Mwanongwa
JF-Expert Member
- Feb 15, 2023
- 611
- 567
Kama mwenendo wa kujiandikisha Kwenye daftari la mkazi kwaajili ya kupiga kura Kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa unasua sua hivi,vipi uchaguzi mkuu mwakani?
Wananchi wengi katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mbeya nikama wamesusia zoezi hili la kujiandikisha wakidai ni kupoteza muda wao tu.
Huku makalani wanaoandikisha wakiwa muda mwingi wanapiga soga tu kutokana na uchache wa wananchi wanaojitokeza.
Story zilizopo mitaani ni kwamba kile ambacho kilitokea wakati wa uchaguzi kama huu wa serikali za mitaa mwaka 2019 Cha wagombea wa chama kimoja kupita maeneo mengi bila kupingwa ndiyo sababu ya wananchi kutojitokeza kwa wingi kujiandikisha.
Leo nimepita Kwenye baadhi ya mitaa na kujionea hali ilivyo,licha ya hamasa kubwa ya viongozi wa vyama na serikali kuhamasisha lakini hali ni Tete.
Soma Pia: Special Thread: Hali ya Vituo vya Kujiandikisha kupiga Kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 kwa Picha na Video
Mitaa kama Ivumwe,Mwakibete,Ntundu,Itezi,Iduda,Tonya,Ituha na mingine mingi, Makalani Wanapiga soga tu huku wengine wakiwa wanauchapa usingizi.
Wananchi wanasema vyovyote itakavyokuwa kwao ni sawa tu lakini kwenda kujiandikisha ni kupoteza muda wao
Vituo vingi vimekuwa havina idadi kubwa ya wananchi ambao wanajiandikisha.
Wananchi wenzangu tujitokeze Kwa wingi kujiandikisha ili tuitumie haki yetu ya msingi ya kuchagua viongozi tunaowataka watuongoze Kwa kipindi Cha miaka mitano ijayo
Wananchi wengi katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mbeya nikama wamesusia zoezi hili la kujiandikisha wakidai ni kupoteza muda wao tu.
Huku makalani wanaoandikisha wakiwa muda mwingi wanapiga soga tu kutokana na uchache wa wananchi wanaojitokeza.
Story zilizopo mitaani ni kwamba kile ambacho kilitokea wakati wa uchaguzi kama huu wa serikali za mitaa mwaka 2019 Cha wagombea wa chama kimoja kupita maeneo mengi bila kupingwa ndiyo sababu ya wananchi kutojitokeza kwa wingi kujiandikisha.
Leo nimepita Kwenye baadhi ya mitaa na kujionea hali ilivyo,licha ya hamasa kubwa ya viongozi wa vyama na serikali kuhamasisha lakini hali ni Tete.
Soma Pia: Special Thread: Hali ya Vituo vya Kujiandikisha kupiga Kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 kwa Picha na Video
Mitaa kama Ivumwe,Mwakibete,Ntundu,Itezi,Iduda,Tonya,Ituha na mingine mingi, Makalani Wanapiga soga tu huku wengine wakiwa wanauchapa usingizi.
Wananchi wanasema vyovyote itakavyokuwa kwao ni sawa tu lakini kwenda kujiandikisha ni kupoteza muda wao
Vituo vingi vimekuwa havina idadi kubwa ya wananchi ambao wanajiandikisha.
Wananchi wenzangu tujitokeze Kwa wingi kujiandikisha ili tuitumie haki yetu ya msingi ya kuchagua viongozi tunaowataka watuongoze Kwa kipindi Cha miaka mitano ijayo