Keagan Paul
JF-Expert Member
- Jul 19, 2018
- 510
- 3,178
- Thread starter
-
- #21
Inaendelea
Kitendo cha kumuona pale Mbele kilinishtua sana na kunitoa nje ya Mchezo. Pale mbele tayari Wasindikizaji wetu (Mates) 12 walikuwepo, Mziki ukafunguliwa pale tukaendelea kucheza.
Watu wote wakaungana na sisi katika kucheza. Wakati tunaendelea kucheza nikamstua rafiki yangu mmoja, nikamwambia nisaidie vitu viwili, chukua glass pita kimya kimya kaniwekee pombe bila mtu yoyote kujua. Nilimwomba hivi sababu nilijua kama pombe ingeisha kichwani nisingeweza kuwakabili hawa watu wawili.
Jamaa alifanya kama nilivyomuomba. Huyu jamaa angu alikuwa anajua kila kilichokuwa kikiendelea. Katikati ya kucheza mziki, ghafla namuona X wangu yule wa Kitengo huyu hapa pamoja na Wazazi wake. Nikawa nazuga zuga tu pale. Moyoni nikawa nasema hapa bila pombe sitoboi, hata kucheza mziki ni kama nilianza kupoteza step.
Jamaa yangu alivyorudi na kunikabidhi glass ya pombe kiaina bila watu kujua, nikamwambia jamaa yangu sikia, ebhana fanya kila unavyoweza kamtoe fulani pale kwenye Meza ya Wazazi. Ongea nae kwa namna utakayoweza wewe lakini pale atoke. Jamaa angu akatikisa kichwa na kuondoka.
Baada ya nyimbo mbili tatu, watu wote wakarudi zao Kukaa. Sasa shughuli ndo inaanza rasmi, sara na utambulisho. Kutupa Jicho pale meza Kuu, namuona Bibie bado amekaa pale pale.
Moyoni nikasema huyu anataka kuniaribia shughuli, anataka kunikosesha furaha tu na mimi siwezi kukubali kukosa furaha kwenye siku yangu kubwa kama hii. Hapo tayari pombe zimekubali kichwani. Nawaza tu kama nitaweza hata kutambulisha watu vizuri kwa mpangilio mzuri.
Nikajikaza nikaanza kutambulisha waliokaa Meza Kuu. Meza kuu kulikuwa na watu wanafika hata 15 pamoja na ndugu zangu waliotoka Mikoani na Vijijini.
Nikaanza kutambulisha pale, Bibie alikuwa amekaa pembeni ya Bibi yangu mzaa Baba, utambulisho ulivyofika kwake nikamruka nikaendelea kutambulisha wageni wengine mpaka nikamaliza watu wote. Nashukuru Mungu zoezi la Kutambulisha watu lilipita salama, japo mdomo ulikuwa mzito kidogo kutokana na nilikuwa nimeshalewa. Ila nadhani wadau hawakujua.
Ratiba nyengine zikaendelea mle Ukumbini. sasa kutokana na pombe nilizokuwa nimeanza kunywa tangu Beach, nilijisikia hali ya kwenda toi. Nikamshtua Bibi Harusi.
Watu wakati wanaendelea kucheza Mziki nikatoroka kidogo kwenda Toi.
Kumbe yule demu ni kama muda wote alikuwa ananiangalia mimi, maana nilivyotoka tu Toi huyu hapa. Kanifata na kunishika Mkono, amekunja sura, nikamuomba twende pembeni tukaongee.
Watu walikuwa busy wanapita pita. Tukatoka hadi nje kabisa ya ukumbini, sehemu moja kwenye giza karibu na magari, pembeni ya Costa tukasimama. Akaanza kuongea kwa jazba pale.
βI just came to tell you that I hate you, I hate youβ
Demu akanikunja suti yangu, huku analia.
Kitendo cha kumuona pale Mbele kilinishtua sana na kunitoa nje ya Mchezo. Pale mbele tayari Wasindikizaji wetu (Mates) 12 walikuwepo, Mziki ukafunguliwa pale tukaendelea kucheza.
Watu wote wakaungana na sisi katika kucheza. Wakati tunaendelea kucheza nikamstua rafiki yangu mmoja, nikamwambia nisaidie vitu viwili, chukua glass pita kimya kimya kaniwekee pombe bila mtu yoyote kujua. Nilimwomba hivi sababu nilijua kama pombe ingeisha kichwani nisingeweza kuwakabili hawa watu wawili.
Jamaa alifanya kama nilivyomuomba. Huyu jamaa angu alikuwa anajua kila kilichokuwa kikiendelea. Katikati ya kucheza mziki, ghafla namuona X wangu yule wa Kitengo huyu hapa pamoja na Wazazi wake. Nikawa nazuga zuga tu pale. Moyoni nikawa nasema hapa bila pombe sitoboi, hata kucheza mziki ni kama nilianza kupoteza step.
Jamaa yangu alivyorudi na kunikabidhi glass ya pombe kiaina bila watu kujua, nikamwambia jamaa yangu sikia, ebhana fanya kila unavyoweza kamtoe fulani pale kwenye Meza ya Wazazi. Ongea nae kwa namna utakayoweza wewe lakini pale atoke. Jamaa angu akatikisa kichwa na kuondoka.
Baada ya nyimbo mbili tatu, watu wote wakarudi zao Kukaa. Sasa shughuli ndo inaanza rasmi, sara na utambulisho. Kutupa Jicho pale meza Kuu, namuona Bibie bado amekaa pale pale.
Moyoni nikasema huyu anataka kuniaribia shughuli, anataka kunikosesha furaha tu na mimi siwezi kukubali kukosa furaha kwenye siku yangu kubwa kama hii. Hapo tayari pombe zimekubali kichwani. Nawaza tu kama nitaweza hata kutambulisha watu vizuri kwa mpangilio mzuri.
Nikajikaza nikaanza kutambulisha waliokaa Meza Kuu. Meza kuu kulikuwa na watu wanafika hata 15 pamoja na ndugu zangu waliotoka Mikoani na Vijijini.
Nikaanza kutambulisha pale, Bibie alikuwa amekaa pembeni ya Bibi yangu mzaa Baba, utambulisho ulivyofika kwake nikamruka nikaendelea kutambulisha wageni wengine mpaka nikamaliza watu wote. Nashukuru Mungu zoezi la Kutambulisha watu lilipita salama, japo mdomo ulikuwa mzito kidogo kutokana na nilikuwa nimeshalewa. Ila nadhani wadau hawakujua.
Ratiba nyengine zikaendelea mle Ukumbini. sasa kutokana na pombe nilizokuwa nimeanza kunywa tangu Beach, nilijisikia hali ya kwenda toi. Nikamshtua Bibi Harusi.
Watu wakati wanaendelea kucheza Mziki nikatoroka kidogo kwenda Toi.
Kumbe yule demu ni kama muda wote alikuwa ananiangalia mimi, maana nilivyotoka tu Toi huyu hapa. Kanifata na kunishika Mkono, amekunja sura, nikamuomba twende pembeni tukaongee.
Watu walikuwa busy wanapita pita. Tukatoka hadi nje kabisa ya ukumbini, sehemu moja kwenye giza karibu na magari, pembeni ya Costa tukasimama. Akaanza kuongea kwa jazba pale.
βI just came to tell you that I hate you, I hate youβ
Demu akanikunja suti yangu, huku analia.