyekiti wetu wa CCM na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta mahema,chakula na mahitaji mengine kwa kweli anawapenda wananchi wake,na sisi wanawake tukasema tuwakimbilie watanzania wenzetu hivyo niwahakikishie kuwa tupo pamoja” Alisema Mwenyekiti Chatanda.
UWT imetoa vitu mbalimbali ikiwemo Magodoro, Nguo, Chakula, Sukari, Mashuka, Chandarua na vitu vinginevyo.