Viongozi wa Yanga waburazana mahakamani kisa maneno ya kashfa (defamation) - Imani Madega v. Yusuf Manji

Viongozi wa Yanga waburazana mahakamani kisa maneno ya kashfa (defamation) - Imani Madega v. Yusuf Manji

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Wakuu, Adv.Imani Madega Wakili Mkongwe na Mwenyekiti wa YANGA Kipindi Hicho Alimshitaki Yusuf Manji Mdhamini wa YANGA Kipindi Hicho.

Kwa Kile Alichodai Kwamba Katika Sherehe ya Kufungua Tawi la YANGA Gongo la Mboto, Manji Akiongea Kama Mgeni Rasmi Alitoa Maneno ya Kashfa Kwamba Madega Ameuza Wachezaji Muhimu wa Timu ya YANGA na Fedha Amezitumia Katika Kampeni za Ubunge, Jimbo la Chalinze.

Kwamba Maneno Hayo Yalilipotiwa na Mokiwa, Yakachapishwa na Jambo Concept Kwenye Gazeti la Jambo Leo.

Kwenye Maombi Yake Mahakamani, Adv. Madega Alidai Zaidi ya Bilioni 5 Kama Fidia Kutoka Kwa Manji.

Sasa Wazee wetu wa Mahakama Ya Rufaa Kwenye Maamuzi Yao wameona kwamba adv. Madega Ameshindwa Kuthibitisha Madai Yake Dhidi ya Manji.

Lakini Wazee wamesema Anatakiwa Kulipwa na Mokiwa, Jambo Concept na Jambo Leo Fidia ya Jumla (General Damages).
.
Sasa Kesi Imerudi Mahakama Kuu Ili Iweze Kukadiria Alipwe Kiasi Gani. [emoji1600][emoji3][emoji3][emoji1487]

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Unatafuta kiki ww habari za mwaka 2005 unazileta leo sasa apo nani kiongoz wa yanga..?
 
Chawa wa mo wameingia kazini Kwa kishindo kikuu wanayanga amkeni amkeni amkeniiiiii
 
Chawa wa mo wameingia kazini Kwa kishindo kikuu wanayanga amkeni amkeni amkeniiiiii

Huu upuuzi ni Utopolo wasiojielewa wanataka justification kuwa suala la zeruzeru linaweza kupelekwa Mahakamani, wakati hizi ni ishu mbili tofauti kanisa
 
Huu upuuzi ni Utopolo wasiojielewa wanataka justification kuwa suala la zeruzeru linaweza kupelekwa Mahakamani, wakati hizi ni ishu mbili tofauti kanisa
We mbumbumbu Kuna sehemu ametajwa zeruzeru kwenye huu uzi? Au Manara ni mumeo mpendwa?
 
Back
Top Bottom