Vituko jikoni, Let us share and have fun

Vituko jikoni, Let us share and have fun

Angel Nylon

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2011
Posts
9,164
Reaction score
18,402
Habari zenu wanajiko.

Leo ningependa tushee mambo yanayotutokea jikoni, yale ya vituko vituko.

Mie mengi yamewahi kunikuta lkn ntaweka machache tu.

Kuna siku mama yangu aliniwachia niangalie pishi la mseto, sikujua kama kabla haujaepuliwa haukorogwi na mwiko si niukoroge, wacha mseto uungue. Nligombwajeee mpk leo nimejua kama mseto haukorogwi hadi uepuliwe ndo usongwe kama ugali.

Nlikua nkikaa jikoni na mama kupika, pishi kama halijaja vizuri basi hufukuzwa jikoni ati naambiwa macho yangu ndo yameharibu, lol.

Kuna siku nlikuwa nataka kukaanga chips, nkakosea kwenye karai badala ya kuweka mafuta nkaweka siki, si muda jikoni kumejaa moshi na harufu ya ajabu kuja kuangalia kumbe nimebeba chupa ya siki badala ya mafuta.

Usiombe kuumua maandazi ukaweka sukari nyingi, utalala hata siku mbili hayajaumuka, hii mpk leo hii mi mwenzenu mara hubugi step.

Haya wana jiko hem na wengine waeleze vituko vinavowapata jikoni, au vilowahi kuwapata wakati wanjifundisha kupika, au kitu gani hupendi uwapo jikoni.
 
Habibty hahahahah mie hiyo ya maandazi ilowahi nikuta zaman siku mama kaenda shopping kwa ajili ya eid ilikua ramadhan nakumbuka basi akaniambia nipike maandazi yeye akirudi atakuja kuchoma....shoga nkalikanda andaaz lainiii wakat anaraudi sasa karibia maghrib anataka kuyachoma bado hayajaumuka na mie kila nkiyasubiri hayaumuki weee kumbe mesahau kutia hamira nlisemwa na makofi mawili mazuriiii lol
 
Hahahah hii ya dada angu

Siku tukatamani mchuzi wa nazi.....mie nikaandaa kila kitu yeye akakuna nazi mana yeye ndo mpishi siku hiyo saaa basi tui la nazi hilo lita 2 lol bibk jingi utasema linataka kupikiwa mchuzi wa shughuli lol nkamwambia abla (dada) hilo tui jingiiii sana weee akanishikisha adabu nkae kimyaaa....

Habibty ulipikwa mchuzi ma hotpot mawili kwa wingi nyama yenyewe kilo 1 alafu mwepesiii kama wa maji hahahahahhahahaha nahiyo chumvi na ma ndimu acha tu ila huwezi amini nipishi hodari sana nowadays kwenye mapishi namugopajeeee......

Mkiona id Sherose jf chef ni yeye anakuja soon
 
Last edited by a moderator:
Hahahah hii ya dada angu

Siku tukatamani mchuzi wa nazi.....mie nikaandaa kila kitu yeye akakuna nazi mana yeye ndo mpishi siku hiyo saaa basi tui la nazi hilo lita 2 lol bibk jingi utasema linataka kupikiwa mchuzi wa shughuli lol nkamwambia abla (dada) hilo tui jingiiii sana weee akanishikisha adabu nkae kimyaaa....

Habibty ulipikwa mchuzi ma hotpot mawili kwa wingi nyama yengewe kilo 1 alafu mwepesiii kama wa maji hahahahahhahahaha nahiyo chumvi na ma ndimu acha tu ila huwezi amini nipishi hodari sana nowadays kwenye mapishi namugopajeeee......

Mkiona id Sherose jf chef ni yeye anakuja sopn

Ha ha haaaaaaaa. Hii Kali kuliko
 
Last edited by a moderator:
Hahahahaha wapishi muna visaa....mi nikibugi simpelekei mtu pishi langu zaidi ya Angyy. ...lol

Ila hio mimambo ya kusahau kuweka hamira kwenye andazi au Bp kwenye cake loh...sina hamu nayo...

Ramadhan moja nilikua mother house kabla sijaolewa na wazee hawakuepo hm kwahio mi ndo nilikua boss..lol, nikawaambia wanangu leo mukande andazi nikirudi job tunachoma..nimefikia kurudi tukakaaaaaa heee haliumuki nkaanza kumtafuta mkandaji (alikua ni mtu mzima fulani alikuja kututembelea akataka yy akande) ah nkashindwa kumwambia kitu nikabaki hivi ulikumbuka kuweka hamira ?

Nae ni mbishi wee kanikazia macho nimeweka labda mbaya tu...lol ikabidi niyachanganye tena upyaa na ilikua late badala ya andazi nikamua kusukuma km chapati..tukala chapati za sukari...mh
 
hahahahaha wapishi muna visaa....mi nikibugi simpelekei mtu pishi langu zaidi ya angyy. ...lol

ila hio mimambo ya kusahau kuweka hamira kwenye andazi au bp kwenye cake loh...sina hamu nayo...
Ramadhan moja nilikua mother house kabla sijaolewa na wazee hawakuepo hm kwahio mi ndo nilikua boss..lol, nikawaambia wanangu leo mukande andazi nikirudi job tunachoma..nimefikia kurudi tukakaaaaaa heee haliumuki nkaanza kumtafuta mkandaji (alikua ni mtu mzima fulani alikuja kututembelea akataka yy akande) ah nkashindwa kumwambia kitu nikabaki hivi ulikumbuka kuweka hamira ? Nae ni mbishi wee kanikazia macho nimeweka labda mbaya tu...lol ikabidi niyachanganye tena upyaa na ilikua late badala ya andazi nikamua kusukuma km chapati..tukala chapati za sukari...mh
lol, huo unaitwa mbadala
 
Mara ya kwanza kuandaa na kuchoma samosa

Nilivyoweka kwenye mafuta zikawa zinafunguka.... Hahaha mchanganyiko wote ukawa umesambaa
Kuumbe ile chapati na uji wa ngano ulikua mzitoo, loh
Nilichekwa sana ila "kukosea njia ndo kujua njia "
 
Umenikumbusha mbali nikiwa binti mdogo ndio najifunza kupika, mama alitoka akaniachia pishi la wali na kukaanga mchuzi wa nyama. Nikatia mafuta jikoni, moto mkali mie nakata vitunguu kidogo dogo.
Kuja kuvitia jikoni, moto si ukawaka sufuriani, kwa woga acha nimwage kila kitu, mafuta yalikuwa ndo yale yale, so ikabidi nitie vitunguu, nyanya na maji kwenye nyama nikachemsha. piga picha ya nyama ambayo haijanona, mchuzi maji matupu. Huo wali sasa - waswahili wanaita madida (wali ambao haujakauka vizuri). Aliporud, saa ya makulaji acha nigombezwe. ila baba alinisifia eti kwa vile chakula kiliiva na kililika. Sisahau hiyo stori.
Habari zenu wanajiko.

Leo ningependa tushee mambo yanayotutokea jikoni, yale ya vituko vituko.

Mie mengi yamewahi kunikuta lkn ntaweka machache tu.

Kuna siku mama yangu aliniwachia niangalie pishi la mseto, sikujua kama kabla haujaepuliwa haukorogwi na mwiko si niukoroge, wacha mseto uungue. Nligombwajeee mpk leo nimejua kama mseto haukorogwi hadi uepuliwe ndo usongwe kama ugali.

Nlikua nkikaa jikoni na mama kupika, pishi kama halijaja vizuri basi hufukuzwa jikoni ati naambiwa macho yangu ndo yameharibu, lol.

Kuna siku nlikuwa nataka kukaanga chips, nkakosea kwenye karai badala ya kuweka mafuta nkaweka siki, si muda jikoni kumejaa moshi na harufu ya ajabu kuja kuangalia kumbe nimebeba chupa ya siki badala ya mafuta.

Usiombe kuumua maandazi ukaweka sukari nyingi, utalala hata siku mbili hayajaumuka, hii mpk leo hii mi mwenzenu mara hubugi step.

Haya wana jiko hem na wengine waeleze vituko vinavowapata jikoni, au vilowahi kuwapata wakati wanjifundisha kupika, au kitu gani hupendi uwapo jikoni.
 
Kuna dada mmoja alitewa tambi na mumewe apike, kumbe hajui na hajataka kumwambia mumewena bahati mbaya basi mume alikua anakuja na wageni.

Basi imefika time ya kula wageni washakaa juu a meza mume kila akitafuta tambi hazioni. Akaona labda mkewe hajazipika, lol. Kumbe shosti tambi kishazipika kama uji. Mwisho wa siku bwana akashindwa kustahamili ikabidi akamuuliza mkewe tambi ziko wapi? Bibi, 'oooh mume wangu, leo nimekupikieni ''poza moyo'' mana naona kila siku tambi za kawaida mnakula ati' looh, kumbe bi dada pishi la tambi halijui ilibidi alishe watu tambi kwa vijiko
 
Nilikua naunga maharage ya wali jion
Wakati nachuja tui nikajisahau, yale machicha ya nazi nikayaweka kweny maharage badala ya tui,
Kuja kutahamaki doh..... acheni tu, na hakukua na mboga nyengine
Nilicharazwa na mama sitosahau.... mpaka leo hii nipo makini sana jikon
 
Kuna hiyo ya mandazi, lol
Ngoja tu ninyamaze
 
Habibty hahahahah mie hiyo ya maandazi ilowahi nikuta zaman siku mama kaenda shopping kwa ajili ya eid ilikua ramadhan nakumbuka basi akaniambia nipike maandazi yeye akirudi atakuja kuchoma....shoga nkalikanda andaaz lainiii wakat anaraudi sasa karibia maghrib anataka kuyachoma bado hayajaumuka na mie kila nkiyasubiri hayaumuki weee kumbe mesahau kutia hamira nlisemwa na makofi mawili mazuriiii lol
naamini makofi hayo mawili ndio yaliyokufanya hadi hii leo ukawa mpishi mzuri
Pole kwa mapito hayo
 
Jameni hivyo vituko jikoni ni kwa kina dada pekee. mbona sie kina kaka na baba tupo kimya, inamaana sie hatujui kupika ama ndio ladies first.
 
Pindi najifunza kupika Ugali, si nikapika mbichi, manake niliweka unga hata maji hayajachemka. We nilichokifanya ni kutupa batini kabla mtu hajaona Halafu nikaanza upya!!
ha ha haaaa, inaelekea ushatupa vingi wewe
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Jameni hivyo vituko jikoni ni kwa kina dada pekee. mbona sie kina kaka na baba tupo kimya, inamaana sie hatujui kupika ama ndio ladies first.
umeona enhee? labda wanaona haya kuchekwa
 
umenikumbusha mbali nikiwa binti mdogo ndio najifunza kupika, mama alitoka akaniachia pishi la wali na kukaanga mchuzi wa nyama. Nikatia mafuta jikoni, moto mkali mie nakata vitunguu kidogo dogo. Kuja kuvitia jikoni, moto si ukawaka sufuriani, kwa woga acha nimwage kila kitu, mafuta yalikuwa ndo yale yale, so ikabidi nitie vitunguu, nyanya na maji kwenye nyama nikachemsha. piga picha ya nyama ambayo haijanona, mchuzi maji matupu. Huo wali sasa - waswahili wanaita madida (wali ambao haujakauka vizuri). Aliporud, saa ya makulaji acha nigombezwe. ila baba alinisifia eti kwa vile chakula kiliiva na kililika. Sisahau hiyo stori.
lol, mwanzo mgumu. lakini tuseme haya na yale kwenye kupika kadri ukikosea ndo unazidi kujua zaidi kupika. ila kuna watu wakikosea mara moja tu wanakata tamaa hawarudii tena kupika kile kitu
 
lol, mwanzo mgumu. lakini tuseme haya na yale kwenye kupika kadri ukikosea ndo unazidi kujua zaidi kupika. ila kuna watu wakikosea mara moja tu wanakata tamaa hawarudii tena kupika kile kitu

Mie nkipika chakula kama hakijakuja vizuri nanunaajee
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nilivyokua 11-12yrs khaloo yangu alitualika kwake bahati mbaya ukweni wakafiwa ikabidi atuachie jiko tupike wenyewe maagizo ilikua tupike wali wa nazi na mchuzi wa maji, tulikua na mke wa my uncle nae alikua sifuri kwenye upishi...doh..ati ananiuliza mm wat to do na mm enzi hizo hata jikoni siingii loh tukaufurumusha wali ukatoka bondo ilimradi umewiva...huo mchuzi sasaa tena wa maji aunty ananiuliza unapikwaje nikamwambia weka mafuta kaanga kitunguu na tungule halafu mimina na maji ...looh mhuuu ,tukafanya hivyo wenye nyumba wamerudi wanashangaa chuzii chururuuu linang'aa mafuta... tukaulizwa ndo wa maji huu??! tukasema si ndio mumetaka mchuzi wa maji!!!
 
Back
Top Bottom