Viongozi Wenye Majina ya Kughushi: Mfumo Darasa la Saba Ubadilishwe

Viongozi Wenye Majina ya Kughushi: Mfumo Darasa la Saba Ubadilishwe

Filipo Lubua

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2011
Posts
339
Reaction score
578
Wadau,

Tumeshuhudia wanafunzi wengi wakifeli darasa la saba wanavyosota mitaani bila mahali pa kwenda, hasa wazazi wao wasipokuwa na uwezo wa kuwapeleka shule binafsi.

Kwa sababu hii pia, bila shaka tumekutana na watu walioko katika kada mbalimbali wakituhumiwa kuwa na majina ya kununua baada ya kufeli mtihani wa darasa la saba. Miongoni mwa viongozi wa kitaifa waliokutana na kashfa hizi ni Naibu Waziri wa Elimu Philip Mulugo, Naibu Katibu Mkuu CUF Julius Mtatiro, na Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba.

Nikiachana na Philip Mulugo ambaye tetesi zinasema alibadili jina baada ya kumaliza kidato cha nne, Mwigulu Nchemba anasemekana kuwa jina lake halisi ni Lameck Mkumbo Madelu, wakati Julius Mtatiro akisemekana kuwa jina lake halisi ni Sunday Charles.

Mimi sihitaji kuthibitisha kama kweli viongozi hawa walinunua majina au waliiba majina kama walivyotuhumiwa. Ninachohitaji kusema hapa ni jinsi mfumo wetu wa Elimu ya Msingi unavyowanyima wanafunzi wanaofeli haki ya kuendelea na masomo. Mwanafunzi anapofeli mtihani wa Darasa la Saba (au anapofaulu lakini kwa uhaba wa shule akakosa nafasi ya kujiunga kidato cha kwanza) anakuwa hana pa kwenda, hasa wazazi wake wasipokuwa na uwezo wa kumpeleka shule binafsi. Wengi wao hutafuta njia mbadala za kuendelea na masomo, hasa kwa kununua majina ya wanafunzi walioacha shule wakiwa darasa la tano au sita. Wanaponunua majina haya, hufanya mtihani huo kwa majina feki, na wanapofaulu, hulazimika kuendelea nayo. Hili husababisha wengi kukutwa na kashfa hizi za akina Mtatiro na Mwigulu. Wengi tunawafahamu watu wa namna hiyo, hasa maeneo ya vijijini, hata mimi nimemaliza na watu wa namna hiyo.

Hoja yangu ni kuwa, kwa nini mfumo wa elimu yetu usitafutiwe njia mbadala ya kuwakaririsha wanafunzi wanaofeli darasa la saba, kama ilivyo kwa Kidato cha Pili, Nne na Sita? Kwanini wanafunzi wanaofeli darasa la saba wasipewe fursa ya kurudia mtihani, kama ilivyo kwa mitihani mingine ya ngazi zinazofuata?

Nawasilisha kwa nia njema kabisa. Nawaomba Watanzania tutoe maoni, na si kusigana kwa itikadi za kivyama au kisiasa.
 
Mie mwenyewe jina ninalotumia sio langu, ni la chalii mmoja aliacha shule akaenda kuchenji kwacha tunduma, na finalize masters na jina hilihili
 
Mie mwenyewe jina ninalotumia sio langu, ni la chalii mmoja aliacha shule akaenda kuchenji kwacha tunduma, na finalize masters na jina hilihili

Kwa hiyo nawe pia ulinunua ulipomaliza darasa la saba?
 
Na tutarajie majina megi ya watu walio na madaraka; wasio na elimu, kwa kuwa hata sasa si lazima mtu kupitia elimu ya msingi, pia si lazima mtu kufanya mtihani wa kidato cha pili. Watu wanapitia njia ya QT mwanzo mwisho...
 
Na tutarajie majina megi ya watu walio na madaraka; wasio na elimu, kwa kuwa hata sasa si lazima mtu kupitia elimu ya msingi, pia si lazima mtu kufanya mtihani wa kidato cha pili. Watu wanapitia njia ya QT mwanzo mwisho...

Huo mtihani unaoitwa QT hautofautiani sana na mtihani wa kidato cha pili. Wanafunzi wanaosoma masomo ya QT ni wale ambao wana uwezo wa kujilipia masomo hayo. Je wale watoto wa wakulima wasio na uwezo watasomaje wafelipo darasa la saba?
 
Mleta hoja ameweka hoja mbili ambazo zina maudhi tofauti ila amezikweka kama hoja moja,hapa nahisi umeteleza!

Hoja ya kwanza ni kutumia majina ya watu wengine,na hoja ya pili ni kuangalia uwezekano wa watahiniwa wa darasa la saba waliofeli kupewa nafasi nyingine ya kurudia mtihani.Hizi ni hoja mbili tofauti kabisa.Labda atuambie yeye anataka tujadili ipi.

Kwa mfano mimi binafsi nilifeli darasa la saba nikarudia kwa kununua jina nikafeli tena.Nikapelekwa private secondary school nikatumia jina langu la mwanzo(original),kuanzia hapo nimekuwa nikifaulu mitihani yangu hadi leo nakaribia kumaliza degree yangu ya udaktari wa binadamu.Hoja yangu hapa nini? Kwa mfano kama ningefaulu kwa kutumia jina la kununua hadi leo ningekuwa nalitumia.Shida iko wapi?Vyeti ninavyo nilivyosomea na kufaulu kwa juhudi zangu,nilichonunua ni jina sio vyeti.Utalamu nilionao ni halisi sio wa kununua,who cares!By the way nani mwenye jukumu la kunipangia nitumie jina gani!Jina linahusika na nini katika performance ya kitaluma?

Turudi katika uhalisia,nini lengo la kunua jina? Binafsi mimi naona ni kwa sababu mtu anahitaji nafasi nyingine ya kufanya mtihani.Ili iweje?Ili afaulu kwa kufuta makosa aliyofanya mwanzo.Halafu kusema ukweli,wanaonunua majina ni watoto wa masikini,sio matajiri! Matajiri wanunue ili iweje? Wao wanao wanapelekwa private moja kwa moja,wakati mwingine hata wale waliofaulu!Nina mifano mingi tu.Tusisahau kuwa kufaulu darasa la saba maana yake ni kwenda shule za kata za gharama nafuu!Je tajiri ampeleke mwanae huko kufanya nini?

Mimi naona hoja ya kununua majina inakuwa na mashiko ikiwa mtu atanunua cheti;lakini sio kupata nafasi kwa jina lingine,ukasota mwenyewe darasani halafu ukishapata utalamu mtu anaibuka na kusema wewe umetumia jina la mtu mwingine!That is not right, maana hata hilo jina analotaka utumie(original) hakukupa yeye na wala hajui lilipotokea!

Kila kitu kina faida na hasara zake.Wakati hasara inaonekana kama mtu ametumia jina la mtu mwingine,faida yake haifichiki.Hii ni nafasi ya mtu mwenye nia ya kujiendeleza kutumia nafasi ya mtu mwingine asiye na nia ya kujiendeleza!This is the game of chance! The time wewe unachezea nafasi yako,mwenzio anaitumia nafasi hiyo kujiendeleza.Laiti kama kusingekuwepo nafasi kama hizo,hao wanaonunua nafasi hizo wasingekuwepo.This means,tungekuwa na watu wawili mtaani wanaohangaika;yaani yule aliyechezea nafasi yake na yule aliyenyimwa nafasi hiyo.Sasa faida iko wapi?

Nini kifanyike sasa? Tusione dhambi kutumia chances chache zinazopatikana ktk kujiendeleza,bali tuone dhambi kuachezea chances adimu tunazopata.Tuwahimize watoto wetu kufanya juhudi ktk masomo yao.Huwezi ukamwondoa mwanao shuleni ukampeleka kumtumikisha shambani,biashara au ufugaji halafu mtoto mwenye nia ya kujiendeleza akitumia nafasi hiyo then unakuja hapa kulalamika!

Kuhusu waliofeli kupewa nafasi nyingine ya kujaribu tena bahati yao,hilo sina tatizo nalo.Naunga mkono hoja 100%!
 
Wanadamu hutumia njia tofauti maishani kufikia malengo. Mara nyingi njia zinazotumika kufikia malengo haya zinatofautiana sana kulingana na maeneo au matabaka ya kiuchumi.
Mfano: watu wengi waliosoma vijijini shule za msingi, walirudia mara nyingi ili waweze KUCHAGULIWA. Na kurudia huku hutumia majina ya wale walioacha shule moja kwa moja. Ninafahamu mtu aliyerudia primary school mara nne, kila mwaka akitumia majina tofauti.
*Kurudia shule ni njia ya kutafuta opportunity
*UK wanaita kujilipua - ambapo mtu hubadili majina, mwaka wa kuzaliwa na uraia ili aweze kupata ukaazi.
*Tanzania tunachohitaji ni kujua tofauti kati ya kutumia jina BANDIA au mwenye IDENTITY zaidi ya moja.
*Tutafute wenye vyeti vya kufoji na wale wenye degree feki (Sio suala la majina)
*Tutafute wenye nafasi ambazo hawastahili


Vinginevyo hii hoja itatutoa kwenye lengo kuu la kupigana na ufisadi wa elimu
 
Mleta hoja ameweka hoja mbili ambazo zina maudhi tofauti ila amezikweka kama hoja moja,hapa nahisi umeteleza!

Hoja ya kwanza ni kutumia majina ya watu wengine,na hoja ya pili ni kuangalia uwezekano wa watahiniwa wa darasa la saba waliofeli kupewa nafasi nyingine ya kurudia mtihani.Hizi ni hoja mbili tofauti kabisa.Labda atuambie yeye anataka tujadili ipi.

Kwa mfano mimi binafsi nilifeli darasa la saba nikarudia kwa kununua jina nikafeli tena.Nikapelekwa private secondary school nikatumia jina langu la mwanzo(original),kuanzia hapo nimekuwa nikifaulu mitihani yangu hadi leo nakaribia kumaliza degree yangu ya udaktari wa binadamu.Hoja yangu hapa nini? Kwa mfano kama ningefaulu kwa kutumia jina la kununua hadi leo ningekuwa nalitumia.Shida iko wapi?Vyeti ninavyo nilivyosomea na kufaulu kwa juhudi zangu,nilichonunua ni jina sio vyeti.Utalamu nilionao ni halisi sio wa kununua,who cares!By the way nani mwenye jukumu la kunipangia nitumie jina gani!Jina linahusika na nini katika performance ya kitaluma?

Turudi katika uhalisia,nini lengo la kunua jina? Binafsi mimi naona ni kwa sababu mtu anahitaji nafasi nyingine ya kufanya mtihani.Ili iweje?Ili afaulu kwa kufuta makosa aliyofanya mwanzo.Halafu kusema ukweli,wanaonunua majina ni watoto wa masikini,sio matajiri! Matajiri wanunue ili iweje? Wao wanao wanapelekwa private moja kwa moja,wakati mwingine hata wale waliofaulu!Nina mifano mingi tu.Tusisahau kuwa kufaulu darasa la saba maana yake ni kwenda shule za kata za gharama nafuu!Je tajiri ampeleke mwanae huko kufanya nini?

Mimi naona hoja ya kununua majina inakuwa na mashiko ikiwa mtu atanunua cheti;lakini sio kupata nafasi kwa jina lingine,ukasota mwenyewe darasani halafu ukishapata utalamu mtu anaibuka na kusema wewe umetumia jina la mtu mwingine!That is not right, maana hata hilo jina analotaka utumie(original) hakukupa yeye na wala hajui lilipotokea!

Kila kitu kina faida na hasara zake.Wakati hasara inaonekana kama mtu ametumia jina la mtu mwingine,faida yake haifichiki.Hii ni nafasi ya mtu mwenye nia ya kujiendeleza kutumia nafasi ya mtu mwingine asiye na nia ya kujiendeleza!This is the game of chance! The time wewe unachezea nafasi yako,mwenzio anaitumia nafasi hiyo kujiendeleza.Laiti kama kusingekuwepo nafasi kama hizo,hao wanaonunua nafasi hizo wasingekuwepo.This means,tungekuwa na watu wawili mtaani wanaohangaika;yaani yule aliyechezea nafasi yake na yule aliyenyimwa nafasi hiyo.Sasa faida iko wapi?

Nini kifanyike sasa? Tusione dhambi kutumia chances chache zinazopatikana ktk kujiendeleza,bali tuone dhambi kuachezea chances adimu tunazopata.Tuwahimize watoto wetu kufanya juhudi ktk masomo yao.Huwezi ukamwondoa mwanao shuleni ukampeleka kumtumikisha shambani,biashara au ufugaji halafu mtoto mwenye nia ya kujiendeleza akitumia nafasi hiyo then unakuja hapa kulalamika!

Kuhusu waliofeli kupewa nafasi nyingine ya kujaribu tena bahati yao,hilo sina tatizo nalo.Naunga mkono hoja 100%!

Umechangia kwa namna nzuri sana. Hapa hazijaletwa hoja mbili tofauti, hoja ni moja ila nilihusianisha tu na hao wanasiasa. Kisheria, huruhusiwi kununua jina la mtu na kuendelea nalo kama lako. Ila hoja yangu haikuwa hapo. Hoja yangu ilikuwa hivi "Mfumo wa elimu ya Msingi unasababisha watu wengi, hasa walio maskini, ambao hawawezi kupeleka watoto wao private, waingie katika ununuzi wa majina." Ndio maana nikashauri kuwa mfumo huu ubadilishwe, na wanafunzi wafelipo wapewe nafasi ya kukariri madarasa na kurudia mitihani, kwa majina yao halisi, kama inavyokuwa katika mitihani ya kidato cha pili, QT, kidato cha nne na kidato cha sita.

Mfumo huu ukibadilishwa hakuna atakayenunua jina tena. Kama mfumo huo ungekuwepo, hata wewe usingenunua jina kwa mara ya kwanza, ila ungerudia mtihani wa darasa la saba kwa jina lako la kuzaliwa.

Unaposema
Tusione dhambi kutumia chances chache zinazopatikana ktk kujiendeleza,bali tuone dhambi kuachezea chances adimu tunazopata
ina maana basi tufanye uhalifu eti kwa sababu hizo ndizo chance chache tuzipatazo?

Maelezo yako mengi ni sahihi, na yana hoja za msingi, kamanda
 
Wanadamu hutumia njia tofauti maishani kufikia malengo. Mara nyingi njia zinazotumika kufikia malengo haya zinatofautiana sana kulingana na maeneo au matabaka ya kiuchumi.
Mfano: watu wengi waliosoma vijijini shule za msingi, walirudia mara nyingi ili waweze KUCHAGULIWA. Na kurudia huku hutumia majina ya wale walioacha shule moja kwa moja. Ninafahamu mtu aliyerudia primary school mara nne, kila mwaka akitumia majina tofauti.
*Kurudia shule ni njia ya kutafuta opportunity
*UK wanaita kujilipua - ambapo mtu hubadili majina, mwaka wa kuzaliwa na uraia ili aweze kupata ukaazi.
*Tanzania tunachohitaji ni kujua tofauti kati ya kutumia jina BANDIA au mwenye IDENTITY zaidi ya moja.
*Tutafute wenye vyeti vya kufoji na wale wenye degree feki (Sio suala la majina)
*Tutafute wenye nafasi ambazo hawastahili


Vinginevyo hii hoja itatutoa kwenye lengo kuu la kupigana na ufisadi wa elimu


Uliyoyasema ni sahihi. Tuna haja ya kutafuta wene degree feki. Hata hivyo, hoja yangu inaendelea kuwa na msingi kuwa endapo mfumo wa elimu ya msingi utabadilishwa, na kuwapa waliofeli darasa la saba fursa ya kurudia mtihani kwa majina yao halisi, suala la ununuzi wa majina lingefutika kabisa. Kuna haja ya serikali kuliangalia suala hili, maana kama serikali haina alternative kwa ajili ya wanaofeli darasa la saba, basi ina maana kuwa inatangaza kuwa huo ndio mwisho wao kielimu. Serikali ikitoa fursa ya kukariri darasa kwa wale waliofeli, kutapunguza ununuzi huu wa majina
 
Uliyoyasema ni sahihi. Tuna haja ya kutafuta wene degree feki. Hata hivyo, hoja yangu inaendelea kuwa na msingi kuwa endapo mfumo wa elimu ya msingi utabadilishwa, na kuwapa waliofeli darasa la saba fursa ya kurudia mtihani kwa majina yao halisi, suala la ununuzi wa majina lingefutika kabisa. Kuna haja ya serikali kuliangalia suala hili, maana kama serikali haina alternative kwa ajili ya wanaofeli darasa la saba, basi ina maana kuwa inatangaza kuwa huo ndio mwisho wao kielimu. Serikali ikitoa fursa ya kukariri darasa kwa wale waliofeli, kutapunguza ununuzi huu wa majina
ukishawapata watakusaidia nini???? kukariri la saba haimaanishi unanunua cheti kwa sababu unafanya mtihani kwa akili yaako,,,, njaa zenu tu zinawafanya mkae chini na kujadili yasiyowahusu kama umekosa fursa jipange haya mengine hayakusaidii bwana mdogo wacha domo tafuta ya kwako
 
ukishawapata watakusaidia nini???? kukariri la saba haimaanishi unanunua cheti kwa sababu unafanya mtihani kwa akili yaako,,,, njaa zenu tu zinawafanya mkae chini na kujadili yasiyowahusu kama umekosa fursa jipange haya mengine hayakusaidii bwana mdogo wacha domo tafuta ya kwako


Nadhani hujanielewa kamanda. Anayways, tuko pamoja
 
Back
Top Bottom