Viti Maalumu vya Ubunge na Udiwani

IshaLubuva

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2008
Posts
250
Reaction score
11
Imeshakuwa ni muda sasa tangu ilipoamuliwa kuwapatia wanawake upendeleo wa kuwa na nafasi za Udiwani na Ubunge zijulikanazo kama Viti Maalum. Oktoba mwaka huu wa 2010 tunaendaq kufanya uchaguzi wa madiwani, wabunge na Rais. Ningependa wana JF tujadiliane kuhusu nani hasa anayenufaika na nafasi hizi za viti maalum? Je, ni kweli kuwa wanawake wa Kitanzania wananufaika kwa namna yoyote? Mbona nafasi hizi zimeendelea, kwa kiasi kikubwa, kugawanywa miongoni mwa wake za wakubwa tu?. Je, kuna haja ya kuendelea kuwa na nafasi hizi?
 
wanaonufaika ni hao wake za wakubwa ambao wameona viti maalum ni sehemu ya ajira. I dont know why someone is an mp on special seats for 15 years na bado anang,ng,ania tu kugombea hadi 2010.whyyyyy?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…