Vituko, raha na viroja vya wala mirungi

bibinnaa

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2017
Posts
1,500
Reaction score
1,378
Baada ya kujadiliana mengi kuhusu Mirungi na wala mirungi....sasa hebu tujulishane statehe zake ma madhara yake kabla hatujamuomba Mh.Msukuma kuwasilisha bungeni tena ili ihalalishwe
 
Kwakweli sijui...ila kuna jamaa yetu alikua kinyozi alikua anapenda mirungi afu anagoma kabisa kula msosi hadi siku akataka kutufia na njaa tukamtandika fimbo za kutosha lakini wapi yeye na chakula kama paka na panya..
 
Kuna mshkaji kitaa aligongwa na taxi alikuwa anavuka barabara bila tahadhari koz ya andasi ya mirungi...akavunjika mguu na mkono cha kushangaza akawa hata halii yaani traffic wamefika jamaa mashavu yamejaa gomba.! Wakasema muacheni tuu hapo ana ganzi ya hatari ya mirungi tumpeleke hospital ya Selian (Ngaramtoni) ila andasi ikiisha ganzi itakata na hapo ndipo atakapotoa kilio cha mbwa koko daah nlichoka sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…