KERO Vitongoji vinavyokizunguka Chuo cha Mzumbe Morogoro ni vichafu mnoo

KERO Vitongoji vinavyokizunguka Chuo cha Mzumbe Morogoro ni vichafu mnoo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

TulaSawyer

Member
Joined
Jun 11, 2017
Posts
20
Reaction score
41
Habari wanajukwaa!!

Kero yangu ni jinsi mazingira ya vitongoji vinavyokizunguka chuo kikuu cha Mzumbe vilivyo vichafu, inakera kweli, unabaki kujiuliza ustaarabu wa mtanzania uko wapi?! Au hadi aje mtu mweupe (kwa hisani, ndipo mazingira yawe masafi)?.

Kwanza ungedhani Ile kukaa karibu na chuo kikuu maisha yangekuwa na ustaarabu kidogo, huku ni kinyume kabisa. Kwanza biashara holela ni nyingi mnooo, taka zinatupwa popote, makazi mengi yamejengwa holela ( huu ni utamaduni sehemu nyingi za Tanzania, ni maada pana haswaaa).

Hakuna mtaa utapita na ukaona ni kusafi. Mbaya zaidi hii ni wilaya ya Mvomero, kwahiyo hata gari za taka zinazoonekana manispaa ya Morogoro hazifiki huku. Pia sifahamu utaratibu wa ukusanyaji taka kwa wilaya ya Mvomero upoje.

Watoto wetu wanacheza mazingira machafu, jamani inatia kinyaa. Mtu mweusi ni kama amerogwa!!! Kipindi cha mvua Sasa Kuna mitaa huwezi hata kuingia.

Wananchi, hili tunaweza wenyewe, siyo lazima muda wote hadi tuletewe misaada. Ule utaratibu ulioanzishwa na hayati Rais Magufuli kwakweli urudishwe, usafi ni tabia, siyo kitu Cha kujifunza siku Moja. Tuone Kuna haja ya kurithisha vizazi vyetu mazingira masafi.

Inatia aibu kuamini watu waliosoma wanaishi mazingira machafu hivi, elimu yetu haitukomboi kwa chochote. Watoto wanakuwa wanaona uchafu kila siku na Sasa wanajengeka hivyo, na wanakuwa wanaamini hayo ndiyo mazingira sawa kabisa kuishi. Hii haijakaa sawa!!
Asanteni.
 
Mzumbe ipi unazungumzia mzee?
Kilimahewa hakuna uchafu wowote ni sehemu nzuri kabisa ya kuishi.
Upande wa juu ilipo mzumbe sekondari pia hamna kero yoyote ile ya uchafu.
Maeneo ya geti kubwa ni mazuri pako kistaarabu.
Eneo la changarawe ndo hakuna ustaarabu sababu kumejaa waswahili na watu masikini lakini uchafu sidhani labda sababu sijaenda huko mda mrefu.

Alafu kingine gari la taka vijijini umeshawahi kuona wapi? vijijini kila mtu anachimba shimo la taka.

Mazingira ya mzumbe hayana tofauti na mazingira ya vyuo vingine tz.
 
Wewe umechukua hatua gani binafsi?
Kulalamika mtandaoni haisaidii kitu
Wewe umechukua hatua gani kupunguza huo uchafu?
Narudia tena, kulalamika mtandaoni sio jawabu, na hii ni tabia ambayo wa Tanzania wengi tunayo...
 
Mzumbe ipi unazungumzia mzee?
Kilimahewa hakuna uchafu wowote ni sehemu nzuri kabisa ya kuishi.
Upande wa juu ilipo mzumbe sekondari pia hamna kero yoyote ile ya uchafu.
Maeneo ya geti kubwa ni mazuri pako kistaarabu.
Eneo la changarawe ndo hakuna ustaarabu sababu kumejaa waswahili na watu masikini lakini uchafu sidhani labda sababu sijaenda huko mda mrefu.

Alafu kingine gari la taka vijijini umeshawahi kuona wapi? vijijini kila mtu anachimba shimo la taka.

Mazingira ya mzumbe hayana tofauti na mazingira ya vyuo vingine tz.
Nina mtizamo kama huu maana kwa mda nilio ishi pale sikuona huo uchafu mkuuubwa kiasi Cha kufungua Uzi lakini pia sio mbaya kuchukua tahadhari mtoa mada ahudhurie kikao kimoja TU Cha mkutano wa Kijiji Cha changarawe na kutoa ushauri wa haraka ya kutenga eneo maalumu la kutupa taka na kuboresha mazingira
 
Mzumbe ipi unazungumzia mzee?
Kilimahewa hakuna uchafu wowote ni sehemu nzuri kabisa ya kuishi.
Upande wa juu ilipo mzumbe sekondari pia hamna kero yoyote ile ya uchafu.
Maeneo ya geti kubwa ni mazuri pako kistaarabu.
Eneo la changarawe ndo hakuna ustaarabu sababu kumejaa waswahili na watu masikini lakini uchafu sidhani labda sababu sijaenda huko mda mrefu.

Alafu kingine gari la taka vijijini umeshawahi kuona wapi? vijijini kila mtu anachimba shimo la taka.

Mazingira ya mzumbe hayana tofauti na mazingira ya vyuo vingine tz.
Siyo lazima uone dampo ndo ukubali mitaa ni michafu. Ukitembea tu barabarani utaona kulivyoo karatasi, makopo, na hiyo hali Iko kila sehemu Tanzania ndiyo maana unaona sawa. Chuo hakuna shida, Kuna watu wanafanya usafi. Huku mitaani Sasa. Na labda ukipita hiyo njia ya lami unahisi kote kupo hivyo. Ingiza barabara za mitaani, watu hawachimbi mashimo ya taka, wanazimwaga taka barabarani. Baadae nitakuletea picha uone. Ni vile TU watanzania tumekubaki kusettle for less.
 
Wewe umechukua hatua gani binafsi?
Kulalamika mtandaoni haisaidii kitu
Wewe umechukua hatua gani kupunguza huo uchafu?
Narudia tena, kulalamika mtandaoni sio jawabu, na hii ni tabia ambayo wa Tanzania wengi tunayo...
Kila siku naokota taka mtaani kwangu nazichoma. Baadae zinaletwa Tena na upepo kwasababu watu hawatunzi taka zao. Na watu wakipita wanakunywa energy drinks zao wanatupa TU popote. Nimeuona uongozi wa Kijiji kuona tutasaidianaje, kwasababu mtu mMoja huwezi badili hali ya mazingira peke Yako, utakuwa unatwanga maji kwenye kinu. Kwahiyo sijalaumu, nimeileta hapa ili kuvuta attention ya watu wengine pia. Narudia, usafi ni utamaduni, inahitaji nguvu ya jamii na siyo mtu mMoja. Ndiyo maana hata ninachofanya kinaweza kisionekane. Mazingira ya nyumbani kwangu yakiwa masafi, halafu barabara ya kuingilia mtaani kwangu imejaa uchafu, ni kazi bure.
 
Back
Top Bottom