Viongozi wa Young Africans walitudanganya kuhusu Mkataba wa Nabi?

Smart AJ

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2022
Posts
5,564
Reaction score
5,884
Feisal alisema alisainishwa mkataba wa misimu mitatu, bila kujua ilihali yeye alitaka mkataba wa miaka miwili tu. Je, tuseme walitudanganya, au walimdanganya na Profesa juu ya mkataba wake?

Kwenye taarifa ya awali ya mkataba mpya alioongeza Nabi mwaka jana, taarifa zinasema tofauti na zile ambazo zinaripoti baada ya Nabi kuondoka.

Je, tuseme viongozi wameshindwa hata mara moja kuwa wawazi?

Huu sio mwaka 2024, iweje mseme kagoma kuongeza mkataba baada ya kuisha? [emoji848]

NB: Ukishapata jibu tulia tuli!

View attachment 2659101
 
Huu sio mwaka 2024, iweje mseme kagoma kuongeza mkataba baada ya kuisha? [emoji848][emoji419][emoji375]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna taarifa official ya yanga inayosema mkataba utaisha 2024
 
Hakuna taarifa official ya yanga inayosema mkataba utaisha 2024
Unataka taarifa gani official zaidi ya taarifa iliyotolewa na Engineer Hersi na kuwekwa kwenye tovuti ya Yanga ikisema Nabi aliongezewa mkataba wa kuendeleq kubakia Jangwani mpaka 2024?

Okay, kama huamini hayo, tazama basi picha hapo.
 
Inawezekana waliomtaka wamevunja mkataba kwa style ya kuweka ela mezani Kama kweli mkataba unaisha 2024
 

Attachments

  • D810F11A-9A78-44C2-B295-274CDC41D04B.jpeg
    185 KB · Views: 2
Unataka taarifa gani official zaidi ya taarifa iliyotolewa na Engineer Hersi na kuwekwa kwenye tovuti ya Yanga ikisema Nabi aliongezewa mkataba wa kuendeleq kubakia Jangwani mpaka 2024?

Okay, kama huamini hayo, tazama basi picha hapo.
Huyo bado ni kocha, Aje mezani, huo sio utaratibu. Mikataba haivunjiki kiholela kama hataki aende CAS.
 
Sina uhakika, ila mimi nadhani Nabi hakumaliza mktaba bali ameuzwa kwa vile waliomtaka walikuja na dau kubwa mara tatu ya analopata Yanga. Katika mawasiliano ya umma, Yanga wameamua kufupisha tu kuwa amemaliza mkataba bali ukweli ni kuwa Kaizer Chiefs wamemwaga hela ndefu sana pale Yanga ili kumpata Nabi. Nasikia wako njiani kuleta nyingine nyingi sana kumnasa Mayele na baadhi ya Wachezaji wa sasa ndani ya Yanga pamoja na sehemu ya benchi la ufundi la Yanga. Hata hivyo wanayanga wasiwe na wasiwasi kwani Injinia Hersi ataanza upya na kukamilisha kila kitu kabla msimu haujaanza.
 
Sijui kwa Nini mi naona sahihi kabisa kuondoka kwa hao watu maana wametumia nguvu nyingi sana huenda wasinge deliver kwa kiwango hicho tena
Waletwe wapywa waambiwe namna wale walioondoka wameleta maendeleo Kisha wapambane kuyaleta nadhani kitu Cha muhimu ni wadhamini na admin hao wakiondoka ndio mtikisiko huwa mkubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…