Viongozi wetu hawataki wahalifu watetewe na mawakili, je ni utawala wa sheria?

Viongozi wetu hawataki wahalifu watetewe na mawakili, je ni utawala wa sheria?

Euphransia

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2017
Posts
937
Reaction score
778
Nimekuwa nafuatilia masuala ya sheria hapa nchini. Nimewahi kusikia kiongozi mmoja akisema kuwa hategemei kusikia mawakili watawatetea watuhumiwa wa madawa ya kulevya.

Leo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Bw.Paulo Makonda wakati akiongea na wanasheria wa kujitolea aliwashukuru sana kusema kuwa Serikali hii inataka kutetea wanyonge na hatarajia wahalifu watatetewa.

Najiuliza utetezi huwa wa upande mmoja? Mbona serikali hii katika kesi za mauaji inatoa mawakili hata upande wa muuaji? Wakati muuaji katenda kosa la kutoa uhai wa mtu? Nadhani viongozi wetu kutetea mharifu lipo kisheria tusilete siasa kwenye haki ya mtu.
 
Mkuu,usipumbazwe na hizo porojo...wanasiasa ni kawaida yao kubwabwaja!
 
Mkuu,usipumbazwe na hizo porojo...wanasiasa ni kawaida yao kubwabwaja!
 
Hata mimi nashangaa sana kwani kumkamata mtu ndiyo imethibitika kuwa katenda kosa, so ina maana mahakama ibague makosa, only in Tanzania,,,,,,,,,,,,,,,
 
Mawakili wa serikali ni dhaifu, we tazama jinsi LISSU anavyocheza na akili zao. Anacheza nazo kama apendavyo yeye.
 
Hakuna mwanasiasa atakayeuona ufalme wa mumgu ingawa mashehe na maasofu watawaombea sana. A government is an instrument of oppression...... Sasa how do you enter the kingdom of god while you chair the council of oppression!
 
Umekosea heading! Ya nini kumtetea muharifu? Labda km mtuhumiwa.
 
Back
Top Bottom