Vipi vitambulisho vya machinga havina muendelezo? Basi walipe ushuru kwa halmashauri

Vipi vitambulisho vya machinga havina muendelezo? Basi walipe ushuru kwa halmashauri

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Wakuu habari,

Kama mnavyojua Rais Magufuli alileta kitu kilichoitwa Vitambulisho vya Machinga mwaka 2019

Vitambulisho hivi ambavyo vililipiwa 20,000 vilipelekea ushuru ambao machinga walikuwa wakilipa kwa Halmashauri kufutwa, na badala yake wangelipa hiyo 20k kila mwaka.

Sasa ni miaka 3 imepita na hivyo vitambulisho havijawahi kulipiwa tena, wala havifuatiliwi tena.

Kama halikuwa wazo zuri basi Serikali iendelee na utaratibu wa zamani wa machinga kulipia ushuru kwa halmashauri, maana wanafanya biashara bure huku serikali ikikosa fedha na kuweka kodi kubwa zinazoumiza wachache.
 
Nenda playstore, download "Machinga App" unaweza kumsajiri machinga wako popote ulipo na Kadi ataipata baada ya muda
 
Zanzibar wameviboresha.

Hapa bara Wanaonekana kero.

Hawa watu sijui wamezaliwa familia za aina gani.

Hawana ubinadamu kabisa.

They are ruthless and heartless.
 
Wakuu habari,

Kama mnavyojua Rais Magufuli alileta kitu kilichoitwa Vitambulisho vya Machinga mwaka 2019

Vitambulisho hivi ambavyo vililipiwa 20,000 vilipelekea ushuru ambao machinga walikuwa wakilipa kwa Halmashauri kufutwa, na badala yake wangelipa hiyo 20k kila mwaka.

Sasa ni miaka 3 imepita na hivyo vitambulisho havijawahi kulipiwa tena, wala havifuatiliwi tena.

Kama halikuwa wazo zuri basi Serikali iendelee na utaratibu wa zamani wa machinga kulipia ushuru kwa halmashauri, maana wanafanya biashara bure huku serikali ikikosa fedha na kuweka kodi kubwa zinazoumiza wachache.
Wamepangwa Ili walipe ushuru,hakuna cha bure
 
Zanzibar wameviboresha.

Hapa bara Wanaonekana kero.

Hawa watu sijui wamezaliwa familia za aina gani.

Hawana ubinadamu kabisa.

They are ruthless and heartless.
Wameweka maboresho gani?
 
Kama lingekuwa wazo zuri wangeanza kwa kuweka sheria inayowalinda machinga na kuvitambua vitambulisho vyao......ile ilikuwa tu ni sarakasi za kukusanya hela na kujipatia mtaji wa kisiasa
 
Kama lingekuwa wazo zuri wangeanza kwa kuweka sheria inayowalinda machinga na kuvitambua vitambulisho vyao......ile ilikuwa tu ni sarakasi za kukusanya hela na kujipatia mtaji wa kisiasa
Matamko ndiyo yanawaendesha duu, na majina ya kubatizwa majukwaani.

Leo WANYONGE. Kesho wapiga kura wetu. Mtondogoo wachafuzi mazingira!
Wanatumika Sana. Ni mtaji WA kisiasa!
Viongozi wao mapandikizi! Wangekuwa smart wangepigania sheria ya kuwalinda wao! Kama ambavyo umenena!
 
Back
Top Bottom