Vitu vitatu vinavyopunguza makusanyo ya kodi

Vitu vitatu vinavyopunguza makusanyo ya kodi

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Makusanyo ya kodi za Tanzania hayafikii malengo kwa sababu ya vitu vitatu vikubwa

1. Machinga: Hatuwezi kuwa na kundi la watu wasiolipa kodi na wawe na haki kuliko walipa kodi. Huwezi kuruhusu wamachinga kuuza vitu vipya bila kodi na sehemu yoyote na hata mbele ya maduka ya walipa kodi. Wanachafua mazingira sana sehemu za barabarani na kuongeza gharama za ushafishaji maji na mitaro. Bila kutafuta utaratibu mzuri wamachinga wanapunguza sana makusanyo ya kodi huo ndiyo ukweli. Yaani unaweza kuwa na machinga wako usilipe kodi hata kidogo.

2. Wanunuzi wanaokubali kulipa kidogo na kukwepa kodi. Mtu yeyote anayekubali kununua kitu bila risiti na wale wauzaji wanaotoa vitu kwa bei ya chini kama hutaki risiti inatakiwa wafungwe. Hii itazuia hii tabia yaani nchi nyingine kuuza bila kutoa risiti ni uhujumu uchumi. Huruma huruma inatakiwa kuisha.

3. Madalali wengi wanapunguza kodi na kuzuia teknologia kutumika mfano kwenye magari kungekuwa na utaratibu wa kununua ticket kwa simu pekee ili kodi ilipwe hukohuko lakini madalali wamekuwa na nguvu za kuzuia maendeleo haya. Lakini kuna madalali wa nyumba, mazao .... ambao hawana tija kwa taifa letu. Udalali usio na manufaa nao upigwe marufuku
 
Makusanyo ya kodi za Tanzania hayafikii malengo kwa sababu ya vitu vitatu vikubwa

1. Machinga: Hatuwezi kuwa na kundi la watu wasiolipa kodi na wawe na haki kuliko walipa kodi. Huwezi kuruhusu wamachinga kuuza vitu vipya bila kodi na sehemu yoyote na hata mbele ya maduka ya walipa kodi. Wanachafua mazingira sana sehemu za barabarani na kuongeza gharama za ushafishaji maji na mitaro. Bila kutafuta utaratibu mzuri wamachinga wanapunguza sana makusanyo ya kodi huo ndiyo ukweli. Yaani unaweza kuwa na machinga wako usilipe kodi hata kidogo.

2. Wanunuzi wanaokubali kulipa kidogo na kukwepa kodi. Mtu yeyote anayekubali kununua kitu bila risiti na wale wauzaji wanaotoa vitu kwa bei ya chini kama hutaki risiti inatakiwa wafungwe. Hii itazuia hii tabia yaani nchi nyingine kuuza bila kutoa risiti ni uhujumu uchumi. Huruma huruma inatakiwa kuisha.

3. Madalali wengi wanapunguza kodi na kuzuia teknologia kutumika mfano kwenye magari kungekuwa na utaratibu wa kununua ticket kwa simu pekee ili kodi ilipwe hukohuko lakini madalali wamekuwa na nguvu za kuzuia maendeleo haya. Lakini kuna madalali wa nyumba, mazao .... ambao hawana tija kwa taifa letu. Udalali usio na manufaa nao upigwe marufuku

Tunashukuru wameona hili kuhusu machinga
 
Tiketi kwa njia ya mtandao bado wakati walusema lutaanza hivi karibuni, wapiga debe wana nguvu ya kuishauri serikali iache.
 
Tiketi kwa njia ya mtandao bado wakati walusema lutaanza hivi karibuni, wapiga debe wana nguvu ya kuishauri serikali iache.
Waziri wa fedha hana ubunifu. Period!!!
 
Waziri WA Tamisemi ameshiba na kujipangia Budget ya Trillion 8 bila kuwa na fikra zinatoka wapi anaanza kuwasodoa wakuu wamikoa wanaopanga taratibu za kuzikusanya!!!
 
Sio kweli
Tanzania kiwango cha kodi ni kidogo kwa sababu shughuli za biashara zisizo za kuganga njaa ambazo zinaweza kulipa kodi vizuri ni chache.Volume ya biashara Tanzania ni ndogo sana japo tuna rasilimali nyingi za kupanua kiwango cha ukubwa wa biashara nchini. Ukianza kukomaa na kodi za wamachinga, mama ntilie na bodaboda ambao ni waganga njaa tu ndio unaharibu kabisa.
 
Kodi pekee sio tegemeo. Mbona mkoloni hakuendesha nchi kwa kodi na alifanya makubwa Sana bila kodi, kutegemea kodi kutoka kwa watu masikini wasiozalisha sidhani kama tunaweza songa. Pili yafaa nini kukusanya kodi kisha zinapigwa na hatua hazichukuliwi
 
Hao wanaoaminuka wanalipa kodi ndio wakwepaji wakuu.

Kuna watu hawaingizi chochote na wanakatwa kodi.

Hata kidogo kinachopatikana, kinapigwa.
 
Sijui mwanasiasa gani aliwahi ropoka Tanzania kodi inayopatikana bandarini inatosha kutuvusha watanzania wote haswa serikali.
 
Makusanyo ya kodi za Tanzania hayafikii malengo kwa sababu ya vitu vitatu vikubwa

1. Machinga: Hatuwezi kuwa na kundi la watu wasiolipa kodi na wawe na haki kuliko walipa kodi. Huwezi kuruhusu wamachinga kuuza vitu vipya bila kodi na sehemu yoyote na hata mbele ya maduka ya walipa kodi. Wanachafua mazingira sana sehemu za barabarani na kuongeza gharama za ushafishaji maji na mitaro. Bila kutafuta utaratibu mzuri wamachinga wanapunguza sana makusanyo ya kodi huo ndiyo ukweli. Yaani unaweza kuwa na machinga wako usilipe kodi hata kidogo.

2. Wanunuzi wanaokubali kulipa kidogo na kukwepa kodi. Mtu yeyote anayekubali kununua kitu bila risiti na wale wauzaji wanaotoa vitu kwa bei ya chini kama hutaki risiti inatakiwa wafungwe. Hii itazuia hii tabia yaani nchi nyingine kuuza bila kutoa risiti ni uhujumu uchumi. Huruma huruma inatakiwa kuisha.

3. Madalali wengi wanapunguza kodi na kuzuia teknologia kutumika mfano kwenye magari kungekuwa na utaratibu wa kununua ticket kwa simu pekee ili kodi ilipwe hukohuko lakini madalali wamekuwa na nguvu za kuzuia maendeleo haya. Lakini kuna madalali wa nyumba, mazao .... ambao hawana tija kwa taifa letu. Udalali usio na manufaa nao upigwe marufuku
Ukikimbilia kuwa kuna kundi hili halilipi kodi wakati ni kufanya utaratibu mzuri wakalipa kogi! Sio haki! Nchi hii ni yetu sote! Kama iliwezekana wakatengenezewa vitambulisho na vikawawezesha kuaminiwa na bank na kufanya marejesho yao bila wasiwasi,
Nchi yetu mifumo ya elimu ni mibaya sana
 
Umekwenda Dukani kununua bidhaa fulani, unaambiwa ukitaka risiti bei ni 250k, bila risiti ni 220k, wewe kama mtozonia mzalendo utachagua bei ipi?


Kuna sheria, kisha kuna uhalisia.
 
Back
Top Bottom