Vita ya Congo DRC na M23 nini kifanyike haraka kuokoa maisha ya watu wasio na hatia na kuiweka Congo salama maisha yake yote

Vita ya Congo DRC na M23 nini kifanyike haraka kuokoa maisha ya watu wasio na hatia na kuiweka Congo salama maisha yake yote

Loading failed

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2023
Posts
2,603
Reaction score
7,501
Ndugu zangu...

Tumekua tukishuhudia, kuona na kusikia huko Congo DRC kukiwa na vita kali kati ya M23 na majeshi matiifu ya serikali, halikadhalika M23 wakinukuliwa kuwa na silaha nzito kuliko majeshi ya serikali , kuwashinda nguvu na kuwafurusha vikali pamoja na kuua wanajeshi wa Congo , pia kunyakua miji kirahisi sana huku wakisababisha mtafaruku wa ukosefu wa amani pamoja na vifo baina ya raia wasiokua na hatia miaka na miaka.

Maswali;

1: Kama kweli vile vikosi vya kulinda amani vipo pale kulinda amani ni kwanini hawapigani na maadui moja kwa moja pindi wanapo hatarisha amani ya watu wa congo, ni kwanini basi wasiingie vitani rasmi kupambana na M23 moja kwa moja?

2: Kwanini vile vikosi vyote vya kimataifa visiondolewe alafu congo iundwe upya na wajitangazie uhuru wao mpya tofauti na wa hawali kutokana na M23 kuendelea kusumbua ili hali wao wapo pale kulinda amani?

3: Je, vita ya Congo ni laana, adhabu na mateso ya malipo wanayolipa raia wa Congo iliyotendwa na mababu zao kwa kumuua Patrice Lumumba na kama ni laana je, kwanini hizi imani zetu zisitumike kuwaombea toba / msamaha kwa Muumba wao ili wa kae kwa amani na kama hazina nguvu kwanini tunaendelea kuziamini na kushikilia imani zisizoweza kusaidia ndugu zetu kwa kuwatoa matatizoni?

4: Kama ni kweli Rwanda inawapa ushirikiano M23 kama inavyodaiwa ni kwanini basi Raisi wa Congo au mkuu wa majeshi wa Congo asitangaze vita rasmi ya moja kwa moja kuivamia kijeshi na kuipiga Rwanda kwa kuatarisha amani ya raia wa Congo?

5: Kama Serikali ya Congo na Jeshi lake limeshindwa kupambana na M23 ni kwanini basi wasione ni vyema kuuza mji wa GOMA na viunga vyake kwa waasi ili raia wawe salama ?

6: Kwanini Congo hawataki kuigawanya iwe nchi mbili kama ilivyogawanywa sudani?

7: M23 wanapata wapi silaha nzito , mafunzo ya kijeshi na kuzitumia na zinapitia wapi, na kwanini wasipige huko zinakopitia na kuweka kambi imara za jeshi la congo ili kufunga milango ya kuingiza silaha na misaada kwa M23?

8: Je, mataifa ndani ya AU, EAC na SADC wanamtazamo gani kuhusu kuikomboa Congo ili liwe taifa huru, je , kwanini wasiweke vikwazo kwa taifa litakalo sadikika kuunga mkono hawa M23 na ikibidi ilipige moja kwa moja ?

9: Kama serikali ya Congo imeshindwa kabisa kupambania amani ya raia wake , ni kwanini wasilitoe sadaka Taifa la Congo liwe chini ya M23 na wajiundie serikali ili raia wawe na amani?

10: Kama mataifa ya Afrika yameshindwa kuisaidia Congo kuwafurusha , kuwaangamiza na kuwateketeza kabisa hawa M23 na vikundi vinavyofanana na hivyo kwanini Raisi wa Congo asiombe msaada kwa Rais wa Urusi ( Putin) amsaidie kuwafurusha waasi vikali?

11: Kama shida ni rasilimali zinazo patikana pale , ni kwanini basi serikali ya Congo isikabidhi maeneo hayo rasmi kwa jeshi tiifu yasimamiwe kijeshi na kwanini isiweke kambi za kijeshi mipakani na kuzunguka maeneo yote zilizo na rasilimali za madini ili waasi na mafisaidi iwe rahisi kushughulikiwa kikamilifu?

12: Ni kwanini raia wa mataifa mbali mbali ikiwemo yale ya ughaibuni hawaiombei Congo amani na kufanya maandamano kama vile walivyokua wanafanya ya free palestina ili dunia isikie na iwasaidie wakongoman?

13: Ni ipi hatima ya raia wa Congo iwapo majeshi yote yatashindwa kupambana na M23?

Naombeni kuwasilisha . Ni yapi maoni yenu kuhusu haya yanayojiri huko Congo miaka na miaka..
 
Congo iweke kambi kubwa ya jeshi karibu na Goma ili reinforcement iwe rahisi Muda ambapo kitanuka,waongeze rasilimali watu( mama ntilie,wauza samaki, n.k kwenye ushushushu,hapo Goma ili ku monitor matukio yeyote ya uvunjifu wa amani..
Iwekeze fedha kwenye mafunzo kwa vijana nje ya nchi...badala ya Rais na senior officers kulipwa mamilioni ya Pesa kila mwisho wa mwezi badala yake wapunguze mishahara then hizo Pesa walete vijana hata 1000 kwetu kwa mwaka mmoja tu naamini TPDF itawapika vizuri,then hao wakirudi Kwao wataweza kuwa wanabadilisha upepo kwenye Uwanja wa vita.
Wakazi wote wa Goma wawe na vitambulisho na watembee navyo.
 
Ndugu zangu...

Tumekua tukishuhudia, kuona na kusikia huko Congo DRC kukiwa na vita kali kati ya M23 na majeshi matiifu ya serikali, halikadhalika M23 wakinukuliwa kuwa na silaha nzito kuliko majeshi ya serikali , kuwashinda nguvu na kuwafurusha vikali pamoja na kuua wanajeshi wa Congo , pia kunyakua miji kirahisi sana huku wakisababisha mtafaruku wa ukosefu wa amani pamoja na vifo baina ya raia wasiokua na hatia miaka na miaka.

Maswali;

1: Kama kweli vile vikosi vya kulinda amani vipo pale kulinda amani ni kwanini hawapigani na maadui moja kwa moja pindi wanapo hatarisha amani ya watu wa congo, ni kwanini basi wasiingie vitani rasmi kupambana na M23 moja kwa moja?

2: Kwanini vile vikosi vyote vya kimataifa visiondolewe alafu congo iundwe upya na wajitangazie uhuru wao mpya tofauti na wa hawali kutokana na M23 kuendelea kusumbua ili hali wao wapo pale kulinda amani?

3: Je, vita ya Congo ni laana, adhabu na mateso ya malipo wanayolipa raia wa Congo iliyotendwa na mababu zao kwa kumuua Patrice Lumumba na kama ni laana je, kwanini hizi imani zetu zisitumike kuwaombea toba / msamaha kwa Muumba wao ili wa kae kwa amani na kama hazina nguvu kwanini tunaendelea kuziamini na kushikilia imani zisizoweza kusaidia ndugu zetu kwa kuwatoa matatizoni?

4: Kama ni kweli Rwanda inawapa ushirikiano M23 kama inavyodaiwa ni kwanini basi Raisi wa Congo au mkuu wa majeshi wa Congo asitangaze vita rasmi ya moja kwa moja kuivamia kijeshi na kuipiga Rwanda kwa kuatarisha amani ya raia wa Congo?

5: Kama Serikali ya Congo na Jeshi lake limeshindwa kupambana na M23 ni kwanini basi wasione ni vyema kuuza mji wa GOMA na viunga vyake kwa waasi ili raia wawe salama ?

6: Kwanini Congo hawataki kuigawanya iwe nchi mbili kama ilivyogawanywa sudani?

7: M23 wanapata wapi silaha nzito , mafunzo ya kijeshi na kuzitumia na zinapitia wapi, na kwanini wasipige huko zinakopitia na kuweka kambi imara za jeshi la congo ili kufunga milango ya kuingiza silaha na misaada kwa M23?

8: Je, mataifa ndani ya AU, EAC na SADC wanamtazamo gani kuhusu kuikomboa Congo ili liwe taifa huru, je , kwanini wasiweke vikwazo kwa taifa litakalo sadikika kuunga mkono hawa M23 na ikibidi ilipige moja kwa moja ?

9: Kama serikali ya Congo imeshindwa kabisa kupambania amani ya raia wake , ni kwanini wasilitoe sadaka Taifa la Congo liwe chini ya M23 na wajiundie serikali ili raia wawe na amani?

10: Kama mataifa ya Afrika yameshindwa kuisaidia Congo kuwafurusha , kuwaangamiza na kuwateketeza kabisa hawa M23 na vikundi vinavyofanana na hivyo kwanini Raisi wa Congo asiombe msaada kwa Rais wa Urusi ( Putin) amsaidie kuwafurusha waasi vikali?

11: Kama shida ni rasilimali zinazo patikana pale , ni kwanini basi serikali ya Congo isikabidhi maeneo hayo rasmi kwa jeshi tiifu yasimamiwe kijeshi na kwanini isiweke kambi za kijeshi mipakani na kuzunguka maeneo yote zilizo na rasilimali za madini ili waasi na mafisaidi iwe rahisi kushughulikiwa kikamilifu?

12: Ni kwanini raia wa mataifa mbali mbali ikiwemo yale ya ughaibuni hawaiombei Congo amani na kufanya maandamano kama vile walivyokua wanafanya ya free palestina ili dunia isikie na iwasaidie wakongoman?

13: Ni ipi hatima ya raia wa Congo iwapo majeshi yote yatashindwa kupambana na M23?

Naombeni kuwasilisha . Ni yapi maoni yenu kuhusu haya yanayojiri huko Congo miaka na miaka..
Mm binafs nnaona wacongo man wassubir misaada ya nch zngne je wao kama taifa wanamaono gan kwa nch yao inawapaswa kuwa wazalendo mbali na kukata mauno na kupenda mpira wamtazame sasa mama yao kwa kumpgania wenyw syo kukimbia
 
Namlaumu sana JK kwa kumsamehe PK ule mwaka; JK na jeshi letu walipiga show ya kibabe hadi PK akaomba poo, yule hakutakiwa kusamehewa, alitakiwa kuondolewa kabisa madarakani, see it now; kanazidi kusumbua tu
Paul Kagame nchi yake ni ya kawaida na jeshi lake ni la kawaida. Isipokuwa anatumia udhaifu wa jeshi la Congo na ndiyo maana anaonekana kama ni nchi yenye jeshi hatari. Si wa kutisha ni nchi ya kawaida na yenye jeshi la kawaida.

Tukirudi kwenye nukta yako ya msingi labda tujiulize: Kwa nini maeneo ambayo yanakombolewa yakikabidhiwa kwa jeshi la Congo hayachukui muda mrefu yanarudi kwa waasi?

Jawabu ni kwamba mchezo unaotokea Congo viongozi wa serikali nao unawanufaisha hivyo hawataki uishe. Na serikali yao wanaitumia hii kama njia ya siasa ya kupata madaraka.


Angalia kipindi cha uchaguzi rais wao alivyokuwa wa moto kuonyesha kwamba anataka kuipigania Congo mpaka watu walidhani itatokea vita kati ya Congo na Rwanda. Ila baada ya kushinda uchaguzi kapoa.

Nchi ya Congo ni taifa lililofeli. Hawa hatakama mkiwakombolea nchi nzima baada ya miezi kadhaa maeneo yatarudishwa kwa waasi. Kwa lugha nyepesi kinachoendelea Congo inabidi majeshi ya nchi nyengine yabaki huko miaka na miaka mpaka wakijielewa.

Sasa huu ni ujinga! Huwezi kuwapigania watu ambao hawataki kujipigania. Suluhisho ni moja tu; kuwaacha wenyewe wapigane na kuwafungia mipaka. Kama nchi yao ikimeguka waachwe hivyo hivyo! Akili itawarudia tu wakianza kuuwana kama wanyama.
 
Kagame ndiye shida katika ukanda huu wa maziwa makuu lakini tatizo ni ile hulka ya kiafrika ya unafiki, hakuna kiongozi yeyote wa kiafrika aliye tayari kumnyoshea kidole hata hiyo anayoita AU haina maana yoyote.

Wakati Russia ilipoivamia Ukraine mataifa ya Ulaya hayakupepesa macho na yaliiunga mkono Ukraine na kuiokoa serikali iliyochaguliwa kidemokrasia na wananchi iendelee kuwepo madarakani hadi leo kitu ambacho Afrika kamwe haiwezi kufanya. Afrika bure kabisa.
 

Attachments

  • VID-20250128-WA0004.mp4
    14.8 MB
Cha kufanya M23 wapigwe hadi Kigali,yaani vita ihamie upande wa Rwanda ndio PK akili itamkaa sawa
 
Paul Kagame nchi yake ni ya kawaida na jeshi lake ni la kawaida. Isipokuwa anatumia udhaifu wa jeshi la Congo na ndiyo maana anaonekana kama ni nchi yenye jeshi hatari. Si wa kutisha ni nchi ya kawaida na yenye jeshi la kawaida.

Tukirudi kwenye nukta yako ya msingi labda tujiulize: Kwa nini maeneo ambayo yanakombolewa yakikabidhiwa kwa jeshi la Congo hayachukui muda mrefu yanarudi kwa waasi?

Jawabu ni kwamba mchezo unaotokea Congo viongozi wa serikali nao unawanufaisha hivyo hawataki uishe. Na serikali yao wanaitumia hii kama njia ya siasa ya kupata madaraka.


Angalia kipindi cha uchaguzi rais wao alivyokuwa wa moto kuonyesha kwamba anataka kuipigania Congo mpaka watu walidhani itatokea vita kati ya Congo na Rwanda. Ila baada ya kushinda uchaguzi kapoa.

Nchi ya Congo ni taifa lililofeli. Hawa hatakama mkiwakombolea nchi nzima baada ya miezi kadhaa maeneo yatarudishwa kwa waasi. Kwa lugha nyepesi kinachoendelea Congo inabidi majeshi ya nchi nyengine yabaki huko miaka na miaka mpaka wakijielewa.

Sasa huu ni ujinga! Huwezi kuwapigania watu ambao hawataki kujipigania. Suluhisho ni moja tu; kuwaacha wenyewe wapigane na kuwafungia mipaka. Kama nchi yao ikimeguka waachwe hivyo hivyo! Akili itawarudia tu wakianza kuuwana kama wanyama.
Uko sahihi sana kaka; nakumbuka juzi tu, chini ya miezi 6 iliopita, jeshi letu lilikwenda kuwasaidia, M23 walipigwa vizuri sana, same day baada ya kipigo, wanajeshi wa Congo wakaonekana sehemu wanakula pombe na kucheza music, yaani wanasherehekea kabla hata hawaja stabilize, pumbafu sana
 
Uko sahihi sana kaka; nakumbuka juzi tu, chini ya miezi 6 iliopita, jeshi letu lilikwenda kuwasaidia, M23 walipigwa vizuri sana, same day baada ya kipigo, wanajeshi wa Congo wakaonekana sehemu wanakula pombe na kucheza music, yaani wanasherehekea kabla hata hawa stabilize, pumbafu sana
Congo ni Taifa la hovyo kwa muda mrefu sana.

Che Guevara mwenyewe aliondoka Congo baada ya kuona wana ujinga mwingi.

Guevara aligundua Congo si wapiganaji, ni rahisi kununulika na kutoa taarifa nje, serikali haitoi support ya kutosha, wanajeshi wake wanapenda starehe na ni waoga kwenye mapambano. Akaona mambo yasiwe mengi akaondoka.

Madhaifu ya hapo juu ndiyo anayoyatumia Paul Kagame. Watu wanamuona kama ni mtu hatari, ila kiukweli anazichezea nchi dhaifu.

Suala kama hilo lilitokea Msumbiji, kikundi cha Wagner cha Warusi kilikwenda kule kupigana na magaidi. Ajabu wanajeshi wa serikali waoga, wanawaacha wagner wanapigana wenyewe!

Halafu serikali haitoi support ya kutosha kuonyesha kuwa inataka kumaliza magaidi. Wagner wakaona mambo yasiwe mengi, wakafungasha virago wakaondoka. Kwa sababu huwezi kuwapigania watu ambao hawataki kujipigania.

Hii hali ndiyo wanayo Congo, laiti kama wangelikuwa wapo tayari kujipigania hao waasi wangekuwa wameshamalizwa kitambo.

Unaingia kandarasi na nchi kubwa kama Russia, unawapa mgodi au migodi kadhaa kama fidia wapambane na waasi wote na wasifishe nchi wakiwa pamoja na wanajeshi wenu.

Kisha kuwaomba wawa training wanajeshi wenu na kuwaacha wawalinde kwa takribani hata miaka 20.
 
Congo ni Taifa la hovyo kwa muda mrefu sana.

Che Guevara mwenyewe aliondoka Congo baada ya kuona wana ujinga mwingi.

Guevara aligundua Congo si wapiganaji, ni rahisi kununulika na kutoa taarifa nje, serikali haitoi support ya kutosha, wanajeshi wake wanapenda starehe na ni waoga kwenye mapambano. Akaona mambo yasiwe mengi akaondoka.

Madhaifu ya hapo juu ndiyo anayoyatumia Paul Kagame. Watu wanamuona kama ni mtu hatari, ila kiukweli anazichezea nchi dhaifu.

Suala kama hilo lilitokea Msumbiji, kikundi cha Wagner cha Warusi kilikwenda kule kupigana na magaidi. Ajabu wanajeshi wa serikali waoga, wanawaacha wagner wanapigana wenyewe!

Halafu serikali haitoi support ya kutosha kuonyesha kuwa inataka kumaliza magaidi. Wagner wakaona mambo yasiwe mengi, wakafungasha virago wakaondoka. Kwa sababu huwezi kuwapigania watu ambao hawataki kujipigania.

Hii hali ndiyo wanayo Congo, laiti kama wangelikuwa wapo tayari kujipigania hao waasi wangekuwa wameshamalizwa kitambo.

Unaingia kandarasi na nchi kubwa kama Russia, unawapa mgodi au migodi kadhaa kama fidia wapambane na waasi wote na wasifishe nchi wakiwa pamoja na wanajeshi wenu.

Kisha kuwaomba wawa training wanajeshi wenu na kuwaacha wawalinde kwa takribani hata miaka 20.
Sahihi sana kaka. Umegusia habari za Msumbiji, hawa nao ndio siwaelewagi kabisa, hawa wamekua wanapigana for years, since mwaka 1975 wanapata uhuru I think hadi mwanzoni mwa miaka ya 90, why hawaoneshi kwamba they have experience? Anyway, majirani zetu pasua kichwa sana. Ifike hatua, tuanze kuwakatalia kuja huku kama ukimbizini
 
Vita ya Congo imeka kimtego sana. Unajua kwanin inakuwa ngumu sana hii vita kuisha, ukiacha haya mambo ya madini hawa waasi wa 23 ni watutsi. Moja ya masharti yao wanataka waingizwe kweny jesho la Congo na wengine wapewe nafasi zingine serikali hapa ndipo penye ugumu.
Kwahiyo inachogopa serikali ya Congo kukubaliana na masharti ya M23 wanahisi wanamwingiza mtutsi ndani ya serikali ambae asili yake ni Rwanda. Hapa ndipo inapotajwa Rwanda kwenye huu mgogoro.
 
Kagame ndiye shida katika ukanda huu wa maziwa makuu lakini tatizo ni ile hulka ya kiafrika ya unafiki, hakuna kiongozi yeyote wa kiafrika aliye tayari kumnyoshea kidole hata hiyo anayoita AU haina maana yoyote.

Wakati Russia ilipoivamia Ukraine mataifa ya Ulaya hayakupepesa macho na yaliiunga mkono Ukraine na kuiokoa serikali iliyochaguliwa kidemokrasia na wananchi iendelee kuwepo madarakani hadi leo kitu ambacho Afrika kamwe haiwezi kufanya. Afrika bure kabisa.
Hapana, kwa upande wa Ukraine umedanganya ndugu.

Ukweli ni kwamba Urusi alipinga Ukraine isijiunge na NATO,Lavrov alizunguka west yote kuwaomba waheshimu ombi la Urusi lkn walimpuuza.ndipo Urusi ikaweka mstari mwekundu Ukraine na NATO wasivuke,wakavuka,Urusi ikavamia.
 
Viongozi wa Afrika wa Sasa ni Vibaka Nashukuru Kwa JK Kikwete Alisema wakumaliza vita hii ni Kagame akutaka kuzunguka Kipindi Mwenyekiti AU
 
Namlaumu sana JK kwa kumsamehe PK ule mwaka; JK na jeshi letu walipiga show ya kibabe hadi PK akaomba poo, yule hakutakiwa kusamehewa, alitakiwa kuondolewa kabisa madarakani, see it now; kanazidi kusumbua tu
Mseven 7 ilibidi amuombe sana JK na Jomo kenyatta
 
Paul Kagame nchi yake ni ya kawaida na jeshi lake ni la kawaida. Isipokuwa anatumia udhaifu wa jeshi la Congo na ndiyo maana anaonekana kama ni nchi yenye jeshi hatari. Si wa kutisha ni nchi ya kawaida na yenye jeshi la kawaida.

Tukirudi kwenye nukta yako ya msingi labda tujiulize: Kwa nini maeneo ambayo yanakombolewa yakikabidhiwa kwa jeshi la Congo hayachukui muda mrefu yanarudi kwa waasi?

Jawabu ni kwamba mchezo unaotokea Congo viongozi wa serikali nao unawanufaisha hivyo hawataki uishe. Na serikali yao wanaitumia hii kama njia ya siasa ya kupata madaraka.


Angalia kipindi cha uchaguzi rais wao alivyokuwa wa moto kuonyesha kwamba anataka kuipigania Congo mpaka watu walidhani itatokea vita kati ya Congo na Rwanda. Ila baada ya kushinda uchaguzi kapoa.

Nchi ya Congo ni taifa lililofeli. Hawa hatakama mkiwakombolea nchi nzima baada ya miezi kadhaa maeneo yatarudishwa kwa waasi. Kwa lugha nyepesi kinachoendelea Congo inabidi majeshi ya nchi nyengine yabaki huko miaka na miaka mpaka wakijielewa.

Sasa huu ni ujinga! Huwezi kuwapigania watu ambao hawataki kujipigania. Suluhisho ni moja tu; kuwaacha wenyewe wapigane na kuwafungia mipaka. Kama nchi yao ikimeguka waachwe hivyo hivyo! Akili itawarudia tu wakianza kuuwana kama wanyama.
True
 
Sahihi sana kaka. Umegusia habari za Msumbiji, hawa nao ndio siwaelewagi kabisa, hawa wamekua wanapigana for years, since mwaka 1975 wanapata uhuru I think hadi mwanzoni mwa miaka ya 90, why hawaoneshi kwamba they have experience? Anyway, majirani zetu pasua kichwa sana. Ifike hatua, tuanze kuwakatalia kuja huku kama ukimbizini
Michezo
 
Ndugu zangu...

Tumekua tukishuhudia, kuona na kusikia huko Congo DRC kukiwa na vita kali kati ya M23 na majeshi matiifu ya serikali, halikadhalika M23 wakinukuliwa kuwa na silaha nzito kuliko majeshi ya serikali , kuwashinda nguvu na kuwafurusha vikali pamoja na kuua wanajeshi wa Congo , pia kunyakua miji kirahisi sana huku wakisababisha mtafaruku wa ukosefu wa amani pamoja na vifo baina ya raia wasiokua na hatia miaka na miaka.

Maswali;

1: Kama kweli vile vikosi vya kulinda amani vipo pale kulinda amani ni kwanini hawapigani na maadui moja kwa moja pindi wanapo hatarisha amani ya watu wa congo, ni kwanini basi wasiingie vitani rasmi kupambana na M23 moja kwa moja?

2: Kwanini vile vikosi vyote vya kimataifa visiondolewe alafu congo iundwe upya na wajitangazie uhuru wao mpya tofauti na wa hawali kutokana na M23 kuendelea kusumbua ili hali wao wapo pale kulinda amani?

3: Je, vita ya Congo ni laana, adhabu na mateso ya malipo wanayolipa raia wa Congo iliyotendwa na mababu zao kwa kumuua Patrice Lumumba na kama ni laana je, kwanini hizi imani zetu zisitumike kuwaombea toba / msamaha kwa Muumba wao ili wa kae kwa amani na kama hazina nguvu kwanini tunaendelea kuziamini na kushikilia imani zisizoweza kusaidia ndugu zetu kwa kuwatoa matatizoni?

4: Kama ni kweli Rwanda inawapa ushirikiano M23 kama inavyodaiwa ni kwanini basi Raisi wa Congo au mkuu wa majeshi wa Congo asitangaze vita rasmi ya moja kwa moja kuivamia kijeshi na kuipiga Rwanda kwa kuatarisha amani ya raia wa Congo?

5: Kama Serikali ya Congo na Jeshi lake limeshindwa kupambana na M23 ni kwanini basi wasione ni vyema kuuza mji wa GOMA na viunga vyake kwa waasi ili raia wawe salama ?

6: Kwanini Congo hawataki kuigawanya iwe nchi mbili kama ilivyogawanywa sudani?

7: M23 wanapata wapi silaha nzito , mafunzo ya kijeshi na kuzitumia na zinapitia wapi, na kwanini wasipige huko zinakopitia na kuweka kambi imara za jeshi la congo ili kufunga milango ya kuingiza silaha na misaada kwa M23?

8: Je, mataifa ndani ya AU, EAC na SADC wanamtazamo gani kuhusu kuikomboa Congo ili liwe taifa huru, je , kwanini wasiweke vikwazo kwa taifa litakalo sadikika kuunga mkono hawa M23 na ikibidi ilipige moja kwa moja ?

9: Kama serikali ya Congo imeshindwa kabisa kupambania amani ya raia wake , ni kwanini wasilitoe sadaka Taifa la Congo liwe chini ya M23 na wajiundie serikali ili raia wawe na amani?

10: Kama mataifa ya Afrika yameshindwa kuisaidia Congo kuwafurusha , kuwaangamiza na kuwateketeza kabisa hawa M23 na vikundi vinavyofanana na hivyo kwanini Raisi wa Congo asiombe msaada kwa Rais wa Urusi ( Putin) amsaidie kuwafurusha waasi vikali?

11: Kama shida ni rasilimali zinazo patikana pale , ni kwanini basi serikali ya Congo isikabidhi maeneo hayo rasmi kwa jeshi tiifu yasimamiwe kijeshi na kwanini isiweke kambi za kijeshi mipakani na kuzunguka maeneo yote zilizo na rasilimali za madini ili waasi na mafisaidi iwe rahisi kushughulikiwa kikamilifu?

12: Ni kwanini raia wa mataifa mbali mbali ikiwemo yale ya ughaibuni hawaiombei Congo amani na kufanya maandamano kama vile walivyokua wanafanya ya free palestina ili dunia isikie na iwasaidie wakongoman?

13: Ni ipi hatima ya raia wa Congo iwapo majeshi yote yatashindwa kupambana na M23?

Naombeni kuwasilisha . Ni yapi maoni yenu kuhusu haya yanayojiri huko Congo miaka na miaka..
Rwanda ikikemewa na wakubwa wa Dunia lazima Drc itulie.
 
Viongozi wa Afrika wa Sasa ni Vibaka Nashukuru Kwa JK Kikwete Alisema wakumaliza vita hii ni Kagame akutaka kuzunguka Kipindi Mwenyekiti AU
Malema alisema AU ni kijiwe cha wazee kupiga gahawa!

Na hakukosea!
 
Back
Top Bottom