Vipaumbele vya tanzania na kamati ya rais

KALEBE

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2011
Posts
773
Reaction score
339
Ndugu wana jamvi taarifa zilizopo kwa sasa ni kuwa raiskuna baadhi ya watu wamejifungi mahali wakijadili vipaumbele sita ambavyo rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania aliviainisha ambavyo miongoni mwake ni kilimo, nishati, elimu na n.k
Hivyo basi hawa watu wanafanya upembuzi yakinifu ya nini kifanyike ili taifa liweze kusogea kutoka hapo lilipo kwa maana ya kuwa kufikia mwaka 2025 tuwe tumeweza kufikia malengo ya tanzania vision
Kwangu mimi naliona ya kuwa ni jambo jema kwani hata nchi za asia kwa mfano malysia, singapore, phillipes waliweza kutambua vipaumbele ambavyo ndivyo walivyoanza navyo hadi kuwafikisha hapo walipo hii leo
Swali langu ambalohadi leo najiuliza kwa huyu rais wetu ni kuwa kwa kipindi chote hicho ambacho alikuwa madarakani kipaumbele au vipaumbele vyake ilikuwa ni nini kwa sababu kama hii leo ndo tunaambiwa ya kuwa rais ameainisha vipaumbele ambavyo vinatakiwa kufanyiwa kazi wakati umebakia mwaka mmoja wa uongozi wake maana yake ni kuwa hakuwa na vipaumbele au kipaumbele chochote katika uongozi wake wote wa miaka tisa aliyokaa madarakani
Lakini pia hawa watu waliochukuliwa kwa lengo la kwenda kufanya upembuzi yakinifu ni vigezo gani v ilivyotumika kuwapata watu hawa?
Kazi hii itafanyika kwa muda wa wiki sita

source: mimi mwenyewe
 

mkuu, kwanza kabisa napenda kukupongeza kwa kutuletea mada hiyo nzuri. ni imani yangu kuwa dhamira yako ilikuwa kutufahamisha watanzania ili tujue jitihada za serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi.

hata hivyo, kuna mashaka na uwasilishaji wako. kwanza kabisa umesema kuwa kwa nini rais ajikite katika kazi hiyo wakati muda wake uliobaki ni mwaka mmoja tu? kwanza napenda ufahamu kuwa hivyo si vipaumbele vya rais, ni vipaumbele vya taifa ili hata kama rais aliyepo ataondoka, anayekuja anaongoza kwa mujibu wa hivyo vipaumbele hivyo. nchi zote duniani zinatumia mfumo huo. sisi tujilaumu kwa kuchelewa kuutumia. ndiyo maana kila rais alikuwa na mikakati yake na hivyo taifa kupoteza mwelekeo. unajua, unaweza kuongoza miaka 8 au tisa isiwe na maana kubwa kwa taifa, lakini mwaka mmoja tu ukafanya mambo ambayo yana manufaa kwa taifa kwa miaka 100 ijayo. kwa upande wangu, rais aliyepo, JAKAYA KIKWETE namuona kama ni shujaa wa taifa hili. karuhusu mchakato wa katiba mpya wakati waliomtangulia walikuwa wanaweka viraka tu, karuhusu hoja za muungano kujadiliwa waziwazi, kaweka mfumo mzuri wa uchaguzi ndani ya ccm, karuhusu taarifa za mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali kujadiliwa waziwazi bungeni na mambo mengi kadhaa. hayo niliyokutajia ni mafanikio ya kimfumo na kimkakati.

kuhusu watu walioteuliwa kufanya kazi hiyo, ninaamini kuwa ni watu makini ingawa hujataja majina yao ili tuwajurge kama wanafit kwenye kazi hiyo. kwani kwa uhalisia wa kazi hiyo, sitegemei watu mbumbu wenye division 0 form four au wamepata A 9 form four lakini hawajaenda chuo, wakafanya kazi hiyo. pia jinsi unaonekana kama wewe ni miongoni mwa watu waliokuwa wanaisubiri kwa hamu kazi hiyo. sasa baada ya kuona umeikosa unaanza kueleza mapungufu ya jk. huo ni unafiki na tukifanya hivyo hatuwezi kuendelea. tuwaamini walioteuliwa kuwa wataifanya kazi hiyo kwa ufanisi.
 
hawana lolote hao na huyo rais wao.yaani kila siku mipango tu utekelezaji unaishia mifukoni.wazee wa vipaumbele na mipango isiyotelekezeka.wanafaidisha wezi wenzao na matumbo yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…