Visa na mikasa: Ujinga wa Mwafrika

Visa na mikasa: Ujinga wa Mwafrika

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Kitabu hiki kinapatikana BURE ndani ya app ya Maktaba Sauti. Ipo playstore.

Somo la kwanza

Kisa cha Vimbwenelehi



Nilipokuwa bado mdogo nilipata kusikia habari za vijitu vya kutisha, vyenye matata sana, vinaitwa Vimbwenelehi. Kimo chao shubiri mbili, akisimama atakufikia gotini. Mimi sikuwahi kuona Kimbwenelehi wakati huo, lakini wanasema ni vijitu vyenye kupenda sana kusifiwa, na usipokisifia utaona cha mtema kuni. Ukikutana nacho kitakuuliza, "Umbwenelehi?" Maana yake, kwa lugha nyingi za kibantu, "Umenionea wapi?"

Haja ni kujitahidi kuthibitisha kwamba yeye siyo mfupi, na kwamba hata watu wengine wanaweza kumwona toka akiwa Imbali. Matarajio yake ni kwamba utamwambia, "Nimekuona mbali sana: tangu kulee-eee!" Hapo utakuwa rafiki wa Kimbwenelehi. Lakini ukisema kwamba umemwona pale pale karibu, hata kama si kwa sababu ya ufupi, basi Kimbwenelehi kitakuandama, utapigwa ngumi mpaka uzimie!

Basi zikavumishwa sana sifa hizo za Vimbwenelehi. Ikasemwa kwamba vinaweza kukufurusha ngumi, au kukupiga rungu. Havipigiki hivyo, Vimbwenelehi, kimo chao shubiri mbili! Hivi majuzi nilikuwa nikiwaza. Vipi vijitu hivi, urefu shubiri mbili, vitakavyoweza kuwapiga majitu ngumi hadi wakazimia; ngumi yenyewe itatoka wapi hasa?

Kumbe yote haya yalitokana na hofu ya kijinga. Hofu ile ile ya vibwengo, ya maruhani, ikaingia kwa Vimbwenelehi. Mtu kaona vijitu vya ajabu, akaanza kuviabudu. Kumbe kaona mbilikimo, binadamu kama sisi, isipokuwa mfupi sana tu. Kudai kujitukuza ndio mwenendo wao. Wanajitambua kuwa wafupi, kwa hiyo wanatamani kujikweza-kweza kidogo. Lakini ndio tuwaogope, tuwasifie sana, kwamba wanaweza kutufurusha kwa ngumi, au kwa magongo? Hivyo hiyo ndio sababu kuhofu kumwambia kweli, kama kweli inapaswa kusema. Tunampaka asali Kimbwenelehi, na kumwambia maneno ya kumpendeza wakati wote, tunaogopa asitupige gongo? Hiyo ni hofu au upumbavu?

Basi wako hata leo wananchi wanaowaogopa sana Vimbwenelehi. Wako Vimbwenelehi wa akili, wenye mawazo mafupi sana. Kwa bahati kapata cheo. Basi nao hawa hutamani sana kutukuzwa, kuvikwa vilemba vya ukoka; hawataki kuelekezwa wakikosa. Watu hawa matata sana, na kweli wanaweza sana kuchachamaa. Lakini shida yao kubwa ni umbwenelehi tu.

Sasa la ajabu ni kwamba na sisi wengine tunawaogopa. Mtu anaona dhahiri jambo linapotoka. Anaogopa kusema, maana Kimbwenelehi kikali, kitampiga ngumi! Wajibu wa mwana-TANU ni kusema kweli daima, bila ya chuki, wala kinyongo. Huenda wazo lako likamsaidia mtu, akajitambua kwamba yeye ni Kimbwenelehi.

Na kwa vyo vyote vile, hata kama Kimbwenelehi kweli akikupiga ngumi, ngumi hiyo itafika wapi mbele ya TANU?
 
Somo la pili

Uchu wa Mzee Mikidadi

*******

Nilipomaliza darasa la sita, nilichaguliwa kuingia la saba katika shule ya boda, mbali sana na kwetu. Kufika kule nikafanya urafiki na kijana mwenzangu Juma Mikidadi, yeye kwao karibu na pale pale shule. Juma akawa rafiki yangu sana. Basi zikafika siku za pasaka, ambapo watoto watokao jirani huruhusiwa kwenda kwao. Juma hakutaka kwenda kwao peke yake, akaniomba twende wote. Tukaomba ruhusa kwa Mkuu wa Shule, tukaenda kwao kwa mapumziko ya siku mbili.

Mzee Mikidadi si mtu mdogo, tulipofika akatushughulikia sana. Haukupita muda tukaona kuku anakamatwa, kapewa Juma kumchinja. Tukaona kwamba leo uhondo. Saa za kula zikafika, watoto wote tukakusanyika. Likatandikwa jamvi kubwa sana sote tukaenea. Likaletwa sinia la wali, na bakuli la nyama ya kuku; nyama zimejaa tele. Mimi mgeni natazama wenzangu wanavyofanya. Watoto wote wametulia kimya; wanamngoja Mzee Mikidadi.

Mara Mzee Mikidadi kafika. Kashika bakuli anatia mchuzi katika sinia la wali. "Kuleni wanangu, sikukuu yenu hii". Mzee Mikidadi filikichi kinywani, na bakuli kalisogeza miguuni pake. Basi sisi tunaendelea kula wali kwa mchuzi. Tumekula mpaka tunakaribia kushiba; lakini wali kwa mchuzi tu, nyama hatujapewa bado. Lakini Mzee Mikidadi akimaliza matonge mawili anaingilia paja, ama shingo, ama nyama zingine tamu tamu za kuku. Na kutuhimiza haachi, "Kuleni wanangu, sikukuu yenu hii."

Mwisho kabisa vikabakia vibawa, na miguu, na vipapatio. Mzee Mikidadi anaanza kutunyofolea kila mtu kidogo-kidogo, afutike mkono wa kushoto. Hatuna ruhusa kula kinyama hicho mpaka sinia la wali limemalizika. Mzee Mikidadi sasa ameshiba, ananawa na kuondoka. Na sisi tukalimaliza sinia la wali tupate kunyofoa vinyama vyetu.

Ni jambo zuri sana kusisitiza heshima ya watoto wakati wa kula. Haifai watoto wazoee kula ovyo bila ya utaratibu, kama watoto wa kitwana. Lakini haifai vile vile taratibu hizo za kula ziwanyime waoto aina za chakula zinazohitajiwa sana katika kujenga mwili wao. Watoto wanakonda, nywele zinageuka rangi, maradhi hayawaishi, si kwa sababu tu hawapati chakula kilicho bora. Ukiwaangalia watoto namna hiyo matumbo yao yametuna kwa ajili ya kushiba; ila chakula chenyewe hakina faida nyingi mwilini. Nyama na vyakula vingine vyenye mwili watoto hawavipati, hata kama sikukuu hii yao.

Kwetu mtoto hali filikichi ya kuku; eti mwiko. Na kumbe filikichi ina thamani kubwa sana ya chakula cha kujenga mwili. Anakula Mzee Mikidadi, mifupa yake isha komaa, haina haja ya kukua tena!

Watoto wetu ndio watakaoijenga Jamhuri hii; Tanzania hii ni yao wao. Tusiwanyime chakula bora kwa visingizio vya kufunza adabu, au vya mila zinazomfanya Mzee Mikidadi ale nyama yote, na watoto waambulie mchuzi. Kama sikukuu hii ni yao, basi lazima tuwaachie wafaidi, na wapate faida ya chakula katika kujenga miili yao.
 
Niliwahi soma shule ya msingi Boarding school flani hivi, kulikuwaga na vimbwanga vya vimbweneleh, Kama mleta mada unavyosema!! Aisee ni balaa! Lakn vilikuwa vinatishia tuu watu!!

NB: sijwah kukutana navyo lakn, naishia kusikia kwa wenzangu tu
 
Somo la pili

Uchu wa Mzee Mikidadi

*******

Nilipomaliza darasa la sita, nilichaguliwa kuingia la saba katika shule ya boda, mbali sana na kwetu. Kufika kule nikafanya urafiki na kijana mwenzangu Juma Mikidadi, yeye kwao karibu na pale pale shule. Juma akawa rafiki yangu sana. Basi zikafika siku za pasaka, ambapo watoto watokao jirani huruhusiwa kwenda kwao. Juma hakutaka kwenda kwao peke yake, akaniomba twende wote. Tukaomba ruhusa kwa Mkuu wa Shule, tukaenda kwao kwa mapumziko ya siku mbili.

Mzee Mikidadi si mtu mdogo, tulipofika akatushughulikia sana. Haukupita muda tukaona kuku anakamatwa, kapewa Juma kumchinja. Tukaona kwamba leo uhondo. Saa za kula zikafika, watoto wote tukakusanyika. Likatandikwa jamvi kubwa sana sote tukaenea. Likaletwa sinia la wali, na bakuli la nyama ya kuku; nyama zimejaa tele. Mimi mgeni natazama wenzangu wanavyofanya. Watoto wote wametulia kimya; wanamngoja Mzee Mikidadi.

Mara Mzee Mikidadi kafika. Kashika bakuli anatia mchuzi katika sinia la wali. "Kuleni wanangu, sikukuu yenu hii". Mzee Mikidadi filikichi kinywani, na bakuli kalisogeza miguuni pake. Basi sisi tunaendelea kula wali kwa mchuzi. Tumekula mpaka tunakaribia kushiba; lakini wali kwa mchuzi tu, nyama hatujapewa bado. Lakini Mzee Mikidadi akimaliza matonge mawili anaingilia paja, ama shingo, ama nyama zingine tamu tamu za kuku. Na kutuhimiza haachi, "Kuleni wanangu, sikukuu yenu hii."

Mwisho kabisa vikabakia vibawa, na miguu, na vipapatio. Mzee Mikidadi anaanza kutunyofolea kila mtu kidogo-kidogo, afutike mkono wa kushoto. Hatuna ruhusa kula kinyama hicho mpaka sinia la wali limemalizika. Mzee Mikidadi sasa ameshiba, ananawa na kuondoka. Na sisi tukalimaliza sinia la wali tupate kunyofoa vinyama vyetu.

Ni jambo zuri sana kusisitiza heshima ya watoto wakati wa kula. Haifai watoto wazoee kula ovyo bila ya utaratibu, kama watoto wa kitwana. Lakini haifai vile vile taratibu hizo za kula ziwanyime waoto aina za chakula zinazohitajiwa sana katika kujenga mwili wao. Watoto wanakonda, nywele zinageuka rangi, maradhi hayawaishi, si kwa sababu tu hawapati chakula kilicho bora. Ukiwaangalia watoto namna hiyo matumbo yao yametuna kwa ajili ya kushiba; ila chakula chenyewe hakina faida nyingi mwilini. Nyama na vyakula vingine vyenye mwili watoto hawavipati, hata kama sikukuu hii yao.

Kwetu mtoto hali filikichi ya kuku; eti mwiko. Na kumbe filikichi ina thamani kubwa sana ya chakula cha kujenga mwili. Anakula Mzee Mikidadi, mifupa yake isha komaa, haina haja ya kukua tena!

Watoto wetu ndio watakaoijenga Jamhuri hii; Tanzania hii ni yao wao. Tusiwanyime chakula bora kwa visingizio vya kufunza adabu, au vya mila zinazomfanya Mzee Mikidadi ale nyama yote, na watoto waambulie mchuzi. Kama sikukuu hii ni yao, basi lazima tuwaachie wafaidi, na wapate faida ya chakula katika kujenga miili yao.
Wazee wengi baadhi Yao wa zamani, walikuwa na tabia ya kujipakulia minyama tuu na uchoyo!!

Utakuta baba ndo anapendelewa minyama kibao, huku watoto wanalishwa vinyama tuwili tuwili,

Huyo anaekula sana hajengi mwili bali anakuza kitmbi tu
 
Wazee wengi baadhi Yao wa zamani, walikuwa na tabia ya kujipakulia minyama tuu na uchoyo!!

Utakuta baba ndo anapendelewa minyama kibao, huku watoto wanalishwa vinyama tuwili tuwili,

Huyo anaekula sana hajengi mwili bali anakuza kitmbi tu
Ni hatari sana. Yaani watoto wanaotakiwa kujenga mwili kwa protini hawapewi nyama za kutosha ila mtu mzima ambaye hazihitaji ndiyo anazifakamia balaa na kuishia kuwa na kitambi. Wengine hata leo hii. Halafu kisayansi mtu ambaye utotoni hakuwa anapata protini za kutosha, akiwa mtu mzima na kuanza kufakamia manyama ana hatari kubwa ya kupata obesity na baadaye kisukari na mapresha. Mwili wake unakuwa haujazoea kuchakata manyama.
 
Hio nimeiona sana!!

Nimewahi kuulizwa kwann inakuwa hivyo
"Wanasema kisa yeye ndo mtafutaji, ati wanampa motisha azid tafuta"

Non sense
 
Back
Top Bottom