Vituko vya utotoni

Mi na rafiki yangu tuliwahi kupewa tenda na mtoto wa mtendaji ya kufanya nyuki wahamie kwenye mzinga wake baada ya kuwa tumejifanya tunajua dawa za kuchoma na kupulizia ili kuwavutia nyuki wahamie kwenye mzinga.. Tumeshakula malipo ya awali ya kama shilingi 40 hivi maana alitupa sarafu za sh 10 kama Mara 4 hivi.. Mda ukazidi kwenda nyuki wamegoma kuhamia jamaa akaanza kumind.. Tukafikiria tufanyeje maana muda si mrefu ulikuwa unaenda kuwa msala, baadae rafiki yangu akaja na plan ilikuwa mission impossible ila hatukua na jinsi tumeshakula hela ya watu.. Lengo ilikuwa ni kuiba nyuki wa kwenye mzinga kwa jirani mmoja hivi tuwahamishie kwa jamaa.. Basi Tukapanga alhamis 1 ndo tufanye tukio, basi kila mmoja akatafuta excuse hatukwenda shule.. Tukawawinda wale majirani wenye mzinga walivobeba majembe kwenda shambani tukastuana tukatimba eneo la tukio jamaa akajitolea kamfuko kake ka sport ka daftari ndo tuwabebee nyuki.. Basi tumefika pale nikapanda na kile kimfuko nikavunja upande mmoja nikazoa lundo nikapakia kwenye kimfuko nikakabana.. Aisee nyuki waliniuma mpaka nikajikuta nadondoka mimi chini na mfuko chini ila kama askari wa miavuli nimefika chini nimeteguka mguu jamaa kapita na kimfuko kakimbia nacho huku kundi lingine la nyuki likimkimbiza kaenda hadi kwenye mzinga wa jamaa kafungua kawamwaga mle kafunika mzinga ulikuwa yale masanduku ya mbao.. Mimi huku nyuma ilibidi nikimbie tu pamoja na maumivu maana nyuki walikuwa wana niuma mpaka basi.. Nikafika sote tunanundu ila kazi tumeimaliza.. wazazi wangu wakaniamshia msala baada ya kuona nimerudi nyumbani nachechemea huku na manundu ya nyuki ikabidi niwaeleze ukweli wakanichapa ila badae mama akanipeleka dispensary.. jamaa hakumalizia malipo maana nyuki hawakukaa mule hata siku 5 maana kumbe malkia wao tulimuacha kwenye ule mzinga tuliouhujum
 
1.niliiba ndala za mgeni nikazichonga matairi ya gari la mbao!.

2. nilipiga baruti saa 3 usiku! watu wakajua majambazi, kila mtu akakimbilia ndani.. mm na mshkaji wangu tukaenda hadi kwenye kibanda cha chipsi tukaiba paja la mbuzi, yale wanaoning'inizaga na mishkaki yote!. kesho yake tuligundulika, mwenye kibanda akatupeleka polisi eti watoto wa mtaani majambazi dah!?.
 
Mimi nliyokuwa chekechea nlikuwaga nnasukwa nywele , watu wananisifia nimependeza, nlivyotaka kuingia la kwanza ikabidi ninyolewe kwa sababu shule niliyoingia darasa la kwanza ilikuwa ikikataza kusuka.

Nakumbuka wenzangu walikuwa kila wakiniona wananicheka so nikawa Nina hasira Sana, nikapanga kulipiza kisasi kwa mtoto mwenye nywele yeyote nifanye njama ya kumuharibu nywele zake.

Sasa siku moja akaja mgeni , alikuja na katoto ka kike kadogodogo Ila hakajui kuongea vizuri kamebanwa nywele zake vizuri kichwani kamewekewa vidolidoli watu wanamsifia.

Wivu ukaniingia nikaamua kwenda kwa mangi nikanunua big G nikaitafuna vizuri afu nikakadanganya katoto twende tukacheze, tulipokuwa tukicheza nilikasokomeza Ile big G kwenye nywele zake, zikajifungafunga, mama yake Yule mtoto alisikitika sana. Ikabidi wampunyue pale kichwani penye big G. Mm nikasema Yan hata sijui hii big G kaitoa wapi.
Na hawakujua km Ni mm.

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hakuna kitu kilikuwa kinaniuma kama umepambana umefanikiwa mudokoa mboga halafu unakuta ni nyanya chungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…