Visiwani wataka pasu kwa pasu vinginevyo muungano uvunjwe

Visiwani wataka pasu kwa pasu vinginevyo muungano uvunjwe

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925
Mbunge wa Jimbo la Micheweni, Bw. Haji Khatibu Kai (CUF) alipendekeza kuwa kuvunjwa kwa muungano kwa kuwa hakuna uwiano katika mambo mbalimbali yanayofanywa na serikali. Alisema kuwa serikali haikueleza ni kero ngapi mpaka sasa zimeshughulikiwa hatua inayowafanya Wanzanzibari kuwa nyuma ikilinganishwa na wabara, hivyo akaomba kuwa kama Zanzibar imeonekana ni mzigo, basi muungano huo uvunjwe ili uundwe upya.

Naye Mbunge wa Magogoni, Bw. Kombo Khamis Kombo (CUF) alisema kuwa kumekuwa na uwiano usiokuwa sahihi katika mambo mbalimbali ambapo alitolea mfano uteuzi wa mabalozi katika nchi mbalimbali. Alisema kuwa mpaka sasa mabalozi wanaotoka Zanzibar ni wanne tu ambao wako katika nchi za Kiarabu huku idadi kubwa ya mabalozi wakitoka bara hivyo akaomba kuwepo uwiano katika teuzi mbalimbali.

Alisema kuwa serikali ina wizara 26, kati ya hizo sita tu ndizo za muungano, lakini mambo mbalimbali ambayo si ya muungano yamekuwa yakitengewa fedha hivyo akahoji usawa katika masuala hayo .Alisema kuwa kama kuna nia ya dhati ya kutatua kero za muungano ni vyema Waziri Mkuu akalisimamia vyema suala hilo ili kurejesha imani ya Wazanzibari.

Majira
 
Kwanza tuwaulize hao wabunge wanaotishia nyau eti Muungano uvunje, hayo ndio wananchi wao waliyowatuma au ni mawazo yao wanatafuta vyeo serikalini?
Warudi majimboni wakawaulize wananchi na ikionekana Wzanzibari hawautaki, basi tuwaachie waondoke! Sina hakika kama watu wa kawaida wana mawazo haya haya?
 
Wazenj wanaupenda sana Muungano, hiyo ya kutishiana nyau ni "sitaki nataka!" Kama huyo Mbunge kweli haupendi Muungano awe wa kwanza kujitoa kwenye Bunge la Muungano, nitaona kweli yuko serious!
 
yaani huyo mbunge alichoona cha maana sana ni uteuzi wa mabalozi, yaani hakuna kingine kabisa kinachohusu muungano ambacho wangekishughulikia kingeleta tija kwa wanzazibari wote.
 
Kwanza tuwaulize hao wabunge wanaotishia nyau eti Muungano uvunje, hayo ndio wananchi wao waliyowatuma au ni mawazo yao wanatafuta vyeo serikalini?
Warudi majimboni wakawaulize wananchi na ikionekana Wzanzibari hawautaki, basi tuwaachie waondoke! Sina hakika kama watu wa kawaida wana mawazo haya haya?

Huyo mbunge kilichomfikisha hapo bungeni hakijui? Bila Muungano angekuwa bungeni Dodoma? Anataka nini sasa?
 
yaani huyo mbunge alichoona cha maana sana ni uteuzi wa mabalozi, yaani hakuna kingine kabisa kinachohusu muungano ambacho wangekishughulikia kingeleta tija kwa wanzazibari wote.

Wabara tungeshika wizara za wazanzibar wangetutafutia majambia, angalia wafanyabiashara wa bara na makanisa ya wakristo yanavyochomwa moto huko Zenj
 
Mbunge wa Jimbo la Micheweni, Bw. Haji Khatibu Kai (CUF) alipendekeza kuwa kuvunjwa kwa muungano kwa kuwa hakuna uwiano katika mambo mbalimbali yanayofanywa na serikali. Alisema kuwa serikali haikueleza ni kero ngapi mpaka sasa zimeshughulikiwa hatua inayowafanya Wanzanzibari kuwa nyuma ikilinganishwa na wabara, hivyo akaomba kuwa kama Zanzibar imeonekana ni mzigo, basi muungano huo uvunjwe ili uundwe upya.

Naye Mbunge wa Magogoni, Bw. Kombo Khamis Kombo (CUF) alisema kuwa kumekuwa na uwiano usiokuwa sahihi katika mambo mbalimbali ambapo alitolea mfano uteuzi wa mabalozi katika nchi mbalimbali. Alisema kuwa mpaka sasa mabalozi wanaotoka Zanzibar ni wanne tu ambao wako katika nchi za Kiarabu huku idadi kubwa ya mabalozi wakitoka bara hivyo akaomba kuwepo uwiano katika teuzi mbalimbali.

Alisema kuwa serikali ina wizara 26, kati ya hizo sita tu ndizo za muungano, lakini mambo mbalimbali ambayo si ya muungano yamekuwa yakitengewa fedha hivyo akahoji usawa katika masuala hayo .Alisema kuwa kama kuna nia ya dhati ya kutatua kero za muungano ni vyema Waziri Mkuu akalisimamia vyema suala hilo ili kurejesha imani ya Wazanzibari.

Majira

Nyerere angekuwa hai hawa waheshimiwa wangekuwa kifungo cha nyumbani indefinately. Nyie wana JF wenye umri chini ya miaka 25 kuna anayemfahamu au kuwahi kumsikia Abood Jumbe?
 
bora muungano uvunjike idadi ya maisilamu ipungue
ungekuwa unajua lengo la muungano ni nn usingelopoka.. muungano ulitengenezwa na nyinyi wakristo kuupitia chama chenu cha magamba kuubana uislaam. kama si hivyo si muuvunje?? kwa nn mwaunganganiaaa? na enyi wenu waislaam mnaotetea muungano kwa kupewa pesa na tuvyeo siku zenu zahesabika.
 
Nyerere angekuwa hai hawa waheshimiwa wangekuwa kifungo cha nyumbani indefinately. Nyie wana JF wenye umri chini ya miaka 25 kuna anayemfahamu au kuwahi kumsikia Abood Jumbe?
Mbona kwenye hotuba yake alidai kuwa kuna watu wanafikiri kujitenga "kwa sababu ya ulevi wa madaraka!" Je, hao watu aliwaweka ndani? Vitu vingine unaropoka tu ndugu!
 
ungekuwa unajua lengo la muungano ni nn usingelopoka.. muungano ulitengenezwa na nyinyi wakristo kuupitia chama chenu cha magamba kuubana uislaam. kama si hivyo si muuvunje?? kwa nn mwaunganganiaaa? na enyi wenu waislaam mnaotetea muungano kwa kupewa pesa na tuvyeo siku zenu zahesabika.
Haaaa haaa! Kumbe kulikuwa na vikao vya Wachungaji na maaakofu juu ya kuunda Muungano? Ama kweli kichwa chako kimejaa tope! Pole sana, hebu kakojoe kwanza ili ukalale!
 
Hawa watu kwann wasipewe tu nchi yao?....kama hawataki kuwapa baci wawatangaze hawa ni wahaini
 
Huyo mbunge kilichomfikisha hapo bungeni hakijui? Bila Muungano angekuwa bungeni Dodoma? Anataka nini sasa?
kafika dodoma kwa sababu ya hila zenu, fika zenj fanya karesearch kadogo ndo utajua kama mungano unatakiwa au la. zanzibar bila tanganyika ni dubai.. na hilo mwalijua tatizo roho mbaya dhidi ya uislaam. kama vipi si uvunjike kwa nn mwaunganganiaaaaaa
 
Mi napendekeza kura za maon ipigwe na tujue km wananchi wanataka kuuvunja muungano.Tusipige soga majukwaani bali wananchi washirikishwe.binafsi nataka uvunjwe maana ni batili coz wananchi hawakushirikishwa na sioni umuhimu wake zaidi ya kero
 
yaani huyo mbunge alichoona cha maana sana ni uteuzi wa mabalozi, yaani hakuna kingine kabisa kinachohusu muungano ambacho wangekishughulikia kingeleta tija kwa wanzazibari wote.
hilo ni moja ktk mengi tatizo muda ni mdogo wanaopewa haiwezekani kusema yote. kwa hilo we unaona sawa?
 
Hawa watu kwann wasipewe tu nchi yao?....kama hawataki kuwapa baci wawatangaze hawa ni wahaini
Mbona mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 yanaitaja Zanzibar kuwa ni nchi? Na kama hawataki Muungano kwa nini wanafanya kazi za kuajiriwa kwenye Wizara na Idara zisizo za Muungano? Je, Bungeni huwa wanatoka nje ya Bunge kunapokuwa na mjadala wa Wizara isiyo ya Muungano? Au Wazanzibari wanapodai kwamba "hatutaki Muungano" huwa wanamaanisha nini hasa?
 
Haaaa haaa! Kumbe kulikuwa na vikao vya Wachungaji na maaakofu juu ya kuunda Muungano? Ama kweli kichwa chako kimejaa tope! Pole sana, hebu kakojoe kwanza ili ukalale!
kakojoe ww kwanza kwa chuki zako juu ya uislam, hata hivyo ndugu zako waislam twakupenda sana.. hatuna chuki na nyie msietupendag
 
bora muungano uvunjike idadi ya maisilamu ipungue
Chuki yako dhidi ya waislam haitakufikisha popote.jenga hoja,changia mada uwe great thinker.usiandike utumbo.nakuonea huruma kwani hujui uislam ni nini na unahusu nini.nakupa homework kausome uislam usiongozwe na jazba .
 
Muungano!!
Uvunjwe tu hata leo hii.
Wazanzibar wanaamini huu muungano ndio kikwazo cha mafanikio yao.
 
Back
Top Bottom