Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,509
- 3,756
Jana, Mei 15, 2020 Uganda imetangaza visa vipya 43 vya #COVID19 vimeongezeka na vyote vikiwa ni vya Madereva wa Malori na kufanya jumla ya visa kufikia 203
Wizara imesema jumla ya sampuli 2,558 zimepimwa kati ya hizo; 1,838 ni za Madereva wa malori na 720 ni za Wakazi wa Uganda ambapo zote 720 zimeonekana hazina maambukizi
Katika visa hivyo 43, Waganda ni 15, 9 ni Wakenya na 4 ni raia wa Eritrea ambao hao wamegundulika katika mpaka wa Elegu. Wengine waliogundulika katika mpaka wa Mutukula ni Watanzania 5 na Mrundi mmoja
Aidha, kuna wengine waliogundulika katika mpaka wa Malaba ambapo 5 ni Wakenya, Waganda 2, Mrundi 1 na dereva mwingine 1 ambaye uraia wake haujajulikana
Lakini pia, Jumla ya Wagonjwa 63 wamepona nchini humo tangu kuzuka kwa janga hilo
Wizara imesema jumla ya sampuli 2,558 zimepimwa kati ya hizo; 1,838 ni za Madereva wa malori na 720 ni za Wakazi wa Uganda ambapo zote 720 zimeonekana hazina maambukizi
Katika visa hivyo 43, Waganda ni 15, 9 ni Wakenya na 4 ni raia wa Eritrea ambao hao wamegundulika katika mpaka wa Elegu. Wengine waliogundulika katika mpaka wa Mutukula ni Watanzania 5 na Mrundi mmoja
Aidha, kuna wengine waliogundulika katika mpaka wa Malaba ambapo 5 ni Wakenya, Waganda 2, Mrundi 1 na dereva mwingine 1 ambaye uraia wake haujajulikana
Lakini pia, Jumla ya Wagonjwa 63 wamepona nchini humo tangu kuzuka kwa janga hilo